• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kiasi cha Shilingi Milioni 89.6 ya Bajeti ya Afua za Lishe 2024/2025

Imewekwa : November 29th, 2023

Kiasi cha Tsh. 89,697,923/- Kimetengwa Kwa Ajili ya Utekelezaji wa Afua za Lishe Kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025

Bajeti hiyo ambayo imepangwa leo Novemba 29, 2023 ikiongozwa na Afisa Lishe wa Halmashauri Bi. Tiliza Mbulla, imebainisha kuwa kiasi cha Shilingi 63,837,923/- kutoka Mapato ya Ndani ya Halmashauri na Kiasi cha Shilingi 21,020,000/- ni Ruzuku kutoka Serikali Kuu, na kufanya jumla ya Bajeti hiyo kuwa Shilingi 89,697,923/-

Halmashauri imeendelea kupambana na matatizo ya lishe duni kwa makundi mbalimbali katika jamii ikiwemo watoto wenye umri chini ya miaka mitano 47,158, kina mama wajawazito 12,908 kwa Mwaka wa Fedha 202/2023, pia hali ya lishe kwa makundi mengine ya wananchi wanaokadiriwa kuwa 322,704 kwa ujumla wao.

Aidha, shughuli za mapambano dhidi ya lishe duni zinafanyika kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wa lishe kwa kuzingatia mikakati ya lishe na kufuata vipaumbele vilivyowekwa katika Mpango Jumuishi wa Taifa wa Lishe (NMNAP II 2021/2022 – 2025/2026).

Utekelezaji wa Afua za Lishe umekuwa na ufanisi kwa uratibu wa watoa huduma 268 wa ngazi ya jamii (CHWs) pamoja na watoa huduma wa afya katika vituo 81 vya kutolea huduma za afya.

Akibainisha vipaumbele vya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025, Afisa Lishe Bi. Avelina Selemani amesema “Lishe ya akina mama, watoto na vijana balehe, Lishe katika siku 1000 za kwanza, Utambuzi na matibabu ya utapiamlo wa kadri na mkali kwa watoto chini ya miaka mitano, Elimu ya kuzuia magonjwa yasiyoambukiza anayohusiana na lishe (DRNCD), Matumizi ya virutubishi vya nyongeza (Vitamin A.) na matibau ya minyoo na Uzalishaji na matumizi ya vyakula mchanganyiko (makundi 6 ya chakula”.

Aidha, Bi. Avelina ameweza kutaja changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa Afua za Lishe kuwa ni pamoja na ufinyu wa bajeti hasa kwa Idara mtambuka, hivyo kufanya utekelezaji kwa uchache ikilinganishwa na mahitaji halisi. Ukosefu wa usafiri, mafuta na posho kwa ajili ya ufuatiliaji wa karibu wa shughuli za lishe, hivyo shughuli kukosa uendelevu.

Pamoja na changamoto hizo, Bi. Avelina ametoa njia ya kuweza kukabiliana nazo ikiwa ni kushirikisha Wadau ili kuweza kusaidia hasa katika suala la usafiri.

Ingawa kumekuwepo na changamoto hizo Wadau na jamii kwa ujumla bado wana uhitaji mkubwa wa elimu ya lishe kwani watu wengi wanaamini kuwa suala la lishe linawahusu watoto na wanawake tu.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa