Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa yamefanyika katika viwanja vya kijiji cha Makatapola kata ya Migoli mapema Aprili 28, 2025 ambapo Kimkoa yamepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba ukitokea Mkoani Dodoma kisha kukabidhiwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Kheri James kwa ajili ya kukimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.
Katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Mwenge wa Uhuru unakagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi yenye thamani ya shilingi Bilioni 4.4 sanjari na kupitia shughuli za klabu mbalimbali na vikundi vya wajasiriamali vijana.
Kijiji cha Ihemi
Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa
Simu ya mezani: 026-2702828/2702585
Simu ya mkononi: 0757 364 994
Barua pepe: ded@iringadc.go.tz
Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa