• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Yatembelea Kata ya Migoli Kukagua Maendeleo ya Kata

Imewekwa : September 19th, 2022

Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Yatembelea Kata ya Migoli Kukagua Maendeleo ya Kata

Kamati hiyo imetembelea Kata ya Migoli tarehe 19/09/2022 kwa ajili ya kuongea na Wataalam wa Kata hiyo juu ya miradi ya Maendeleo.

Kati ya mambo ambayo yameongelewa katika kikao hicho ni pamoja kuwakumbusha kuwa, Wataalam na Diwani wa Kata hiyo Mheshimiwa Benitho Kayugwa kusimamia kwa umakini miradi ya maendeleo ili kufanikisha maendeleo ya wananchi.

Akiongea katika kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Steven Mhapa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo amesema, “Maendeleo ya Kata yanatokana na usimamizi mzuri wa ninyi Wataalam, hivyo mnapaswa kuwa mstari wa mbele katika usimamizi. Diwani na Wataalam lazima muwe na mawasiliano ya pamoja katika suala zima la utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hivyo siyo sawa kupishana kauli na kupelekea mgongano wa utekelezaji na kusababisha sintofahamu kwa wananchi”.

Mheshimiwa Mhapa ameongeza kusema kuwa, “heshima ni kitu cha msingi sana, yatupasa kuheshimiana bila kujali cheo wala nafasi uliyopo. Pia kuwe na mipaka katika masuala ya kazi. Kila mtu afanye kazi kulingana na mipaka yake ya kazi inapoishia”.

Aidha, Mheshimiwa Mhapa ameongelea suala la siasa akisema, “Madiwani ndiyo tunatakiwa kufanya siasa na si Wataalamu. Pamoja na kuwa viongozi wengi wanatokana na siasa, lakini Mtumishi wa Umma hatakiwi kuwa Mwanasiasa kwani yeye ni Mtendaji, na kufanya kazi kwa kadri taratibu zinavyomtaka na siyo kuleta siasa”.

Aidha Mheshimiwa Mhapa amewata watumishi wasiwe wanatoleana maneno makali na lugha zisizofaa, hata kama kuna jambo limekufanya uwe na hasira hadi kupelekea maumivi ya moyo, vumilia na kutafuta namna ya kulitolea ufumbuzi.

Kadhalika, Mheshimiwa Mhapa ametoa shukrani kwa wajumbe wa Kamati hii kwa kujitoa na kushiriki vema katika kuchangia hoja zilizopo katika kikao hicho.

Naye Diwani wa Kata hiyo Mheshimiwa Benitho Kayugwa amesema, “nipo tayari kwa kila jambo kushirikiana na Wataalamu ili kuendeleza gurudumu la maendeleo katika Kata yangu ya Migoli. Nitashirikiana vema na Mtendaji wa Kata hii na Watendaji wa Vijiji vyote vya Migolo”.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bi. Beatrice Augustine alikuwa na haya ya kusema, “pamoja na mambo mengine yote, ni vizuri kila mtu asimame katika nafasi yake na ajue haki na wajibu wake. Tukitambua hili kila mtu atafanya kazi kwa raha na hakutakuwa na manung’uniko yoyote”

Bi. Beatrice amewasihi watumishi kufanya kazi kwa kupendana na kuchukuliana, kufanya kazi kwa bidi ili kuleta tija kwa maslahi mapana ya wananchi katika maendeleo.

  

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa