• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Makatibu Tarafa, Watendaji wa KataVijiji na Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Kata Wanolewa Ukusanyaji Mapato

Imewekwa : November 4th, 2022

Makatibu Tarafa, Watendaji wa Kata, Vijiji na Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Kata Wanolewa Ukusanyaji Mapato

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja akiwa na Kamati ya Menejimenti ya Halmashauri hiyo, amekutana na Maafisa wote wa Tarafa na Kata kwa ajili ya kuweka mikakati ya ukusanyaji mapato tarehe 03/11/2022.

“Kama Kamati ya Menejimenti ya Halmashauri hii tumekubaliana tukae pamoja na kupeana maelekezo ya namna ya kuendesha Halmashauri. Katika mambo makubwa yanayotakiwa kufanyika ni ukusanyaji wa mapato na kusimamia miradi ya maendeleo, na kwamba jambo hili liwe na uelewa wa pamoja. Kila Afisa kwa anatakiwa kusimamia ukusanyaji mapato katika eneo lake na kwa uaminifu sana, kwani Halmashauri inategemea sana ukusanyaji wa mapato katika uendeshaji wake”. Haya yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wakati akiongea na Maafisa hao Ngazi ya Tarafa na Kata.

Sambamba na hilo Wakili Muhoja amewaambia Maafisa hao kuwa, wana mpango wa kupita kila Kata kwa siku tatu mfululizo, kwa ajili ya kukagua miradi ya maendeleo. “Tumeandaa mpango wa kupita kila Kata kutembelea na kukagua miradi inayoendelea. Hivyo muda ukifika tutapeana taarifa ili kila mmoja wenu ajiandae na kutoa taarifa kamili ya maendeleo ya mradi katika eneo lake, na kwamba siku ya Baraza la Madiwani itatakiwa kutolea taarifa ya kila mradi.”

Wakili Muhoja ameendelea kuwaasa Maafisa hao kuwa, waache tabia ya kujisemesha kwa wananchi kuwa ndiyo wameleta maendeleo ya ujenzi miradi inayoendelea. “mnajisema kwa wananchi kuwa ninyi mmeleta fedha kwa juhudi zenu, mimi kama Mkurugenzi wa Halmashauri sipendi unafiki wala majungu. Iwapo fedha za miradi zimefika nje ya bajeti huwa natoa taarifa kwa Waheshimiwa Madiwani ili kila mmoja wetu afahamu jambo hilo. Lakni Mtendaji anapojisifia kuwa yeye ndiye kaleta fedha za miradi unakuwa ni unafiki jambo ambalo halina afya kwa ustawi wa Halmashauri”.

Wakili Muhoja ameendelea kuwaambia Watendaji wa Kata kuwa, Walezi wa Kata watakapopita kwenye Kata wanatakiwa kutoa ushirikiano na kueleza uhalisia wa maendeleo ya Kata, hakuna haja ya kificho kwani hali halisi inajulikana.

Wakili Muhoja amewaasa Watendaji kutoa elimu kwa wananchi kutokana na uchumi na hali ya chakula. “Wananchi wasijisahau kuuza chakula hadi wakaishiwa, kwani hali siyo nzuri, lazima kuwepo na chakula cha akiba”

Ameongeza kusema kuwa, uandikishaji wa mbolea ya ruzuku ufuate sheria na haki bila kufanya upendeleo.

Kwa upande wa Maafisa Ngazi ya Kata nao walitoa changamoto zao, na Mkurugenzi Mtendaji amezichukua kwa ajili ya kuzifanyia kazi.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa