• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkaa na Kuni Sasa Basi

Imewekwa : November 1st, 2022

Mkaa na Kuni Sasa Baaasiiii!

Mjadala wa siku mbili wa tarehe 01 – 02 Novemba, 2022 umeandaliwa kujadili matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia katika jamii yetu.

Mjadala huo ambao umeandaliwa na Wizara ya Nishati ukiongozwa na Waziri mwenye dhamana Mheshimiwa Januari Makamba, na kufunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, umesisimua wajumbe na washiriki kwa kutoa mawazo chanya juu ya nini kifanyike katika kuendeleza nishati hii ya gasi.

Akizungumza katika hotuba yake ya ufunguzi Mheshimiwa Rais amesema” mjadala huu ni wa kihistoria na umkuja wakati muafaka katika kipindi hiki cha kizazi cha sasa. Mkutano huu ulipangwa kuhudhuriwa watu 1000 lakini kutokana na umuhimu wake watu zaidi ya 3000 wameweza kujiandikisha, hii inaonesha kuwa watu wana juu ya jambo hili”

Mheshiwa Rais ameendelea kusema kuwa, “nawapongeza Mikoa yote iliyoshiriki katika mkutano huu kwa njia ya mtandao ambayo ni Dar es salaam,Shinyanga, Iringa na Tabora. Nawakaribisha kutoa mawazo yenu ili kuleta mtazamo chanya katika matumizi ya gesi nyumbani”

Mheshimiwa Samia ameendelea kusema, “kwa nini nishati safi? Kwa sababu njia hizi zinazotumika sasa za kupikia mkaa na kuni huleta changamoto kiafya, na Wataalamu wametueleza athari za kutumia njia hizi.” Mh. Samia amesema.

Pia tatizo la mazingira, mgao wa umeme na maji hii yote husababisha na ukataji miti na kuchoma mkaa na kusema kuwa, Mkoa wa Pwani unaoongoza kwa kukata miti na kusababisha matatizo na kukauka kwa mito hasa mto Ruvu.

“Tunapokata miti tunasababisha gharama kubwa za maisha zaidi, mfano kwa mwanamke kienda kutafuta kuni anaweza akabakwa huko porini, unapigwa kwa sababu ya kuchelewa kurudi nyumbani, kukutana na wanyama wa pori na kuweza kuwadhuru, na mambo mengine yanayohatarisha maisha yao na matumizi ya kuni huhatarisha afya”.

Kubwa moja ni kubadilisha mtazamo ambapo kwa mfano nyumba uzuri lakini lazima ujenge jiko la nje, ili tu uweze kutumia jiko la kuni. Sasa hivi si jambo la kufumbia macho ni lazima tutekeleze afua hizi za nishati. Takwimu zinaonesha wananchi wanaotumia nishati ya gasi ni 5% umeme 2%.

Mheshimiwa Rais ameelekeza kuwa, utatuzi wa Kisera umechukulia suala hili si la muda mfupi, lazima tuanze sasa tena kwa kasi kubwa. Kianzishwe kikundi kazi ambacho kitashughulikia nishati safi, na si kwa Serikali peke yake, pamoja na Sekta Binafsi, Maendeleo ya Jamii na TAMISEMI kusikilize Sekta Binafsi wanasemaje kwani ndiyo fursa yao katika jambo hili.

Kikosi kazi hiki kitakuja na suala moja la suluhu ya mpango wa matumizi ya nishati safi na endelevu. Kikosi kazi hiki kitaratibiwa na Wizara ya Nishati.

Mheshimiwa Rais pia amesema ni lazima twende na nishati safi ya kupikia kukinga wanawake ambao wanapata madhara makubwa na hawalipwi chochote, sasa angalau tuwapunguzie madhara wanayopata. Pia itasaidia kupata muda wa kufanya shughuli la kiuchumi. Kikosi kazi hiki kitakuwa cha Kitaifa ambacho kitaratibiwa Kitaifa zaidi. Tanzania tumejiingiza kwenye mambo kadhaa kwa mpango wa Women Rights in Justice hii itampa mwanamke muda wake, kwamba sisi ni Machampion. Mkakati huu utadumu miaka 10 ili 80-90% wawe katika nishati safi ya kupikia, kinachotakiwa ni kutoa elimu kwa wananchi ili waelewe madhara ya kutumia kuni na  mkaa.

Sisi Serikali tutafanya bajeti ambayo itaanzisha Mfuko wa Nishati Safi ya Kupikia kama ilivyo kwenye Kampeni ya Kumtua Mama Ndoo ambayo imefikia 80%. Mpango huu utatoa mchango wa Mashirika ya Wadau wa Maendeleo.

Mikoa inayoongoza kwa kukata miti ya asili ni Pwani, Morogoro, Tabora, Lindi na Ruvuma kwa kisingizio ni bei rahisi ya mkaa. Miti mingi tunayotakiwa kupanda ni miti ya matunda. Hii itasaidia kuzalisha asali ambayo ni hitaji la Dunia.

Nilielekeza kuwa Taasisi zinazotumia zaidi ya watu 300, ni lazima watumie Gesi ili kuzuia kutumia nishati chafu. Ifikapo 2024, nataka nisimame kwa wananchi kuwa nimefanya mambo mbalimbali ikiwemo jambo hili la nishati safi ya kupikia.

Mheshimiwa Rais amemaliza kwa kusema, “Tunahitaji nishati safi na salama ya kupikia kwani italeta ufanisi wa Afya Bora kwa Jamii Yetu”.

Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluh Hassani kufungua mjadala wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Halima Dendego ameongoza mjadala huo kwa kushirikiana na Wakuu wa Wilaya waliopo Mkoani humo.

Katika mjadala huo Wakuu wa Wilaya, Wenyeviti wa Halmashauri, Makamu Wenyeviti na wadau mbalimbali, wameweza kutoa ushauri juu ya nini kifanyike ili kuweza kuepukana na ukataji wa misitu na ni namna gani kama Watanzania tunaweza kuongeza matumizi ya gesi ya nyumbani.

Moja ya ushauri waliotoa Wadau kwa Serikali ni kuweza kuweka ruzuku kwenye gesi na vifaa vyake jambo ambalo litapelekea gesi kuuzwa kwa bei ya chini ambapo wananchi wengi wataweza kununua na kuachana na matumizi ya kuni na mkaa.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa