• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

CMT Yafanya Ziara Kukagua Miradi kwa Robo ya Kwanza, 2023/2024

Imewekwa : October 17th, 2023

CMT Yafanya Ziara Kukagua Miradi Kwa Robo ya Kwanza, 2023/2024

Kamati ya Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, imefanya ziara kukagua miradi Oktoba 16, 2023 kwa Robo ya Kwanza Julai – Septemba, kwa Mwaka wa Fedha 2023/2023.

Kamati hiyo ambayo inaongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wakili Bashir Muhoja, imetembealea miradi iliyokamilika na ambayo bado haijakamilika na kuwa ujenzi wake bado unaendelea.

Miradi iliyotembelewa ni kama Shule ya Sekondari Lufita, Kata ya Luhota, ambapo inajengwa nyumba ya Watumishi (2 in 1), ambapo Serikali ya Rais Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan ilileta fedha kiasi cha Milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hiyo. Hadi sasa zimetumika Milioni 69.186 na kwamba ujenzi wake umefikia asilimia 50. Ujenzi ulianza Septemba 05, 2023 na unategemewa kukamilika Oktoba 30, 2023.

Aidha Kamati iliweza kutembelea Shule ya Msingi Itagutwa katika Kata ya Kiwele. Shule hii ilipewa fedha kiasi cha Milioni 40 kwa ajili ya ukarabati wa madarasa manne. Ukarabati huo utaanza mara baada ya mchakato wa uzabuni kukamilika.

Vilevile Kamati iliweza kutembelea Shule ya Sekondari mpya ya Weru ambayo ipo Kata ya Ulanda. Shule hii imejengwa kwa mpango wa SEQUIP, wa kujenga shule ambazo unajenga shule mpya ili kupunguza umbali mrefu kwa wanafunzi. Shule hii itawasaidia wanafunzi wanaotarajia kuanza Kidato cha Kwanza 2024 wa Kijiji cha Kibebe, Mwambao, Weru na Lipalama ‘B’, ambapo mwanzo walikuwa wanapangwa kwenda shule ya Sekondari Kalenga. Kiasi cha Milioni 583.128 na hadi sasa kiasi cha Milioni 527.503 kimetumika kujenga shule hiyo yenye madarasa 8, Jengo la Utawala, Maabara 3 (Kemia, Fizikia na Baologia), vyoo vya Walimu na vyoo vya wanafunzi. Nguvu za wananchi wamechangia kiasi cha Milioni 2.230. Mradi ulianza Agosti, 2023 upo hatua za mwisho na umefikia asilimia 90.

Kamati pia iliweza kutembelea Shule ya Sekondari Tosamaganga ambapo kulikuwa na ujenzi wa Bweni lenye thamani ya Milioni 130, Madarasa 3 Milioni 75 na ujenzi wa vyoo Milioni 12. Ujenzi ulianza Juni, 2023 na umekamilika Agosti 23, 2023 kwa asilimia 100 kwani majengo yote yanatumika.

Shule ya Msingi Wenda iliyopo Kata ya Mseke, ambapo imepewa kiasi cha Shilingi Milioni 60 kwa ajili ya ukarabati wa madarasa matatu. Ukarabati utaanza mara moja baada ya mchakato wa uzabuni kukamilika.

Shule ya Msingi Tarajiwa ya Kilimahewa (Kibaoni) iliyopo Kata ya Ifunda, imejengwa kwa Mpango wa Boost. Kiasi cha Milioni 347.5 kimetumika kujenga shule hiyo ambapo ujenzi ulianza Juni 01, 2023. Majengo hayo yataanza kutumika Januari, 2024. Hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 98. Shule hii itasaidia kupunguza umbali mrefu wa watoto ambapo wanakwenda shule ya Msingi Kibaoni.

Kamati ilifanya hitimisho la ziara yake katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Ifunda iliyopo Kata ya Ifunda. Hapo kulikuwa na ujenzi wa bweni, madarasa na vyoo kwa Mpango wa Barick. Ujenzi ulianza Juni 20, 2023 na umekamilikwa kwa asilimia 100 Septemba 2023, na majengo yote yanatumika.

 

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa