• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mhapa Awataka Watendaji kutoa Ushirikiano kwa Madiwani

Imewekwa : November 10th, 2022

Mhapa Awataka Watendaji kutoa Ushirikiano kwa Madiwani

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mhe. Stephen Muhapa amewataka Watendaji Kata Kutoa ushirikiano kwa Madiwani ikiwemo kuwataarifu kuhusu maagizo wanayoyapata na Miradi inayokwenda kutekelezwa katika Kata husika.

Ameyasema hayo katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Robo ya kwanza uliofanyika tarehe 09-10/11/2022 katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo, amesema katika utekelezaji wa miradi lazima kuwepo na ushirikiano baina ya Watendaji na Madiwani hivyo utoaji wa taarifa itasaidia kuboresha na kuchochea ukamilikaji wa miradi.

Pia amesema kuwa waheshimiwa Madiwani wana nafasi kubwa katika maendeleo ya Halmashauri hivyo wanapaswa kuzungumza na kujenga hoja zenye mashiko kwa Halmashauri.

Kadhalika amewata waheshimiwa Madiwani kuendelea kufanya kazi kwa ukaribu na wataalamu kutoka Halmashauri kwani Taasisi hiyo inajengwa na pande zote mbili yaani Baraza la Madiwani na Wataalamu hivyo ushirikiano ndio chachu ya maendeleo.

“… Hata shilingi ina pande mbili na ukitoa upande mmoja haitakua na thamani yoyote ndivyo hata sisi yatupasa tuwe, tufanye kazi kwa pamoja na kwa kushirikiana baina yetu sisi Madiwani na Wataalamu wetu.”

Aidha Waheshimiwa  Madiwani wamewasilisha taarifa za Kamati za kudumu za Halmashauri na taarifa za  utekelezaji wa Kata kwa kuwasilisha changamoto walizokumbana nazo kwa robo ya kwanza, miongoni mwa changamoto nyingi zilizowasilishwa ni Uhaba wa Watendaji wa Vijiji, Uhaba wa nyumba za Waalimu, na upungufu wa waalimu pamoja na uchakavu wa miundombinu.

Akijibu hoja hizo Mwenyekiti wa Halmashauri amewataka Waheshimiwa Madiwani kuendelea kusubiri wakati changamoto hizo zikiendelea kutatuliwa, Hapa kinachotakiwa ni uwezo wetu wa kibajeti kama bajeti yetu itaruhusu basi tutaangalia namna ya kutatua changamoto hizi na hatuwezi kuzitatua kwa mara moja tutaangalia tumepata kipi na tupeleke wapi. Amesema.

Naye Mbunge wa Jimbo la Ismani Mhe William Lukuvi ameshauri na kusema kuwa Waheshimiwa Madiwani wana nafasi ya kukutana na kujadili kuhusu upandishaji wa ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri kwa kufanya vikao na kuja na hoja za ni kwa namna gani tunaweza kupandisha ukusanyaji wa mapato yetu ili hata hizi chagamoto zetu tuweze kuzitatua kwa fedha zetu za ndani.

“kadri tutakavyokua tumekusanya mapato kwa kiasi kikubwa ndivyo tutakavoweza pia kupunguza uchangishaji kwa wananchi na tutakuwa na uwezo wa kukamilisha miradi hiyo sisi wenyewe.”

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja amewashukuru Madiwani kwa kuchangia hoja zenye mashiko kwa Halmashauri na kuwaomba watoe ushirikiano katika Miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Kata zao ikiwemo Miradi ya ujenzi wa madarasa ya kidato cha kwanza 2023.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Iringa Vijijini Mhe. Costantino Kiwele amesema kuwa anawapongeza Halmashauri kwa kuendelea kuratibu na kusimamia zoezi la utoaji wa chakula kwa wanafunzi mashuleni kwani ni ajenda ya kitaifa.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa