• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Maagizo ya Waziri Mkuu aliyoyatoa Idodi yatekelezwa

Imewekwa : October 2nd, 2019


Maagizo  aliyoyatoa Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Kassim alipokuwa ziarani Mkoani Iringa katika Kijiji cha Idodi Halmashauri ya Wilaya ya Iringa  yametekelezwa.

Wataalamu kutoka Idara ya Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wakiongozwa na Mkuu wa Idara hiyo Bw. Evidence Machenje walifika katika Kijiji cha Kitisi (Idodi)  siku ya Jumatatu tarehe 30.09.2019 na kufanya mkutano na Wajumbe wa Halmashauri za Vijiji viwili vyenye Mgogoro wa kimpaka ambavyo ni Kitisi na Mapogoro ili kufikia muafaka wa mgogoro huo wa muda mrefu wa kugombea mpaka.

Wajumbe wa Vijiji vyote viwili walikubaliana kukaa kikao cha pamoja siku ya Jumatatu tarehe 07.10.2019 ili kupitia upya mpaka kati ya Vijiji vyao ambao unaleta mgogoro, na makubaliano watakayokuwa wamefikia katika kikao hiko yapelekwe kwa Mkuu wa Idara ya Ardhi wa Halmashauri ili arudi tena Kijijini hapo kuweka rasmi mpaka watakaokuwa wameridhia Vijiji vyote viwili, ambapo Mkuu wa Idara ya Ardhi ameomba kabla ya tarehe 15.10.2019 awe amepata makubaliano yao kwa ajili ya kuumaliza mgogoro huo na kupeleka taarifa kwa Mhe. Waziri Mkuu.

Aidha Maafisa wa Polisi walifika katika Kijiji cha Idodi Siku ya Jumatatu tarehe 30.09.2019 na kuwakamata Viongozi wa Jumuiya ya Watumia maji ya Matunguru ambao wanatuhumiwa kufanya ubadhirifu wa shilingi milioni 7.

Katika Ziara yake Mkoani Iringa tarehe 28.09.2019 Mhe. Waziri Mkuu alliongea na Wananchi wa Kijiji cha Idodi katika Mkutano wa hadhara, ambapo katika Mkutano huo ziliibuka tuhuma dhidi ya Viongozi wa Jumuiya ya Watumia maji kutafuna shilingi milioni 7, hali iliyopelekea  Mhe. Waziri Mkuu kutoa maagizo ya kukamatwa kwa Viongozi wote wa Jumuiya hiyo waliojihusisha na ubadhirifu huo.

Pia liliibuka sakata la mgogoro wa kimipaka wa muda mrefu kati ya Vijiji vya Kitisi na Mapogoro, ambapo Mhe. Waziri Mkuu alimwagiza Mkuu wa Idara ya Ardhi wa Halmashauri kufika mara moja Kijijini hapo na kutatua mgogoro huo.

Matangazo

  • Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. September 23, 2019
  • Tangazo la kuanza kwa Zoezi la Uandikishaji Wapiga Kura tarehe 08.10.2019 October 04, 2019
  • Tangazo la kuhama kwa Makao Makuu ya Halmashauri October 25, 2019
  • Kila la Kheri Kidto cha nne 2019 November 04, 2019
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Wananchi Wapongeza Juhudi za Halmashauri katika Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Iringa.

    December 03, 2019
  • Shirika la SOS latoa Msaada wa shilingi Milioni 23 kwa Wanafunzi wanaoishi kwenye mazingira magumu.

    December 02, 2019
  • Mgogoro wa Kimipaka uliodumu muda mrefu kati ya Vijiji vya Mboliboli na Makuka watatuliwa.

    December 02, 2019
  • Tatizo la Maji Kijiji cha Magombwe kubaki Historia- Mhe Hapi

    December 01, 2019
  • Tazama zote

Video

UZINDUZI WA CHANJO YA SURUA RUBELLA MKOANI IRINGA
video

Viungo vya haraka

  • Dashibodi ya Mapato
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Gangilonga

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0754 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa