Mamia ya waombolezaji wajitokeza kumsindikiza kwenye safari yake ya mwisho ndugu yetu Mhe. Felix Waya aliyekuwa Diwani wa kata ya Kiwele katika kijiji cha Mgera Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mei 26, 2025.
Shughuli ya mazishi imeongozwa na viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali Mkoani Iringa akiwemo Mwenyekiti CCM Mkoa wa Iringa ndugu Daudi Yasin, wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Salim Abri Asas na Mhe. Richard Kasesela
Kwa upande wa Serikali Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Kheri James, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mhe Steven Mhapa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ndugu Robert Masunya na watumishi wengine wa Halmashauri ya Wilaya wameshiriki mazishi hayo.
Diwani Felix Waya alifarika ghafla baada ya kuanza kuumwa muda mfupi baada ya kumaliza kuhutubia mkutano wa hadhara kwenye muendelezo wa ziara ya CCM mkoa wa Iringa kwenye kata hiyo.
Marehemu Felix Antony Waya amepumzishwq nyumbani kwake Kijiji cha Megara kilichopo katika kata ya Kiwele wilayani Iringa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ndugu Robert Masunya anatoa pole sana kwa wote walioguswa na msiba huu ambao pia ni pengo kwa Halmashauri, marehemu apumzike kwa amani.
https://www.instagram.com/p/DKJfyx0MMHG/?igsh=cWYxbTE0N29mMmRt
Kijiji cha Ihemi
Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa
Simu ya mezani: 026-2702828/2702585
Simu ya mkononi: 0757 364 994
Barua pepe: ded@iringadc.go.tz
Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa