• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2022

Imewekwa : June 28th, 2022

"Msikae Kizembe Kwenye Maeneo yenu ya Kazi" - DC Moyo

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Mohamed Moyo amewataka watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kuepuka kukaa kizembe katika maeneo yao ya kazi na ni muhimu kuchangangamkia fursa zilizopo ili kuwekeza na baadae kuja kuwa msaada wako wakati wa kustaafu.

Ameyazungumza hayo leo tarehe 28.08.2022 alipokuwa akihitimisha Maadhimishi ya wiki ya Utumishi wa Umma kwa Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa yaliyofanyika katika Hospitali Teule ya Wilaya Tosamaganga, ambapo amekuwa Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo.

Amewataka Watumishi wa Umma kuwa na nidhamu ya kazi, kupenda kufanya kazi bila kushurutishwa ikiwemo kuwahudumia wananchi kwa weredi, uzalendo na kwa uaminifu mkubwa bila kutanguliza rushwa au kuchelewa.

Sambamba na hilo amewaomba Watumishi wa Umma kuendelea kupunguza kero za wananchi katika maeneo yao ili kupunguza foleni katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya au Mkoa. Pia amewataka Watumishi wa Umma kuacha kufanya kazi kwa mazoea, wabadilike katika utendaji wao wa kazi.

"Mtumishi lazima uwe mbunifu mahali pa kazi ili hata ikitokea umehamishwa eneo la kazi basi Watumishi na wananchi wakuongelee vizuri kwa kuacha alama na si washangilie na kupika pilau kwa kuondoka kwako".

Mhe. Moyo pia ametoa pongezi kwa Viongozi na Watumishi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kwa kufanikisha zoezi la anuani za makazi na hivyo kupelekea kuwa wa kwanza kitaifa ingawa bado zoezi la kuandika na kupachika namba za nyumba linaendelea.

Aidha amesisitiza juu ya upigaji vita masuala ya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto, amesema watuhumiwa wote ni vyema kuchukuliwa hatua za kisheria na ni marufuku kwa mtuhumiwa akikamatwa kumalizana wenyewe kwa wenyewe ikibainika pia wote watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Akizungumza katika Maadhimisho hayo Katibu Tawala Wilaya ya Iringa Ndugu Stomin Kyando amesema lengo la maadhimisho hayo ni kukumbushana majukumu ya kiutumishi ambapo amesema kuwa Watumishi wote wa Umma wanafanya kazi kwa ridhaa ya Mhe. Rais kwani yeye ndio mwenye mamlaka ya kuanzisha au kufuta taasisi yoyote nchini.

"Tunapaswa tutekeleze majukumu yetu kwa niaba ya Mhe. Rais, Matendo yako yaakisi na yaendane kama Mtumishi wa Umma, tusifanye dhuluma katika kutoa huduma ni dhambi kubwa, lakini pia ninawashukuru kwa ushirikiano mlionao na kwa kazi mnazozifanya hongereni sana."Amesema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja amewapongeza Watumishi wote wa Halmashauri kwa ufanyaji kazi mzuri japo kuna baadhi yao ni wakorofi lakini bado anaendelea kuwaelewesha namna nzuri na sahihi ya utendaji kazi kama baba.

Pia amezungumzia suala la mapokezi ya Watumishi wapya wanaotarajia kuwasili na amesema kuwa amewaagiza Watendaji wa Vijiji kuandaa mazingira rafiki kwa Watumishi hao wapya kwa kuwatafutia nyumba nzuri pamoja na mahitaji yao mengine ya msingi kwani kwa kufanya hivyo kutapelekea kuwafanya wajihisi vizuri na wasione tofauti yoyote.

Akisoma risala (Taarifa) ya Maadhimisho hayo Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Bibi Beatrice Augustino amesema kuwa Halmashauri ina jumla ya Watumishi 3134 na katika maadhimisho haya Jumla ya Kata 8 na Watumishi 226 wametembelewa na mada mbalimbali zimewasilishwa na kulikuwa na jumla ya changamoto 47, changamoto 42 zimetolewa ufafanuzi na changamoto 5 zinafanyiwa uchunguzi.

Tumefanya hitimisho leo kwa kufanya usafi katika maeneo ya Hospitali ya Tosamaganga ninawashukuru Watumishi wote kwa ushirikiano mlionipa na wale Watumishi ambao wametkka nje ya Halmashauri ambao tumezunguka pamoja katika maadhimisho haya ninasema asante na Mwenyezi Mungu awabariki sana.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa