Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Kheri James, amepokea Ugeni wa Kampuni ya CC AIRWELL kutoka Nchi ya Austria Barani Ulaya wenye lengo la kuwekeza katika Kuvuna Maji Safi kutoka Angani Kwa Teknolojia ya Kisasa, pamoja na Uhifadhi wa Mazingira katika maeneo yanayokabiliwa na hali ya ukame ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.
Mmiliki na mwanzilishi wa kampuni ya CC AIRWELL, Wolfgang Rainer Fuchs, amesema Kampuni hiyo inajishughulisha na uhifadhi na urejeshwaji wa mazingira katika maeneo yanayokabiliwa na hali ya Ukame ikiwemo maeneo ya jangwa kwa kuzalisha maji safi kwa ajili ya matumizi ya binadamu, mazingira, ikolojia na maendeleo ya kiuchumi kwa kutumia teknolojia mpya ya uvunaji wa maji yaliyo katika hewa angani.
Fuchs ameeleza zaidi akisema kuwa Kampuni hiyo inatarajia kujenga mitambo yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ikiwa na lengo la kuzalisha maji na kuyasambaza katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Iringa ikiwemo mbuga ya hifadhi ya Taifa ya Ruaha.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Kheri James, ameeleza kuwa Kampuni hiyo itafanya Uwekezaji Kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya hiyo kusaidia katika Uvunaji na Usambazaji wa Maji takribani Lita Milioni 260 Kwa Mwaka kutoka angani Kwa ajili ya Matumizi ya Binadamu, sambamba na utunzaji wa Mazingira Kwa kuvuna Hewa ya ukaa.
"Maeneo yatakayohusika ni Yale ambayo Kwa Sasa yanakabiliwa na ukame kama maeneo ya Izazi, Mboliboli, Migoli, Itunundu, lakini Kipekee wameichagua Izazi kuwa Sehemu ya kuanzia, Wilaya ya Iringa tupo tayari kuhakikisha Mazingira yanatunzwa na Huduma za Maji zinazidi kuboreshwa na kusogezwa Karibu na Wananchi" - Amesema DC Kheri James.
#iringaimaratutaijengakwaumojanauwajibikaji
https://www.instagram.com/p/DKQLSyAtZjd/?igsh=MWt1d3o1cGQ0M2d1Zw==
Kijiji cha Ihemi
Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa
Simu ya mezani: 026-2702828/2702585
Simu ya mkononi: 0757 364 994
Barua pepe: ded@iringadc.go.tz
Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa