• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAMISAA WA SENSA MAMA ANNA MAKINDA AWATAKA MAAFISA HABARI WA SERIKALI KUTOA ELIMU YA SENSA YA WATU NA MAKAZI

Imewekwa : May 12th, 2022

Makinda atoa neno kwa Maafisa Habari, Uhusiano na Mawasiliano Serikalini kuhusu Sensa 2022

Na Zaituni Gwaja

Spika Mstaafu wa  Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na Kamisaa wa Sensa Bi. Anna Makinda amezungumza na Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali katika kikao kinachoendelea kufanyika Jijini Tanga katika Ukumbi wa Regal Naivela juu ya majukumu yao katika suala zima la Sensa.

Ambapo Kauli Mbiu ya Mkutano huo ni “Mawasiliano ya Kimkakati Nyenzo Muhimu Kufanikisha Sensa ya Watu na Makazi 2022”

Bi. Makinda amesema kuwa, sensa ni jambo la lazima katika kila Taifa, Kwa Taifa letu sensa hufanyika kila baada ya miaka kumi na kwa Tanzania ni sensa ya sita tangu kuungana kwa Tanganyika na Zanzibar, na mwaka huu Sensa itafanyika mwezi Agosti, 23.

“Itakuwa sensa ya kidigitali kwani itatumia sana mifumo (TEHAMA), ambayo itahesabu hadi majengo, ili kujua kuna majengo mangapi ya Serikali, Taasisi, makazi n.k.” amesema.

Bi Makinda ameendelea kusema kuwa, zitatumika rasilimali zilizopo ili kufanikisha zoezi hili, kwani hakuna bajeti iliyoandaliwa kwa kazi hii.

Ameongeza kusema kuwa, sensa hii ni shirikishi na Maafisa Habari ndiyo hasa wanatakiwa kuifanya kazi hii kwa kutangaza na kutoa takwimu sahihi. Sensa hii watakaonufaika ni vijana kwani asilimia kubwa huwa wanatumia mitandao ya kijamii, pia itasaidia kujua vijana wangapi wameajiriwa, hawana ajira, na wangapi wamejiajiri.

Katika maandazili haya ya Sensa ni 81% imekamilika na 19% imebaki kwa ajili ya kutoa matangazo ya watu kuomba kufanya kazi ya kkarani.

 Katika zoezi hili ajira zimegawanyika katika sehemu tatu ambazo ni; Karani wa kuhesabu, Msimamzi wa Maudhui na Karani wa Mfumo (TEHAMA), hivyo imesisitizwa watu wajitokeze kwa wingi kuomba nafasi hizi.

“Asijitokeze muombaji yoyote kutoa fedha ili apatiwe nafasi ya ukarani, hii ni kosa kisheria”, amesema Bi. Makinda.

Bi. Makinda amesisitiza kuwa, itumike mitandao mbalimbali kuweka ujumbe wa Sensa, hotuba mbalimbali za viongozi lazima mwishoni kuwepo na ujumbe wa sensa. Pia katika vipindi vyote vya runinga na redio kuwepo na ujumbe huo kwani ni Agenda ya Kitaifa.

Ifikapo Juni mafunzo juu ya kufanya Sensa yatatolewa, na Ifikapo Julai 27 shule zote zitafungwa hadi Septemba 4 ili kurahisisha zoezi hili.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Mheshimiwa Allan Kijazi amesema, malengo ya kufanya sense kwanza ni umuhimu wake katika taifa kwani itasaidia katika mambo kama; kupata takwimu za makazi yote, kufanya tathimini ya makazi ili kutoa huduma bora, kukusanya mapato kwa njia bora, Serikali kuendeleza Miji, kujua mgandamizo wa makazi, kufanya umiliki na mengine mazuri.

Amesema pamoja na haya tujitokeze kuhesabiwa na kutoa ushirikiano katika jambo hili.

Kauli Mbiu ya Sensa kwa Mwaka huu ni: “Sensa kwa Maendeleo, Jiandae Kuhesabiwa”.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa