• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkurugenzi Iringa DC Awataka Watumishi Kuepuka Mikopo ya Mitaani

Imewekwa : January 2nd, 2023

Mkurugenzi Iringa DC Awataka Watumishi Kuepuka Mikopo ya Mitaani 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bahir Muhoja amewataka watumishi kuwa makini na mikopo ya mitaani ambayo ina riba kubwa kuliko hata mkopo wenyewe.

Wakili Muhoja ameyasema hayo mapema leo tarehe 02, Januari 2023 alipofanya kikao na watumishi wa Halmashauri kwa robo ya pili mwaka wa fedha 2022/2023 kujadili utendaji kazi, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri (Siasa ni Kilimo).

Amesema watumishi walioomba mikopo hadi sasa ni 88 na fedha iliyokuja kwa ajili ya kukopesha watumishi ni milioni 300 na jumla ya kiasi kilichoombwa ni Bilioni 1.68 hivyo kuna baadhi waombaji itabidi wakose

Katika kikao hicho mada mbalimbali zimewasilishwa ikiwemo Malezi ya Watoto na unyanyasaji wa kijinsia pamoja na Lishe. Akiwasilisha mada ya unyanyasaji wa kijinsia Afisa Ustawi wa Jamii Bibi Gladness Amulike amewataka watumishi kukataa kutumika ili kupata wepesi katika jambo fulani mathalani cheo au madaraka.

“Wewe kama Mtumishi usikubali kutumika kufanya mapenzi kazini ili usaidiwe huo ni udhalilishaji, lakini pia msikubali kushikwa sehemu zisizofaa na wakuu wa kazi”.

Kadhalika amesema kuwa ili kuzuia ukatili mahala pa kazi inabidi mtumishi anapoona kuna dalili za ukatili atoe taarifa (katika Idara ya Utawala au Dawati la malalamiko (Afisa Kero), lakini pia kuwepo na elimu ya mara kwa mara kwa watumishi kuhusu ukatili mahali pa kazi.

Naye Afisa Lishe wa Halmashauri Bibi Tiliza Mbulla amewataka watumishi kuzingatia ulaji sahihi wa chakula kwani chakula kina virutubisho ambavyo vinasaidia kuzalisha nishati kwa ajili ya mwili ikiwemo ukuaji na kuendesha mifumo ya uzazi.

“Hali ya kiafya inatokana na ulaji wa mtu hivyo hali inaweza kuwa mbaya au nzuri kutokana na ulaji wa mtu husika”.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmasahuri Wakili Muhoja amesema ni lazima kwa watumishi kujali afya zao wakiwa maeneo ya kazi lakini pia ni alzima kujali utu wa watumishi na familia zao kwani mtumishi akiwa mgonjwa basi hawezi kufanya kazi kwa ufasaha.

Aidha amewapongeza  watumishi kwa kazi nzuri katika nyanja zote amesema tumeanza mwaka vizuri na anatumaini watafanya vizuri zaidi.

“Ukusanyaji wa mapato umeshuka hivyo tujitahidi kukusanya mapato vizuri, kadhalika madeni na stahiki za watumishi zilipwe lakini kubwa zaidi ni nidhamu hasa kwa viongozi na wakuu wa kazi ikiwemo kuwepo kazini, kufanya kazi na kupokea maelekezo.”

Pia Wakili Muhoja amelizungumzia suala la maandalizi ya kuhamia Makao makuu ya Halmashauri yaliyojengwa katika Kijiji cha Ihemi Kata ya ifunda amesema ujenzi unaendelea kukamilika na bado ujenzi wa ukuta ambapo hadi kufikia mwezi aprili tutakuwa tumeshahamia na kuhusu samani zitanunuliwa.  

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa