Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Kheri James amefanya ziara ya kukagua miradi pamoja na kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika Tarafa ya Idodi Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mei 12, 2025
Mhe. Kheri James ametembelea na kukagua kazi ya maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Iringa - Msembe inayojengwa kwa kiwango cha lami ambapo maandalizi ya awali yameshaanza kwa ujenzi wa kambi na kusembua njia za mchepuo.
Akizungumza na wananchi pamoja na wasimamizi wa kazi, Mhe. Kheri amewahakikishia madereva kuwa mchakato wa kuwapata madereva utakuwa wazi na utatangazwa hivyo wenye sifa wataomba kazi na kufanyiwa majaribio bila upendeleo wowote.
Maeneo mengine ambayo Mkuu wa Wilaya ametembelea ni viijiji vya Mapogolo na Malizanga ambapo ameweza kusikiliza na kutatua kero za wananchi kupitia mikutano ya hadhara. Masuala yaliyoangaziwa zaidi ni ardhi na migogoro ya wakulimabna wafugaji katika maeneo haya.
Eidha Mhe. Kheri amesisitiza kuwa wananchi wanapaswa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa ikiwa wanahitaji maeneo ya makazi, kilimo au ufugaji ili kuepusha migogoro inayoweza kujitokeza sanjari na kuzingatia matumizi bora ya ardhi.
Ziara hii ni mwendelezo wa ziara zinazotarajiwa kuvifikia vijiji yaani kijiji kwa kijiji ili kusikiliza na kutatua kero za wananchi sanjari na ukaguzi wa miradi ya maendeleo.
https://www.instagram.com/p/DJnzBdyM6Mi/?igsh=bTg4aTE5ejFid2E2
Kijiji cha Ihemi
Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa
Simu ya mezani: 026-2702828/2702585
Simu ya mkononi: 0757 364 994
Barua pepe: ded@iringadc.go.tz
Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa