• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Pichani ni Wajumbe wa kamati ya Elimu,Afya na Maji ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wakiangalia jengo la utawala lililokarabatiwa katika shule ya sekondari Tosamaganga ikiwa ni miongoni mwa majengo yaliyofanyiwa ukarabati katika shule hiyo.

Imewekwa : June 11th, 2020

Halmashauri ya Wilaya ya Iringa yaishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kukarabati shule Kongwe.

Na Ummi Mohamed (Afisa Habari na Uhusiano,Iringa- DC)

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bw. Wapa Mpwehwe amesema Serikali ya awamu ya tano imetoa fedha kiasi cha shilingi Bilioni 1.4 kwa ajili ya kukarabati majengo ya shule kongwe za sekondari Tosamaganga na Ifunda wasichana kwa mwaka wa fedha 2019 /2020 na ukarabati huo unaendelea.

Akitoa ufafanuzi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bw.Mpwehwe amesema serikali imetoa milioni 650 kwa ajili ya ukarabati shule ya Sekondari ya Tosamagana na milioni 767 kwa ajili ya shule ya Sekondari ya Ifunda wasichana.

“Ukarabati katika shule hizi mbili unafanywa na serikali bila kuhusisha nguvu ya wananchi na kama ambavyo mmeona kazi iliyofanyika na inayoendelea kufanyika katika ukarabati huu”amesema Bw. Mpwehwe.

Kwa upande wake Mwnyekiti wa kamati ya Elimu,Afya na Maji Mh Bruno Kindole alisema;

“Naipongeza sana Serikali kwa kutenga fedha hizi kwa ajili kukarabati miundombinu ya shule hizi kongwe na kuzifanya ziwe na mandhari zinazovutia kujifunza, lakini nampongeza sana Mkurugenzi Mtendaji Bw.Robert Masunya kwa kushirikiana na Wataalam wake wanafanya kazi nzuri sana katika Halmashauri yetu hasa katika miradi ya maendeleo”alisema.

Aidha, Mh.Kindole alitembelea pia,mradi wa kituo cha Afya cha kimkakati kinachojengwa  katika Kata ya Ifunda kijiji cha kibena na kujionea mradi wa kituo cha afya ulioanzishwa kwa nguvu ya wananchi.

 “Binafsi nimefurahishwa sana na jinsi mlivyojitoa katika suala la maendeleo kwa kujenga hili boma kwa kweli mnastahili sana kupongezwa”alisema na kuongeza;

 “Serikali hailali inaona na inafanya kazi sana, iwapo wananchi wanaibua na kuanzisha miradi ya maendeleo katika maeneo yao Serikali haisiti kuweka nguvu ikibaini wananchi kweli wanauhitaji wa huduma wanayoianzisha na ndio maana kiasi hiki cha milioni 200 kimeletwa hapa katika kijiji cha Kibena baada ya kuibua mradi huu wa kituo cha Afya”alisema.

Mh Kindole amesema uongozi wa Kijiji hiko uwe mfano wa kuigwa na vijiji vingine katika shughuli za maendeleo na ameipongeza serikali ya kijiji cha Kibena kwa kuonyesha Ari ya kupenda maendeleo hasa kwa jinsi walivyojitoa katika kuanzisha ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kimkakati.

Wakati huo huo,Diwani wa Kata hiyo Mh.Elikus Ngweta ameitoa hofu Kamati hiyo na  amewahakikishia wajumbe kuwa wananchi hao wanapenda maendeleo na wamedhamilia kukiletea kijiji chao maendeleo hivyo watajitoa kila watakapo takiwa kufanya hivyo.

“Utendaji wa ushirikishaji wa jamii umepelekea wananchi kuwa waelewa na hasa kijiji hiki sio wavivu kabisa tena ujenzi ukikamilika kituo hiki cha afya kiitwe Kibena kwa kuwa wananchi wa kijiji hiki tu ndio wamejitoa katika kata nzima yenye vijiji sita”alisema Mh Ngweta.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa