• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA MHE. STEPHEN MHAPA AKIWASILISHA TAARIFA ZA UTEKELEZAJI WA KATA YA NZIHI KATIKA MKUTANO WA BARAZA LA WAH. MADIWANI ULIOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA SIASA NI KILIMO

Imewekwa : May 10th, 2022

Mhe. Mhapa Asisitiza Mahusiano na Mawasiliano Mazuri baina ya Wahe. Madiwani na Wataalamu kutoka Halmashauri

Na Ofisi ya Habari na Uhusiano,Iringa-DC

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mhe. Stephen Mhapa ameongoza Mkutano wa Baraza la Madiwani Robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2021/2022 katika ukumbi wa Halmashauri siasa ni kilimo 10/05/2022.

Akitoa taarifa Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Mhapa amewashukuru Wah. Madiwani kwa kuendeleza ziara za kikazi na amethibitisha Baraza kupokea taarifa za utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kimaendeleo za kata kwa robo ya tatu Machi hadi Mei 2021/2022.

Katika kuwasilisha taarifa hizo za maendeleo ya kata Waheshimiwa Madiwani kutoka Kata mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kwa kiasi kikubwa wameshukuru Serikali kwa kuwaletea fedha za maendeleo lakini pia wamemshukuru Mwenyekiti, Mkurugenzi na Wataalamu kutoka Halmashauri kwa ushirikiano wanaouendeleza ili kufanikisha shughuli za maendeleo kwa kila Kata.

Waheshimiwa Madiwani kutoka Kata mbalimbali wamewasilisha taarifa zao kwa mtindo wa kusoma changamoto ili kuwafanya wataalamu kuwa na uelewa ni wapi pa kuanzia, kuongeza nguvu na kutafuta njia mbadala katika kutatua changamoto hizo.

Miongoni mwa changamoto zilizowasilishwa kutoka Kata mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ni pamoja na Suala la ubovu wa bararabara kutokana na mvua zilizonyesha zimekuwa na athari kali, ukosefu wa maji ambayo kiujumla  inaathiri shughuli za kimaendeleo

Upungufu wa maji, ukosefu wa hosteli, upungufu wa matundu ya vyoo, uchakavu wa vyoo, ukosefu wa nyumba za walimu na wataalam wa afya, ukosefu wa walimu wa kike, upungufu wa watendaji wa Vijiji, Ukosefu wa usafiri kwa wataalamu n.k

Wakiwasilisha changamoto hizo Wah. Madiwani wameiomba Halmashauri iweze kusaidia na kutia nguvu maeneo hayo yenye changamoto ili kupunguza kama sio kumaliza kabisa matatizo hayo ambayo yameonekana kuwa kikwazo cha maendeleo ya Kata na Halmashauri kiujumla.

Akitoa msisitizo kwa yaliyowasilishwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mhe. Mhapa amesema; kwa ujumla wake tumeona bado tuna tatizo kubwa la umeme katika vitongoji vyetu tujue ni vingapi havina umeme na hii itatusaidia katika utoaji wa taarifa katika vikao mbalimbali ikiwemo kikao cha wilaya

Lakini pia amesema tuna tatizo kubwa la umaliziaji wa majengo mbalimbali ya zahanati, nyumba za walimu, madarasa, mabweni ninaomba hilo lote liwekwe sawasawa, wananchi wamejitihadi kwa nafasi zao hivyo serikali lazima itambue,

"Na ikiwezekana  majengo yote yapigwe picha kwa ajili ya kumbukumbu na ipelekwe serikalini ili na wao pia watusaidie tulipoishia".

Watendaji wa vijiji nao ni changamoto kubwa  na shughli za maendeleo zinahitaji watendaji wa Vijiji ili waweze kuhamasisha na kusimamia shughuli hizi za kimaendeleo, tunatakiwa tujue ni namna gani tunapata hawa watendaji, lazima tuchukue hatua za ziada. Amesisitiza.

Pia Mwenyekiti Mhe. Mhapa amewaagiza Wakuu wa Idara kufuatilia na kuleta majibu juu ya hoja na changamoto zote zilizowasilishwa na kuwataka Waheshimiwa Madiwani kusimamia fedha za serikali zinazoletwa, kuhakikisha shughuli zinafanyika na kujitahidi kusemea.

Akifunga Mkutano wa Baraza la wah. Madiwani kwa siku ya kwanza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mhe. Mhapa ametoa shukrani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bashir Muhoja na wataalamu wa Halmashauri.

 "Niwashukuru sana Mkurugenzi na wataalamu, tumeshuhudia madiwani takribani wote wamewashukuru sana na mimi naungana nao kuwapongeza, niwatake wataalamu kuwa na mawasiliano mazuri na madiwani ili kuleta ufanisi katika shughili za kimaendeleo.

Mkutano wa Baraza la Wah. Madiwani linatarajiwa kukutana tena kwa siku ya pili tarehe 11/05/2022 kwa ajili ya maswali ya papo kwa papo na kupokea taarifa mbalimbali za Kamati za Kudumu za Halmashauri.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI - MBOMIPA March 18, 2023
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA KWA ROBI YA PILI KWA MWAKA FEDHA 2022/2023. January 16, 2023
  • ZIARA YA MKUU WA MKOA WA IRINGA December 14, 2022
  • Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA YA IRINGA AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUBORESHA SEKTA YA ELIMU

    March 24, 2023
  • WATENDAJI KATA WILAYANI IRINGA WAAGIZWA KUSIMAMIA UTOLEWAJI WA CHAKULA SHULENI

    March 20, 2023
  • ZAIDI YA MADAWATI 162 YATOLEWA KWA SHULE YA SEKONDARI KIDAMALI NA SHAFA AGRO COMPANY LIMITED

    March 18, 2023
  • Maandalizi ya Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2023

    March 14, 2023
  • Tazama zote

Video

FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA POLIO, DALILI NA NJIA ZA KUJIKINGA
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Gangilonga

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0767778106

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa