• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Baadhi ya Watendaji, Waratibu na Wakuu wa Shule pichani wakiwa kwenye kikao kazi kilichoitishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halamshauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja

Imewekwa : October 7th, 2021

DED Iringa  ateta na Watendaji, Waratibu na Wakuu wa Shule

Ummi Mohamed na Antoni Ramadhani (Ofisi ya Habari na Uhusiano-Iringa DC)

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja Oktoba 6 mwaka huu amekutana na Watendaji wa Kata,Waratibu wa elimu na Wakuu wa shule kwa lengo la kupitia na kuweka maandaliza mazuri kwa ajili ya miradi na kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2022.

Akizungumza katika kikao kazi hiko Wakili Muhoja amesema pamoja na kutambua kazi nzuri wanazofanya lakini wanatakiwa kujiwekea mipango mizuri itakayopelekea kutokuwepo na changamoto ya upungufu wa madawati katika shule zao.

“Namshukuru sana Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Samia Suluhu Hassan kwa kuona changamoto ya madarasa katika maeneo mengi na sisi Halmashauri ya Wilaya ya Iringa tupo katika neema ya madarasa hayo tuna mshukuru sana”alisema na kuongeza;

Kuhusu maandalizi ya Miradi Mkurugenzi amesema kuwa anatarajia kuanza kutembelea shule zote hivi karibuni na amewataka watendaji na waalimu kujiandaa na kuwaandaa watoto. Aidha ameongezea kwa kutoa rai juu ya matumizi sahihi ya fedha.

“Wengine wanajiuliza kwa nini tunazungumzia fedha ambazo hata bado hazijafika, ni vizuri kuanza maandalizi mapema kwa sababu hatuna muda, lakini pia ni lazima kuzingatia matumizi sahihi ya fedha”

Amewataka pia Waalimu wakafanye maandalizi mazuri kwa wanafunzi ili waweza kufanya vyema mitihani yao kwa kutumia yale waliofundishwa kwa kipindi cha miaka mine kwa kidato cha nne. na miaka miwili kwa kidato cha pili na sio kuwafundisha ama kuwaandaa kufanya mitihani hiyo kwa udanganyifu.

Nae Afisa Elimu Sekondari wa Wilaya Mwl.Hamis Mapoto amesema katika mtihani wa utamilifu matokeo hayakuwa mazuri hususani kidato cha pili kwa kuwa na ufaulu wa 58% na GPA 4.08 huku kidato cha nne wakiwa na ufaulu wa asilimia 92.9 na GPA ya 3.55.

“Matarajio yetu ilikuwa ni watoto wafaulu zaidi ya hayo matokeo, walimu tusibweteke tuwe karibu na watoto wetu na kuwapatia msaada wa kila hali ili wafaulu vyema kama ambavyo tumetarajia na kuwawezesha kufanya mitihani kwa kijiamini na sio kuibia.” alisema.

Aidha Mwl.Mapoto aliwapongeza na kuwataka wafanye kazi zote kwa kushirikiana ili kubaini kama kuna changamoto zinazowakabili wanafunzi na kuzipatia ufumbuzi mapema kabla hazijaathiri maandalizi ya wanafunzi au mwananfunzi husika.

Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kama Halmashauri zingine zinakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo uhaba wa madawati na vyumba vya madarasa.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa