• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

NEMC, WAMILIKI WA KUMBI ZA STAREHE WAKUTANA NA RC

Imewekwa : July 3rd, 2023

NEMC, WAMILIKI WA KUMBI ZA STAREHE WAKUTANA NA RC

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Halima Dendego amefungua na kufanya kikao na wataalamu kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Viongozi wa serikali, na wamiliki wa kumbi za starehe na baa katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo Iringa tarehe 03.07.2023.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Dendego amesema “kumekuwa na malalamiko mengi katika jamii zetu, malalamiko ya wagonjwa hawalali hata sisi wenyewe kawaida hatulali lakini pia upande wa pili kuna wenzetu wamewekeza na wanahitaji kupata kile walichowekeza kutokana na uwekezaji huo kwa hiyo kwa kutambua hilo Serikali imetutaka tukae pamoja lengo ni kujenga na sio kubomoa”.

Mhe. Dendego ametaka mazungumzo yafanyike kwa kuzingatia maslahi ya pande zote ili wafanya biashara wafanye kazi zao na wanufaike na uwekezaji wao, vilevile jamii nayo isipate usumbufu kutokana na kelele zinazozalishwa.

Kwa upande wa Mipango Miji Mhe. Dendego amesema, “Mpaka tumefika hapa lazima tujitathmini, tuna tatizo sana kwenye suala zima la Mipango Miji katika Miji yetu, ambayo haijapangiliwa kulingana na mahitaji yetu. Katikati ya makazi kuna nyumba za Ibada, masoko, nyumba za starehe, magenge nk. Hii sio sahihi”. Amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kulifanyia kazi suala hili la Mipango Miji hasa kwa maeneo ambayo bado hayajasongamana.

Naye Mtaalamu kutoka NEMC ametoa wasilisho lake la masuala ya mazingira amesema, “kuna viwango vya kelele ambavyo havitakiwi kwenye maeneo mbalimbali mfano eneo la makazi, viwanda, maeneo ya starehe n.k hivyo wamiliki wa kumbi za starehe na baa mnatakiwa kuwa na vifaa vya kupima viwango vya kelele ili kutovuka kiwango elekezi kutokana na eneo”.

Kwa upande wao wamiliki wa kumbi za starehe wamekubaliana na wasilisho lililotolewa na kuomba kuwa elimu hii iwe endelevu ili kuwafikia wadau wengi zaidi yaani washereheshaji, wamiliki wa kumbi na waongoza mziki (DJ), ili kuwa na uelewa wa pamoja na kurahisisha utekelezaji wake jambo ambalo limekubaliwa na kupokelewa.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa