• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA FEDHA, UTAWALA NA MIPANGO YAFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI

Imewekwa : February 14th, 2024


Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mheshimiwa Stephen Mhapa, imefanya ziara kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Halmashauri Februari 14, 2024.

Ziara hiyo ilianzia katika shule ya Msingi Lyamgungwe iliyopo Kata ya Lyamgungwe, kuna ujenzi wa vyoo matundu 19. (Wasichana matundu 10, Wavulana matundu 6 na Walimu matundu 3), mnara wa kuweka tanki la maji na kichomea taka.

Kiasi cha Shilingi Milioni 50 zilitolewa na Serikali katika mradi huo na nguvu za wananchi wamechangia kiasi cha Shilingi Milioni 11.3 na kufanya jumla ya kiasi cha Shilingi 61.8 hadi kukamilika kwake. Mradi ulianza mwaka wa Fedha 2022/2023 umekamilika kwa 100% na unatumika.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Lyamgungwe ameomba kuwa, kama ikitokea ukaletwa mradi mwingine wanaomba kupewa usafiri kwa ajili ya kusafirishia madini ujenzi, pia huduma ya maji ya kudumu iwepo ili kurahisisha utendaji kazi.

Kamati imepongeza mradi kwenda vizuri na kuomba mradi utunzwe vizuri kwa usalama wa afya zao.

Kamati pia imetembelea Kijiji cha Ibumila ambapo kuna shamba la parachichi na kujionea shughuli zilizofanyika hapo.

Akitoa lengo la mradi wa shamba hilo Bi. Luvy Nyallu amesema ni kuweka shamba darasa, kuongeza kipato baada ya mavuno. Shamba hilo lenye ukubwa wa heka 12 ambapo imepandwa miche 912 na imetumia kiasi cha Shilingi Milioni 30 na kwamba msimu wa tano wanategemea kuvuna kukadiria kupata zaidi ya Shilingi Milioni 47.

Kamati imeridhia mradi huo na kutoa ushauri kuwa, ujengwe uzio ili kuimarisha ulinzi.

Wakisalia hapo Ibumila katika mabwawa ya samaki manne ambayo yamejengwa kwa lengo la kufanya shamba darasa na kuongeza kipato. Kiasi cha Shilingi Milioni 116.3 zilitengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.

Vifaranga zaidi ya 9,600 vitapandwa na kilo zaidi ya 12,800 zitapatikana katika mabwawa hayo. Hatua ya mradi ni 100%.

Kamati imeridhishwa na mradi huo na kutoa ushauri kuwa, zipandwe nyasi kando ya mabwawa ili kuzuia mmomonyoko wa udongo.

Kamati pia imepata nafasi ya kutembelea Shule ya Sekondari Lumuli iliyopo Kata ya Lumuli katika ujenzi wa vyoo vya wanafunzi matundu 9. Kiasi cha Shilingi Milioni 7.8 kilitengwa na nguvu za wananchi ni Shilingi Milioni 6 na kufanya jumla ya fedha kuwa Shilingi Milioni 13.

Kamati imeridhia mradi na kutoa ushauri kuwa, ujenzi ukikamilika vyoo visitumike hadi mfumo wa maji utakapokuwa tayari. Ujenzi umefikia 90% ujenzi unaendelea.

Kamati imefika Shule ya Sekondari ya Ufundi Ifunda na kujionea mradi wa ujenzi wa Bweni la Wasichana lenye uwezo wa kulawa wanafunzi 80, ambapo kiasi cha Shilingi Milioni 130 zililetwa kutekelezwa mradi.

Mradi ulianza Oktoba 2023 na ulitakiwa kukamilika Januari 2024, Lakini kutokana na changamoto mbalimbali hadi sasa ujenzi unaendelea na sasa umefikia 90%.

Kamati imeridhia mradi na kushauri kuwa, Mkandarasi aongeze kasi ya ujenzi, na ametakiwa hadi kufikia Febaruari 20, awe amekamilisha mradi na kukabidhi.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa