• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC Moyo Aagiza Watoto Kupatiwa Chakula Mashuleni

Imewekwa : October 21st, 2022

DC Moyo Aagiza Watoto Kupatiwa Chakula Mashuleni

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Mohammed Moyo ametoa maagizo hayo katika kikao cha tathmini ya mkataba wa lishe kwa robo ya kwanza (Julai - Septemba 2022) kilichofanyika terehe 21.10.2022 katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Iringa.

Amesisitiza na kutoa maagizo kwa watendaji walipokuwa wakisaini mkataba wa lishe na Mkurugenzi Mtendaji kuhakikisha kuwa mkataba wa lishe uendane na hali halisi kwa kuhakikisha kuwa kila shule inatoa chakula kwa wanafunzi ili kujiepusha na madhara yatokanayo na ukosefu wa lishe kama vile udumavu na utapia mlo.

"Nendeni mkazingatie sheria, msicheke na wazazi, watoto lazima wapate chakula wakiwa shuleni na wazazi lazima wachangie kwa kuzingatia sheria, nyinyi kazi yenu ni kwenda kusimamia sheria hiyo ili watoto hawa wajiepushe na athari zitokanazo na ukosefu wa lishe".

Amesema kuwa kitaifa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa imefanya vizuri sana, na hiyo yote ni kutokana na jitihada kubwa na juhudi zilizofanywa kufanikisha hilo hivyo amewataka Watendaji na Wataalamu kuendeleza jitihada na juhudi hizo ili kuweza kupanda zaidi.

Aidha amepongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa chini ya Mwenyekiti Mhe. Mhapa na Mkurugenzi Mtendaji Wakili Muhoja kwa kuhakikisha kuwa fedha iliyotengwa kwa ajili ya masuala ya lishe inawasilishwa kwa wakati na inatumika ipaswavyo.

"Ninajuwa mna mambo mengi lakini pia hamkuweza kulisahau hili la lishe hivyo ninawapapongeza sana na muendelee kufanya hivyo".

Lakini pia Mkuu wa Wilaya Mhe. Moyo amesisitiza Wataalamu kuendelea kutoa elimu na hamasa kwa wananchi kujisajili kwa ajili ya kupata mbolea ya ruzuku.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja amesema kuwa kuwajali watoto ni jukumu la wote na kama tusipowajali kwa kuwapatia lishe bora basi tutakuwa na kizazi cha hovyo kwa hapo baadae.

" Hawa watoto kwa hapo baadae watakuja kuwa kwenye meza ya maamuzi hivyo tuwaandae hawa watoto na kuwaandaa ni pamoja na kuwafanya wawe na bongo nzuri na bongo nzuri inatokana na lishe".

Naye Afisa Lishe Wilaya Bibi Tiliza Mbula ameshukuru Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri kwa kuweza kusimamia vyema na kuifanya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kufanya vizuri kitaifa kadhalika amewaomba na kuwataka watendaji kuendelea kuhamasisha lishe kwa wanafunzi ili Halmashauri iweze kufanya vizuri na ipande nafasi za juu zaidi.

Mkurugenzi Mtendaji Wakili Muhoja amesaini na kukabidhi mikataba ya lishe kwa Watendaji wa Kata za Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kwa lengo la kufanya utekelezaji kwa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa