DC IRINGA AFANYA ZIARA TARAFA YA ISMANI
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe Kheri James amefanya ziara katika Tarafa ya Ismani ikiwa ha lengo la kukagua miradi ya maendeleo, kuhamasisha maendeleo, kusikiliza na kutatua kero za wananchi Mei 15, 2025.
Huu ni mwendelezo wa ziara ya kijiji kwa kijiji ambapo tayari tarafa ya Idodi, na Pawaga na sasa Tarafa ya Ismani.
Maeneo yaliyotembelewa kwenye ziara hii ni ujenzi wa kituo cha afya Malengamakali katika kijiji cha Mkulula ambapo pia ulifanyika mkutano wa hadhara kusikiliza na kutatua kero za wananchi, mkutano wa hadhara katika kijiji cha Ilambilole kata ya Kising'a na ukaguzi wa ujenzi wa mabweni mawili ya wanafunzi katika shule ya sekondari Izazi sanjari na mkutano wa hadhara katika kijiji cha Izazi.
Aidha katika mikutano ya hadhara iliyofanyika, wananchi wameelimishwa na kuhamasishwa juu ya suala la umuhimu wa lishe bora kwa watoto, akina mama wajawazito na vijana, umuhimu wa elimu kwa watoto, matumizi bora ya ardhi na wito kwa wananchi kufanya kazi ili kujipatia kipato.
#iringaimaratutaijengakwaumojanauwajibikaji
https://www.instagram.com/p/DJtByuRM3Y5/?igsh=bm5ub3R2MnBvcWl4
Kijiji cha Ihemi
Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa
Simu ya mezani: 026-2702828/2702585
Simu ya mkononi: 0757 364 994
Barua pepe: ded@iringadc.go.tz
Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa