• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Diwani wa Kata ya Maguliwa Mh.Jane Mhangala akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wataalam kutoka Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wilaya ya Iringa na wananchi waliojitokeza katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa Kijinsia.

Imewekwa : December 4th, 2021

Kutokuwajibika,Pombe vyaelezwa kuwa vyanzo vya matendo ya Kikatili katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.

Anton Ramadhan (Iringa - DC)

Kilele cha maadhimsho ya siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia ambapo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa yamefanyika katika Kata ya Magulilwa, Kijiji cha Ng’enza jana Disemba 3 mwaka huu wa 2021.

Akizungumza katika Maadhimisho hayo Diwani wa Kata ya Magulilwa Mh.Jane Mhangala ambaye alikuwa Mgeni Rasmi ametoa rai kwa wakazi wa Kata hiyo kujikita katika shughuli mbalimbali za kujiingizia kipato ili kutopata muda wa kufanya matendo maaovu yakiwemo matendo hayo ya ukatili.

“Iwapo wananchi na Wakazi wa Ng’enza na Magulilwa kwa ujumla mkiwa mnatumia muda mwingi katika kazi za kuwaingizia kipato ni wakati gani mtapata muda wa kuwapiga,kuwang’ata,kuwachoma moto,kuwakatakata,kuwajeruhi au kubaka watoto”alisema na kuongeza

“Nina ahidi kwenda kuzungumza na taasisi inayojihusisha na masuala ya sheria ili waje kuwapa elimu ya sheria ili muweze kufahamu makosa na adhabu za mtu au watu wanaokinzana na sheria”alisema.

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bi.Gladness Amunike amewaomba wananchi kuwa wapesi kutoa taarifa za Ukatili kwa kuwa sasa katika maeneo yao wapo wananchi ambao wamefundishwa namna ya kutambua na kukabiliana na matendo ya ukatili wa kijinsia.

“Tusiwafiche wabakaji wa watoto wetu hata kama ni ndugu au wenza wetu tutoe taarifa haraka ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa na waliofanyiwa ukatili waweze kupatiwa msaada na huduma kwa haraka”alisema.

Aidha Kaimu Afisa Maendeleo wa Halmashauri ya Wilaya Bi Dora Mlomo amesisitiza umuhimu wa kujishughulisha na kazi mbalimbali za kijikwamua kiuchumi hasa kwa wanawake ili waweze kujizuia na matendo ya ukatili hasa ya vipigo na mashambulio ya mwili ikiwemo kuchoma moto watoto,kuwang’ata na kupata adhabu kandamizi.

Pia,Afisa Polisi Dawati la Jinsia na Watoto Elizabeth Swai ameelezea namna jamii inavyoharibu mashauri yakiwa katika hatua za awali za upelelezi,huku pombe ikitajwa kichochea kikuu cha matendo ya ukatili.

Amesema katika hatua za awali ndipo jamii iliyotendewa kosa hukuatana na upande wa mtenda kosa na kukubaliana kumaliza shauri hilo kwa kupeana fedha au mali na kupelekea mashauri mengi kutofanikiwa katika hatua ya maamuzi kwa kuwa jamii iliyotendewa kusita kufika mahakamani kwa ajili ya kutoa ushahidi pindi wanapotakiwa kufanya hivyo au kuwatorosha wahusika waliofanyiwa vitendo vya kikatili.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa