• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

JAMII YAKUMBUSHWA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA MAAMBUKIZI YA VVU/UKIMWI

Imewekwa : December 1st, 2023

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mhe. Stephen Mhapa kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Iringa ameikumbusha jamii kuchukua hatua dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI kwani UKIMWI unapunguza nguvukazi ya Taifa na kuzalisha utegemezi kwa watoto kukosa malezi ya wazazi. Mhe. Mhapa mezungumza hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika katika kijiji cha Isimani Tarafani Kiwilaya 01.12.2023.

 “Serikali yetu ya Rais Samia Suluhu Hassan inaleta fedha nyingi sana kwenye sekta mbalimbali kujenga miundombinu lakini kama hatutachukua tahadhari dhidi ya VVU/UKIMWI, hivyo vitu vinavyofanywa tutaishia kuvisikia tu na vitakosa wa kuvitumia,” amesema.

Eidha Mhe. Mhapa ameiasa jamii kutoa matunzo na malezi kwa watoto ili waweze kufikia ndoto zao. “Hawa watoto wote wanaosoma wakikosa malezi ya Wazazi na familia maana yake ndoto zao zinapungua kwa sababu hawana wa kuwatunza, leo hii tunapata elimu bila malipo lakini ukweli ni kwamba bado yanahitajika matunzo na huduma mbalimbali mzazi inabidi apambane nazo kwaajili ya mtoto wake” amesema.

Kwa upande wake mmoja wa watu wanaoishi na maambukizi ya VVU/UKIMWI Bi Rehema Michael Sanga ametoa wito kwa jamii kujitokeza na kujua afya zao na kwa wale watakaopatikana na maambukizi wasiache kufuatilia afya zao na kuwa na ufuasi wa dawa bila kuacha kwani hata yeye ana miaka mingi akiwa na maambukizi lakini kwa kujiweka wazi ameweza kufanya ufuasi bora wa dawa na hatimaye afya yake ni nzuri na ameweza kulea familia yake.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Bi. Saumu Kweka amewashukuru wananchi wote wa kijiji cha Kihorogota kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki maadhimisho haya sanjari na wadau mbalimbali walioshiriki moja kwa moja kufanikisha shughuli hii wakiwemo wadau kutoka Shirika la Compassion

Maadhimisho haya yamefanyika yakiwa na kauli mbiu isemayo, “Jamii Iongoze Kutokomeza UKIMWI”

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa