• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

M-MAMA YAJA MKOANI IRINGA

Imewekwa : May 16th, 2023

M-MAMA YAJA MKOANI IRINGA

Mhe. Peres Boniphace Magiri Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa amezindua Mfumo wa Kidigitali wa huduma kwa akinamama wajawazito na watoto hasa katika eneo la usafirishaji na ufuatiliaji (M-MAMA) katika Mkoa wa Iringa, mpango utakaosaidia kuokoa maisha ya akinamama wajawazito na watoto wachanga kwa kuchelewa kupata huduma.

Akizungumza wakati wa kikao cha uzinduzi wa mpango huu Mhe. Magiri amesema, “M-Mama inakuja ili kuongeza thamani ya jitihada za Serikali hivyo, Mkoa wa Iringa tuna wajibu wa kulibeba jambo hili litapoanza 15.08.2023 kuhakikisha kuwa tunapunguza au kuondoa kabisa vifo vya wamama wajawazito na watoto wachanga”

Pia Mhe. Magiri ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuzindua rasmi mpango wa usafirishaji wa dharura wa akinamama wajawazito, waliojifungua na watoto wachanga (M-Mama) Kitaifa Mkoani Dodoma, mpango ambao utasaidia kupunguza vifo vya wamama wajawazito na watoto wachanga utakaotekelezwa nchi nzima.

Naye Dr. Mshana Dastan kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi amesema Serikali imefanya jitihada za kununua magari ya kubebea wagonjwa (ambulance) Zaidi ya 700 ambapo kila Mkoa utapata gari ya Ambulance ya kisasa kabisa yenye huduma zote ndani za kitabibu na kila Halmashauri itapata gari mbili za Ambulance za kawaida mgao ambao utaenda kwa awamu. Sanjari na hayo pia Dr. Mshana amesema kuwa Ambulance zinapaswa kutumika kwa ajili ya kazi tarajiwa tu ambayo ni kuwahudumia wagonjwa na kufanya ukarabati wa zile zinazoharibika.

Kwa upande wake Mratibu wa Afya ya Uzazi na Mtoto (RRCHCO) Mkoa wa Iringa, Bi Wende Mwavika ameeleza hali halisi ya miundombinu na vifo vya wamama wajawazito na watoto vinavyotokea kwenye maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Iringa sanjari na jitihada au hatua zinazochukuliwa kukabiliana na changamoto zilizojitokeza.

Kwa niaba ya Wenyeviti wa Halmashauri Mkoa wa Iringa Mhe. Stephen Mhapa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, ameshukuru na kupongeza kuhusu mpango huu wa M-Mama ambao umeanza hatua ya awali kwa kuwashirikisha viongozi wanaowafikia wanchi moja kwa moja na kuomba ushirikishwaji huu uwe endelevu ili kuwa na uelewa wa pamoja hivyo kuleta ufanisi.

Mpango wa M-Mama utatumia kanzidata ya mawasiliano na kanzidata ya usimamizi na ufuatiliaji. Kutakuwa na kituo ngazi ya Mkoa ambacho kitakuwa ndio kituo cha kuratibu dharura (Dispatchers) na kituo kitakuwa kinapokea taarifa kutoka kwa wahudumu wa vituo vya kutolea huduma za afya ngazi mbalimbali na kuratibu masuala ya usafiri na ufuatiliaji wa huduma kwa mgonjwa. Namba itakayotumika kutolea taarifa ya dharura ni 115 ambayo ni tall free na itawafikia Dispatchers moja kwa moja kwa hatua.

Kwa mkoa wa Iringa Mpango huu unatarajiwa kuanza rasmi katikati ya mwezi August 2023 baada ya hatua zingine kufikiwa kulingana na mpango kazi ulioandaliwa.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa