• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kampeni ya Chanjo ya Polio Kitaifa Awamu ya Tatu (RD3), Yavuka Lengo la Mafanikio

Imewekwa : October 11th, 2022

Kampeni ya Chanjo ya Polio Kitaifa Awamu ya Tatu (RD3), Yavuka Lengo la Mafanikio

Kamati ya Afya ya Msingi imekaa leo Oktoba 11, 2022 kufanya tathimini na kutoa taarifa ya Utekelezaji wa Kampeni ya Chanjo ya Polio Kitaifa Awamu ya Tatu (RD3), ambayo imefanyika mwezi Septemba. Kampeni hiyo ilijikita kupita nyumba kwa nyumba kwa ajili ya kuelimisha jamii na kutoa chanjo kwa watoto chini ya miaka mitano juu ya ugonjwa wa polio.

Awamu ya Kwanza ya Kampeni hii ilifanyika kwa Mikoa inayopakana na nchi ya Malawi yaani Mbeya na Songwe, kwa sababu ugonjwa huu ulianza kulipuka nchini Malawi. Awamu ya Pili ya Kampeni imefanyika kwa Mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani ili kuwakinga watoto chini ya miaka mitano kutokana na ugonjwa huu ambapo lengo ni kuwafikia watoto zaidi 53,191 na kufanikiwa kuwachanja watoto zaidi ya 55,055 sawa na 103%.

Katika Awamu ya Tatu kwa malengo ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, iliazimia kuwakinga watoto zaidi ya 47,158 hivyo kuvuka lengo na kufanikiwa kuwafikia na kuchanja watoto zaidi ya 51,646 sawa na 110%.

Akitoa pongezi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Mohamed Moyo, ambaye ni Mwenyekiti katika Kamati hiyo amesema, “kwanza nawapongeza sana timu yote ya Afya kwa uhamasishaji na kutekeleza zoezi hili na kuvuka malengo tuliyojiwekea katika kuwachanja chanjo ya polio kwa watoto chini ya miaka mitano”. Pia amemuomba Mkurugenzi Mtendaji kuwapatia barua ya pongezi kwa Timu yote ya Afya kwa kufanya vizuri katika zoezi hili la chanjo.

Mheshimiwa Moyo ameongeza kusema kuwa, amealika na Kamati ya Ulinzi na Usalama ili waone umuhimu katika uhamasishaji wa zoezi hili pia wawe mabalozi wazuri kwa watu wengine.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja alikuwa na haya ya kusema, “pamoja na kuwa Halmashauri hii imetawanyika sana lakini Timu ya Afya ambayo inaongozwa na Mganga Mkuu, imepambana katika kuwafikia walengwa nyumba kwa nyumba, na hatimaye kuvuka lengo na kufikia 110%.” Hii inatia moyo sana na kuchukua suala la Mheshimiwa Moyo la kuwapatia barua za pongezi timu hiyo.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya Daktari Samwel Marwa amesema, “katika zoezi hili la utoaji wa chanjo safari hii tumefanya kitalaamu zaidi kuliko kipindi kingine chochote, kwani hakukuwa na ubabaishaji. Tumetumia vifaa ambavyo vimepima na kuonesha kuwa kila nyumba imechanja watu wangapi (GPS), hivyo hakuna upotoshaji wa taarifa”. Mganga Mkuu amemaliza kwa kuwashukuru Timu nzima ya afya na kuwaomba kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa