• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Yafanya Ziara Kukagua Miradi ya Maendeleo kwa Robo ya Tatu 2022/2023

Imewekwa : May 12th, 2023

Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Yafanya Ziara Kukagua Miradi ya Maendeleo kwa Robo ya Tatu 20222/2023

Kamati ya Fedha,  Utawala na Mipango imefanya ziara kukagua miradi mbalimbali ambayo inatekelezwa katika Halmashauri kwa mwaka wa Fedha 2022/2023.

Kamati hiyo ambayo imeongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Mheshimiwa Methew Nganyagwa, imeanza kwa kwenda katika Kijiji cha Ilambilole Kata ya Kising’a kukagua mradi wa kinga maji ambao unatekelezwa na walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa kupewa ajira ya muda.  Kamati baada ya kuona mradi wameshauri mambo mbalimbali ikiwemo kumalizia mradi kwa wakati. Mradi umepewa siku 60 hadi ukamilike na ulianza 01/03/2023.

Pia Kamati imeweza kwenda hadi kijiji cha Makuka Kata ya Izazi katika mradi wa ujenzi wa Josho, ambapo mradi huu unatekelezwa na Halmashauri kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira kupitia mpango wa Sustainable Landscape Restoration – SLR. Mradi ulianza Machi, 2023 na unatarajiwa kukamilika Juni 15, 2023. Kamati imeshauri kuharakisha mradi huo ili ifikapo Juni 15, 2023 uwe umekabidhiwa.

Kamati imeendelea kufanya ziara yake hadi Kijiji cha Mnadani Kata ya Izazi ambapo kuna mradi wa ufugaji ng’ombe 3  wa maziwa, ambao unafanywa na kikundi cha Tumsifu chenye watu 6 wenye Ulemavu, ambapo kuna wanaume 4 na wanawake 2. Ng’ombe hawa wametolewa kwa Ruzuku kutoka Ofisi a Makamu wa Rais Mazingira kwa mpango wa Sustainable Landscape Restoration – SLR.

Aidha Kamati imetembelea katika Kijiji cha Migoli Kata ya Migoli katika mradi wa upandaji miti ya matunda. Mradi huu unatekelezwa na Walengwa wa TASAF kwa kupewa ajira ya muda. Miti iliyopandwa ni aina ya miembe, machungwa, malimao na mapera.

Kamati haikuishia hapo, bali imeenda kijiji cha Mbweleli Kata hiyo ya Migoli katika mradi wa utengenezaji barabara inayolimwa kwa njia ya mikono, ambapo mradi unatekelezwa na Walengwa wa TASAF kwa kupewa ajira ya muda.

Vilevile katika Kata hiyo ya Migoli Kijiji cha Makatapola kuna mradi wa ufugaji mbuzi, ambapo unatekelezwa na kikundi cha Nanyolai chenye watu 20 wakiwa wanawake 17 na wanaume 3. Kikundi hiki kilipatiwa Fedha ya Ruzuku zaidi ya Milioni 10 na kuanzisha mradi wa mbuzi 95. Hadi sasa mbuzi 37 wamezaa na kupatikana ndama 39 na kufanya jumla ya mbuzi kuwa 134. Mradi ulianza mwezi Machi, 2023.

Kwa niaba ya Kamati Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Mheshimiwa Methew Nganyagwa, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi ili kutekeleza miradi mbalimbali katika Halmashauri. Mheshimiwa Nganyagwa amewasihi wote wanatekeleza miradi hiyo kufanya kazi kwa bidii na kwa ufanisi ili ikitokea fursa nyingine wasiweze kukosa.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja, ametoa rai kwa kikundi cha Ufugaji mbuzi cha Nanyolai kuendelea kupanda miti ili kuhifadhi mazingira na kuwa chanzo cha mvua. Kutokana na Tabia Nchi mazingira yanapoeza uoto wa asili na kusababisha jangwa kubwa.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa