• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Education

Halmashauri ya wilaya ya Iringa hadi kufikia Disemba 2014 ina jumla ya shule za awali 113, Elimu maalum 1, Shule za msingi 146 na Vituo vya ufundi stadi 2 kwa mchanganuo ufuatao:-

  • Wanafunzi wa Awali 8090 ambapo wavulana 4050, wasichana 4040
  • Wanafunzi walemavu 57 kati ya hao wasioona ni 28, Walema wa viungo 14, Bubu viziwi 10 na walemavu wa akili 5.
  • Mahitaji ya Walimu  ni 1473 waliopo ni 1358 wanaume 649 na wanawake 709
  • Mahitaji ya vyumba vya madarasa 1473 yaliyopo 1238 upungufu 235
  • Kwa nyumba za walimu mahitaji ni 1473 zilizopo 611 upungufu 862
  • Mahitaji ya matundu ya vyoo ni 2730 yaliyopo 1824 upungufu 906
  • Mahitaji ya madawati ni 29457 yaliyokuwepo 18490 pungufu 10967

 

Mafanikio

 

  • Shule 113 za msingi kati ya 146 zina madarasa ya awali
  • Uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la kwanza umefikia 99.8% kwa kuwasajili wanafunzi 9474 ambapo wavulana ni 4856 na wasichana ni 4618
  • Kiwango cha ufaulu katika elimu ya msingi darasa la saba kimezidi kuimarika kutoka 62.19% mwaka 2013 hadi kufikia 68.23% mwaka 2014
  • Kuhusu miundombinu ya elimu ya awali kwa wanafunzi walemavu inaboreshwa kwa kujengewa mabweni ya kisasa kulingana na mahitaji yao.
  • Vituo viwili vya ufundi stadi vinaendelea kutoa wahitimu wa ufundi wa fani za ujenzi ambao hatimaye huwawezesha kujiajili wenyewe.

 

Changamoto

  • Ukosefu wa fedha za ujenzi/ukarabati wa vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, matundu ya vyoo na kununulia madawati.
  • Ukosefu wa vyombo vya ufundi (Handtools) kwa fani za uwashi, useremala, sayansikimu na umeme.
  • Ukosefu wa chombo cha usafiri kwa ufuatiliaji wa taaluma katika shule za msingi, vituo vya awali, elimu maalum na vituo vya ufundistadi.
  • Upungufu wa vifaa/zana za kufundishia na kujifunzia.

 

 

 

 

 

 

 

Sekta ya Elimu ya Sekondari.

 

Halmashauri kupitia Sekta ya  Elimu Sekondari  imeendelea kutekeleza kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusimamia ujenzi wa maabara 84 za masomo ya Sayansi, ujenzi wa hosteli ya wasichana shule ya sekondari Kalenga, ujenzi wa Hosteli ya Wasichana hatua ya kwanza Shule ya Sekondari Dimitriusi, Kuwapokea wanafunzi wa kidato cha tano, kufanya ufuatiliaji wa Taaluma katika Shule za Sekondari 28 pamoja na kusimamia ukarabati wa karakana ya kufundishia masomo ya Ufundi katika Shule ya Sekondari Ifunda ufundi.

Kumalizia ujenzi wa maabara tatu za masomo ya Sayansi kwa kila    shule

Halmashauri kupitia Idara ya Elimu sekondari imefanikiwa kukamilisha ujenzi wa maabara 84 za masomo ya sayansi. Ambapo Maabara 37 zimekamilika kujengwa na ambazo zinatumika kwa masomo ya Kemia na Baiolojia, maabara 4 bado zipo katika hatua za mwanzo za ujenzi. Maabara 43 zipo katika hatua ya umaliziaji ikiwa ni pamoja na kupiga lipu kufunga milango na madirisha. Jumla kuu ya michango kwa ajili ya ujenzi wa maabara ni Tshs. 355,160,000

   Ujenzi wa Hosteli ya wasichana shule ya sekondari Kalenga.

 

Halmashauri imefanikiwa kukamilisha Ujenzi wa Hosteli ya wasichana shule ya Sekondari Kalenga. Ujenzi umegharimu kiasi cha Tshs 258,000,000.00 mpaka kukamilika na inatumika. Hosteli hiyo ina uwezo wa kuchukua wanafunzi 120.

 

Ujenzi wa Hosteli ya wasichana hatua ya kwanza shule ya sekondari Dimitrius.

 

Halmashauri imejenga Hostel moja ya wasichana katika Shule ya Sekondari Dimitrious. Ujenzi wa hatua ya kwanza wa Hostel hii umekamilika na umefikia hatua ya kupauliwa. Ujenzi huu wa Hostel umegharimu Jumla ya Tshs 70,000,000 na awamu ya pili ya kumalizia ujenzi utaendelea mwaka wa fedha 2015/2016.

 

 Mapokezi ya wanafunzi wa Kidato cha Tano.

 

Idara ya Elimu Sekondari imepangiwa jumla ya wanafunzi 2389 wa Kidato cha tano katika Shule zake sita.

Idadi ya wanafunzi wa Kidato cha tano kwa 2014/2015 imeongezeka kutoka 1433 mpaka 2389 sawa na  asilimia 156% ukilinganisha na idadi ya wanafunzi waliopokelewa  mwaka 2013/2014. Ongezeko la idadi ya wanafunzi hao katika Shule za Sekondari za Halmashauri ya Wilaya ya Iringa linaonyesha namna Halmashauri inavyochangia kwa kiasi kikubwa kutoa nafasi za wanafunzi kupata elimu ya kidato cha sita.

Ufuatiliaji wa Maendeleo ya Taaluma  katika Shule ya Sekondari za 

     Muhwana, Isimila, Kiwere na Ifunda Ufundi.

Halmashauri imefanya ufuatiliaji wa ufundishaji na Maendeleo ya Taaluma katika Shule za Sekondari 28 za Halmashauri yetu. Zoezi la ufuatiliaji limefanyika ili kuona hali halisi ya ufundishaji pamoja na matumizi ya fedha ya ruzuku. Baada ya zoezi hilo wakuu wa Shule hizo pamoja na walimu waliagizwa kusimamia vizuri matumizi ya fedha za Ruzuku pamoja na ufundishaji na ujifunzaji ili kuinua taaluma Shuleni.

Kusimamia ukarabati wa karakana ya kufundishia masomo ya ufundi katika shule ya Sekondari ya ufundi Ifunda.

 

Halmashauri imesimamia kufanyika kwa ukarabati wa karakana ya kufundishia masomo ya ufundi katika shule ya Sekondari ya ufundi Ifunda. Ukarabati huo upo katika hatua za mwisho na umegharimu Tsh 355,000,000.00 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa