• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Care International waadhimisha kilele cha siku ya wakulima

Imewekwa : April 11th, 2025

Care International Waadhimisha Kilele Cha Siku ya Wakulima 


Care Internatinal ni Shirika lisilo la Kiserikali ambalo husaidia wakulima na Wajasiriamali na kuwawezesha kazi za mikono na kuwatafutia masoko.

Wadau wa Care wamekuwa msaada mkubwa katika kuwawezesha wakulima kuwapa mafunzo ya namna ya kulima kwa tija na kupata Mazao mengi na kutoa ushauri.

Katika kutekeleza majukumu yao Care wameadhimisha Siku ya Mkulima kwa kwenda kukagua shamba darasa ambalo lilipandwa zao la soya kwa Mkulima na Mjasiriamali

Hafla ya Kilele cha Mkulima imefanyika Aprili 11, 2025 katika Kata ya Mgama Kijiji cha Mgama kwa kualika Wadau mbalimbali kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine na Mbeya, na Wadau wengine kutoka sehemu mbalimbali.

Akiongea katika sherehe hizo Bwana Habibu Robert Masanja Meneja wa Mradi wa Care amesema, katika kutimiza malengo ya mkulima tuliweka vigezo nane ambayo ni kama njia ya kumuongoza mkulima kuwa, kuwawezesha vikundi na Maafisa Ugani ili waweze kufanya kazi kwa pamoja, kufanya ufuatiliaji kile kilichofundisha, suala zima la lishe, suala la jinsia hasa mwanaume  mwenye mtazamo chanya, kufuatilia akiba na mikopo kwa vikundi, kukabiliana na tabia ya nchi ili mkulima aweze kulima kulingana na wakati, kutafuta masoko na ushawishi kwa Wadau mbalimbali.

Pamoja na hayo lengo la Care ni kufikisha mashamba darasa 800 ndani ya miaka mitatu ili wakulima waweze kujifunza kwa ukaribu zaidi.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri wa Wilaya ya Iringa Mheshdimiwa Stephen Mhapa ambaye alikukwa Mgeni Rasmi katika Hafla hiyo amesema, “Shughuli ya kuelimisha wananchi ni ya Serikali lakini Wadau hawa wa Care wamejitokeza kuja kutushika mkono, hivyo sisi kama Serikali ni muhimu tuwaunge mkono na kuwaonesha njia. Pia vikundi hivi nashauri waombe mkopo ili waweze kutimiza kazi zao za ujasiriamali kama kununua mashine za kukamulia mafuta ili kuepukana na kwenda mbali kwa ajili ya kupata huduma hiyo”.

Mheshimiwa Mhapa ameendelea kusema kuwa, “nawakumbusha wakulima kuendelea kufuata ushauri kupitia mashamba darasa ili tulime kwa tija na tuongeze uchumi”.

Wananchi wameishukuru Care kwa kuja katika kijiji chao kuwafundisha kilimo cha kisasa chenye tija, na kuahidi kufuata mafunzo na ushauri waliopata.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa