• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mamlaka ya Mawasilano Tanzania (TCRA) Nyanda za Juu Kusini yatoa mafunzo kwa Watumishi wa Umma jinsi ya kutumia mitandao mbalimbali

Imewekwa : September 21st, 2022

Mamlaka ya Mawasilano Tanzania (TCRA) Nyanda za Juu Kusini yatoa mafunzo kwa Watumishi wa Umma jinsi ya kutumia mitandao mbalimbali

Mamlaka ya hiyo imetoa mafunzo hayo jana katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ikijumuisha Watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Taasisi za simu (Vodacom, Tigo, Halotel na Airtel).

Akitoa salamu katika mafunzo hayo Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu Ndugu Deogratius Yinza amesema, “Sasa hivi Dunia inaenda kimtandao zaidi hasa kwa shughuli mbalimbali, hivyo tujitahidi kutumia fursa hizi za mtandao kwa manufaa yetu. Japo zipo changamoto nyingi kama utapeli kwenye simu, unyanyasaji, maudhui yasiyofaa kama picha za utupu, taarifa za uongo ushawishi mbalimbali na mengine mengi, inatupasa kujihadhari sana”.

Ndugu Yinza ameongeza kusema kuwa, kutuma nyaraka mbalimbali za Serikali kwenye mitandao siyo sawa, ni kosa kisheria, hasa zikiwa nyaraka za siri. Sekta ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ipo kisheria na ni Taasisi ya Serikali ina Taratibu na Miongozo yake.

Pia amewashukuru Watumishi wote waliohudhuria mafunzo haya na kuomba kuendelea kutumia mitandao kwa kujihadhari na matumizi sahihi.

Naye Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Nyanda za Juu Kusini Ndugu Asajile John Mwakisisile amesema, ‘Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ni Taasisi ya Serikali ambayo ilianzishwa mwaka 2003, ambapo inasimamia mawasiliano nchini’.

Pia Mamlaka hii inashirikiana na Mitandao ya Simu mbalimbali ambayo ipo nchini kote, na kushughulikia mambo mbalimbali yanayohusu matumizi ya simu, pia kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa watumiaji. Aidha, inatoa nafasi kwa watumiaji wa mitandao kutoa malalamiko yao na kuhakikisha yanashughulikiwa.

Serikali kupitia Sekta ya Mawasiliano inapata kodi yake kutoka kwenye vyombo vya simu. Hivyo Mamlaka in jukumu la kusimami watoa huduma na wanaohudumiwa katika suala zima la mawasiliano bila kuwaumiza watoa huduma na wapokeaji huduma.

Pamoja na maelezo mengi ya kazi za Mamlaka na Mawasilaino, Meneje alitoa nafasi ya kuuliza maswali, na maswali mbalimbali yaliulizwa na kujibiwa ipasavyo.

“Nina Imani baada ya mafunzo haya mtakuwa mabalozi wazuri kwa wananchi huko mtaani, kwa kuwaelekeza matumizi sahihi ya mitandao ya simu”, haya yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mh. Mohamed Moyo alipokuwa anafunga mafunzo haya na kusisitiza watumishi wawe wanafanya matumizi sahihi ya mitandao.

Pia Mh. Moyo amewaomba Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuleta mitandao (minara) ya simu katika Vijiji ambayo bado mawasiliano ni ya shida, na kufafanua baadhi ya Kata ambazo hazina mitandao kama Malengamakali, Kihanga, Nyang’oro, Masaka na kwingineko, ili wananchi waweze kunufaika na mawasiliano.

“Kuna faida kubwa sana kwa kupata mitandao, wanaanchi wanaweza kufanya biashara kupitia simu na kufanya shughuli zao kidigitali zaidi”, amesema Mh. Moyo.

Pia Mh. Moyo ameowaomba Mamlaka kuboresha miundombunu ya simu upande wa mtandao (networks), ili mtu afanye mawasiliano ya uhakika, kadhalika upande wa kupakua (downloads) vitu mbalimbali.

Mwisho amewashukuru Watumishi kushiriki mafunzo hayo kwa wingi na kwenda kuyafanyia kazi yale yote waliyojifunza na maswali ambayo walikuwa wanajiuliza.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa