• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Imewekwa : June 23rd, 2022

"Ifanye kazi yako kuwa sehemu ya Ibada"- Mkuu wa Idara Utumishi Beatrice Augustino

Ifanye kazi yako kuwa sehemu ya ibada, tutekeleze kazi zetu kwa uadalifu mkubwa, tukifanya hvyo ndivyo tunavyobarikiwa sisi, na familia zetu, tuzitendee haki ipasavyo kazi tunazozifanya.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mkuu wa Idara ya Utumishi Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bi Beatrice Augustino ameyasema hayo katika uzinduzi wa Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2022.

Maadhimisho hayo yamefunguliwa rasmi leo tarehe 23, Juni 2022 katika Kata ya Wasa na kukutanisha baadhi ya watumishi kutoka kata hiyo wakiongozwa na Mtendaji wa kata ya Wasa Ndugu Daudi Mohamedi, Watendaji wa Vijiji, baadhi ya Walimu kutoka shule za Msingi na Sekondari, Maafisa Kilimo pamoja na wataalamu wa Afya.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Kaimu Mkurugenzi Bi Beatrice amesema Ofisi ya Rais, Menejinenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ni Mratibu wa maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma nchini na maadhimisho haya ni moja ya matukio katika kalenda ya Umoja wa Afrika (AU) ambapo nchi wananchama huadhimisha kwa kufanya maonesho ya kazi mbalimbali na kongamano kuhusu masuala ya Utumishi wa Umma.

Aidha Amesema kuwa chimbuko la maadhimisho haya ni uamuzi wa Mkutano wa Mawaziri wenye dhamana ya Utumishi wa Umma uliofanyika Tangiers, Nchini Morocco mwkaa 1994, Uamuzi huu ulizitaka nchi za Afrika kusheherekea wiki hii kwa kauli mbiu moja kwa Bara zima la Afrika."Kauli mbiu ya Maadhimisho haya kwa mwaka 2022 ni Kuimarisha Ustahimilivu wa Utawala wa Umma katika Afrika ili kuwezesha utambuzi wa Mahitaji ya Lishe Afrika wakati na baada ya Janga la Corona".

Kauli mbiu ndogo ambayo imependekezwa kutumika kwa nchi yetu ni "Ni nafasi ya Mapinduzi ya Nne ya Viwanda katika masuala mapya yanayojitokeza kuhusu utoaji wa huduma na urejeshaji wakati  na baada ya janga la corona.

Kadhalika amesema kwa mwaka 2022, Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma yataadhimishwa kwa kuwatembelea watumishi na watendaji wa Taasisi za Umma walio katika maeneo ya pembezoni ili kuhimiza uwajibikaji wa hiari, kusikiliza changamoto zinazowakabili kiutendaji na kuzitatua.

Pia ameishukuru pia Serikali ya awamu ya sita kwa kufanya kazi nzuri, ndani ya mwaka mmoja wa awamu hiyo Halmashauri ya Wilaya ya Iringa pekee watumishi 1700 wamepandishwa vyeo, pia kwa mwaka huu wa fedha 2021/2022 malimbikizo mbalimbali ya mishahara tangu 2017 kwa takriban watumishi 500 wamelipwa kiasi cha Tsh. Biln 01.

"Tunamshukuru mama na Serikali kiujumla kwa jitihada na juhudi zao walizozionesha kwa Watumishi wa Umma, lakini pia tunamshukuru kwa jambo la mama ambalo kwa wengi wetu tunalisubiri kwa hamu pale mwezi wa saba".

Ushauri wangu, ninajua kuwa Watumishi wengi hapa lengo lao ni kufanya majazilizo ma kabla ya kufanya hivyo basi ninawashauri ni lazima uwe na mipango, kitu cha kwanza ni mipango halafu ndio kujaziliza, ikiwa kujaziliza itakuwa ya  kwanza hatutafanikiwa, maana ukishapata pesa matatizo yanakuja, kwa hyo nasisitiza mipango kwanza halafu ndio mengine yafuate. Ameongeza.

Amesema haki na wajibu vinaenda sambamba, madaraja, kima cha chini, madeni tumelipwa hivyo tufanye kazi kwa haki na wajibu."Kama unafikiri kazi hauielewi basi ni vyema kuuliza kwa watu sahihi, una changamoto uliza, maswali mengine ni mepesi sana ilaa tunapewa majibu magumu hivyo tuwasiliane kwanza". Amesisitiza.

Akizungumza katika Maadhimisho hayo Afisa TAKUKURU Mkoa Ndugu Ditram Muhoma amesisitiza juu ya suala la uadilifu kwa Watumishi na amewataka kutenda jambo bila kuambiwa au kusukumwa na kila mmoja atimize wajibu wake mahala pa kazi.

Akizungumza Kuhusu athari na madhara ya Rushwa kiutumishi amesema ni pamoja na kuwa na Watumishi wasiowajibika, wasio na sifa kutokana na masuala ya kutoa hongo ili kupata nafasi fulani na mwisho wa siku kupata watumishi amabao ni wabovu, lakini pia ni kupelekea kukosekana kwa fursa sawa kwa wote kutokana na wachache wao kupita mlango usio stahili, kubwa kuliko amesema kuwa ni kudhalilisha Utumishi wa Umma.

Ili kuepukana na hizi athari Ndugu Muhoma amesema watumishi wanatakiwa kuwa waadilifi, wenye staha, wachapa kazi wasiopendelea, wawazi, kuwa na utaratibu wa kupokea maoni pamoja na malalamiko kutoka kwa wananchi ambao ndio wateja wetu.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Mwanasheria wa Halmashauri Method Msokele amesema kuwa watumishi wengi wamekata tamaa kutokana na Watumishi wenyewe kutokujituma, kutokuwajibika kwa sheria pamoja na kuwepo kwa malalamiko ya kutokupandishwa vyeo.

"Tunatakiwa tuwe waaminifu, wawajibikaji kwa kuzingatia sheria na bila kuvuka mipaka, tuwe wawazi katika shughuli zetu za kiutumishi aidha tuwe waadilifu na tuwe huru."

Wakitoa changamoto mbalimbali na kero katika Maadhimisho haya baadhi wa Watumishi wametoa madai yao kama vile masuala ya kucheleweshewa mafao mbalimbali, uhaba wa watumishi katika Idara mbalimbali, uhamisho wa Watumishi, Malipo ya fedha za kujikimu kwa Watumishi, kadi za utambulisho wa Watumishi, Ubovu wa miundombinu pamoja na changamoto za TEHAMA.

Changamoto na kero zote zimetolewa majibu  na Wataalamu walioongozana na Kaimu Mkurugenzi Bi Beatrice Augustino lakini pia zingine zimechukuliwa kwa ajili ya kufanyiwa kazi.

Maadhimisho haya yameanza leo terehe 23.06 2022 na kutamatishwa tarehe 28.06.2022, yanatarajiwa kuendelea kuadhimishwa katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ikiwemo Idodi, Pawaga, pamoja na Kalenga.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa