• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA WAKILI MUHOJA AKIHUTUBIA KATIKA UFUNGUZI WA MAFUNZO YA SIKU TATU KWA WAWEZESHAJI WA TASAF HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA

Imewekwa : May 10th, 2022

Siku Tatu za TASAF Iringa DC Kuwapa Madini Wawezeshaji kuhusu Warsha za Jamii

Na Ofisi ya Habari na Uhusiano Iringa DC

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja amefanya ufunguzi wa mafunzo ya kujenga uelewa kuhusu uendeshaji wa warsha za jamii, Ufanisi wa zoezi la malipo, Masharti ya Elimu/Afya na majukumu ya usimamzi kamati ya usimamizi CMC.

Ufunguzi huo umefanyika katika Ukumbi wa Ofisi za Mipango zilizopo katika Jengo la Siasa ni Kilimo ambapo mafunzo hayo yatadumu kwa muda wa siku tatu kuanzia tarehe 10 hadi tarehe 12 Mwezi Mei 2022.

Katika ufunguzi huo Mkurugenzi Mtendaji Wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja ambaye amekuwa Mgeni rasmi wa ufunguzi huo ameshukuru uongozi wa TASAF kwa kumpa fursa hiyo na kumfanya kujumuika pamoja katika ufunguzi huo.

Amesema warsha za jamii ni mikutano inayoandaliwa na kufanyika ili kuwajengea walengwa wa mpango uelewa wa mada muhimu zitakazosaidia kubadaili mtazamo na fikra kwa nia ya kujiletea maendeleo.

"Uwepo wa warsha za jamii zitatumika kuhusisha taarifa za kaya na walengwa kutoa na kubadilisha mawazo na uzoefu. Maafisa ugani waliopo ngazi ya kata ndio wanajukumu la kuendesha warsha za jamii".

Kuhusu ukosefu wa elimu miongoni mwa walengwa juu ya warsha hizi na ufanisi wa zoezi la malipo na masharti ya elimu na afya Mkurugenzi amesema;

"Ndugu washiriki elimu kwa walengwa inabidi itolewe kila wakati na wawezeshaji wetu ambao mko hapa leo. Mtapimwa kwa kuangalia mafanikio ya walengwa".

Aidha Mkurugenzi Wakili Muhoja amesisitiza kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji katika ngazi ya jamii kwa kuhakikisha watumishi wanafuatilia shughuli za mfuko wa maendeleo ya jamii hasa zile zinazohusu ustawi wa walengwa ili zilete tija.

Kwa Upande wake Muwakilishi wa Mkurugenzi wa TASAF, Bibi Irene Shayo amewashukuru washiriki waliofika kupata mafunzo hayo na kuwataka kuwa makini kwa kipindi chote cha mafunzo ili mwisho wakafanye kazi kwa uadilifu na umakini ili kufikia malengo ya serikali.

Akiwasilisha mada mbalimbali amesisitiza na kutoa ufafanuzi juu ya umuhimu wa warsha za jamii kwa walengwa pamoja na umuhimu wa kuzingatia muda katika ufanyikaji wa warsha hizo ili kufanikisha shughuli hizo kwa wakati

"Ni lazima kuwepo na ratiba maalumu kuhusu warsha za jamii mtakazokuwa mnazifanya hii itasaidia kuwepo kwa mpangilio na kufahamu nini kifanyike kwa wakati gani na kwa kiasi gani". Amesisitiza.

Kadhalika amezungumzia matumizi sahihi ya lugha kwa walengwa kwani inaweza kupelekea kuzuka kwa mtafaruku baina ya Mlengwa na Mratibu kusipokuwepo kwa matumizi mazuri na sahihi ya lugha.

Mnapokwenda katika warsha za jamii mzingatie lugha nzuri na yenye utu ndani yake msiwaite vilema ni watu wenye ulemavu na sio Kipofu ila ni Mtu mwenye uoni hafifu au asiyeona kabisa, Amesisitiza.

Mratibu wa Mpango Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bibi Agatha Lugome ametoa maelekezo kwa washiriki wa mafunzo kuwa makini na kuzingatia kanuni za mafunzo lakini pia kuwa makini kipindi chote cha mafunzo ili kuleta ufanisi mzuri wakati wa utekelezaji katika vijiji.

Aidha akijibu changamoto mbalimbali zilizoainishwa na washiriki na kuonekana kuwa vikwazo kwenye utekelezaji wa kuwahudumia walengwa wa mpango Bi. Agatha amesema changamoto ni nyingi lakini kubwa ni kutokuzingatiwa kwa muda na kupelekea kuibuka kwa changamoto zingine.

"Tatizo kubwa hapa ni muda na hili linatokana na uhaba wa magari ambayo yamekuwa kikwazo ila ninaahidi kuyafanyia kazi ili kutokujirudia kwa wakati mwingine".

Washiriki pia wamepata nafasi ya kutoa matarajio yao mara baada ya mafunzo na wengi wao  wameonesha kufurahishwa na mafunzo haya na kutaja matarajio chanya katika utendaji kazi wao.

Warsha hizi zitafanyika mara moja kila baada ya miezi miwili kulingana na mzunguko wa dirisha la malipo na litafanyika katika vituo vya malipo, walengwa watatakiwa kuhudhuria bila kukosa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI - MBOMIPA March 18, 2023
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA KWA ROBI YA PILI KWA MWAKA FEDHA 2022/2023. January 16, 2023
  • ZIARA YA MKUU WA MKOA WA IRINGA December 14, 2022
  • Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA YA IRINGA AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUBORESHA SEKTA YA ELIMU

    March 24, 2023
  • WATENDAJI KATA WILAYANI IRINGA WAAGIZWA KUSIMAMIA UTOLEWAJI WA CHAKULA SHULENI

    March 20, 2023
  • ZAIDI YA MADAWATI 162 YATOLEWA KWA SHULE YA SEKONDARI KIDAMALI NA SHAFA AGRO COMPANY LIMITED

    March 18, 2023
  • Maandalizi ya Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2023

    March 14, 2023
  • Tazama zote

Video

FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA POLIO, DALILI NA NJIA ZA KUJIKINGA
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Gangilonga

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0767778106

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa