• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mheshimiwa Moyo azindua zoezi la Upandaji Miti Halmasahuri ya Wilaya ya Iringa

Imewekwa : March 3rd, 2022

DC Moyo azindua zoezi la Upandaji Miti Halmasahuri ya Wilaya ya Iringa

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Mohamed Hassan Moyo amezindua zoezi la upandaji miti ambalo limefanyika katika Tarafa ya Mlolo, Kata ya Masaka, Kijiji cha Sadani eneo la Shule ya Sekondari Mseke tarehe 03/03/2022.

Akizindua zoezi hilo Mheshimiwa Moyo amesema, miti takribani mia moja imepandwa katika eneo hilo, huku Kauli Mbiu ya Mwaka Huu ni : "Miti Mazingira Yangu, Tanzania Yangu, Naipenda Daima", ambapo inakadiriwa kupandwa miti milioni moja na laki tano kila mwaka.

Katika hotuba yake Mheshimiwa Moyo amefurahishwa na mahudhurio ya wananchi kwa kushiriki uzinduzi huo, amesema “Mkusanyiko huu wa wananchi unaonesha wazi kuwa, mmejidhatiti katika shughuli hii ya upandaji miti”.

Aliongeza kusema kuwa malengo ni kupanda miti milioni moja na laki tano kila mwaka, hii itasaidia kuboresha hali ya hewa na wananchi  kujikwamua kiuchumi kutokana na shughuli hii ya ulimaji miti.

“Upandaji wa miti ulishaanza na utaendelea hadi mvua zitakapokoma”.

Ili kuboresha kilimo cha miti ni lazima kuzingatia kupalilia, kulinda miti, kuzuia moto, pia kuwa wavumilivu ili kuvuna baada ya muda uliopangwa kitaalamu, amesisitiza.

Wakati huohuo Mh. Moyo ametoa maagizo kwa wananchi kuwa, kuna wafanyabiashara ambao si waaminifu wanauza mbolea ambayo si halisi, na kupelekea kuwadanganya wananchi. Amewataka wananchi kutoa taarifa kwa viongozi wa Serikali au Polisi mara wanapobaini kuna mtu wa namna hiyo.  

Lakini pia ametoa msisitizo kwa wananchi kutoa ushirikiano katika suala zima la anuani za makazi, Sensa ya Watu na Makazi, pamoja ugonjwa wa UVIKO – 19 ili watu wakapate chanjo, kwani zinapatikana bure katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Ponsiano Kayage amewapongeza wananchi wa Kata ya Masaka kwa kukubali kufanyika uzinduzi katika eneo lao, na kuwataka kuwa mfano wa Kata zingine katika shughuli ya upandaji miti.

“Miti ni uhai wa viumbe vyote duniani, hivyo madhara ya ukataji miti tunatambua. Yatupasa kuwajibika kupanda miti kila wakati”, amesema.

Naye Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bi. Lucy Nyallu amempongeza na kumshukuru Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Moyo kwa kukubali kuwa Mgeni Rasmi katika zoezi hili la uzinduzi wa upandaji miti.

Aidha amesema kuwa, zoezi hili lilianza kufanyika mapenda mwaka huu na leo ilikuwa ni siku ya uzinduzi tu, na kwamba zoezi hili litakuwa endelevu.

Akitoa taarifa ya uzinduzi wa upandaji miti Afisa Misitu wa Wilaya Ndugu. Joachim Mshana amesema, shughuli ya upandaji miti hufanyika kila tarehe 1/04, lakini katika ngazi ya Halmashauri imeadhimishwa leo tarehe 03/03/2022.

“Katika miaka mitano iliyopita ilipandwa miti 10,367,967 lakini miti ilipona na kukua vizuri ni 6,682,000 sawa na 49%.”

Pia Ndugu Mshana amewashukuru wadau mbalimbali kwa michango yao katika kufanikisha shughuli hii ya upandaji miti wakiwemo, Mfuko wa Misitu Tanzania (TAFF), Wakala wa Huduma za Misitu(TFS), One Acre Fund, Clino Development Initiative, world vision, Forest Development Trust na Panda Miti Kibiashara.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa