• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RC Dendego Alia na Mamba Mtera

Imewekwa : January 11th, 2024

RC Dendego Alia na Mamba Mtera

Matukio ya watu (wavuvi) kuliwa na mamba katika Bwawa la Mtera lililopo Kata ya Migoli, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mheshimiwa Halima Dendego amefanya ziara kwenye Kata hiyo na kuweza kuongea na wananchi wanaovua katika bwawa hilo Januari 10, 2024.

Mheshimiwa Dendego amesikiliza maoni yao na kutaka kufahamu nini kifanyike ili kukabiliana na mamba hao, ambapo wananchi hao wamemuomba kutumia silaha za asili kama ndoano ili kuwanasa mamba hao, kwani silaha kama bunduki zimeshindwa kufanya kazi majini.

Akipokea maoni ya wananchi hao Mheshimiwa Dendego ametoa maagizo kwa viongozi wa maeneo hayo kuwataka kuanza kazi mara moja ya kutega ndoani hizo kwa kushirikiana na Taasisi ya TAWA ambayo inahusika na wanyama pori.

Aidha mheshimiwa Dendego ametoa maagizo kwa Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kufanya tathmini ya vikundi vya wavuvi na idadi ya wavuvi kwa ujumla, ili kuweza kuwasaidia kupata mkopo wa ununuzi wa boti ambazo watatumia katika shughuli za uvuvi, na kwamba  mwaka wa Fedha 2024/2025 Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa boti na kusaidia kuondokana na changamoto ya mvuvi mmoja mmoja inayosababisha kuliwa na mamba kila wakati.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Dendego ameweza kutembelea Shule ya Msingi Mtera na kujionea uandikishaji wa wanafunzi wa Awali na Darasa la Kwanza kwa mwaka 2024. Pia kuona uelewa wa wanafunzi kwa jinsi wanavyofundishwa darasani, na kwamba ameridhishwa na kazi zinazofanywa na Walimu hao.

Aidha, Mheshimiwa Dendego alifika hadi Shule ya Sekondari Nyerere, kujionea wanafunzi walioripoti wa Kidato cha Kwanza. Idadi ya wanafunzi walioripoti shuleni hapo ni 32 tu na kuona idadi ni ndogo ikilinganishwa na wanafunzi 386 waliopangwa kuanza Kidato cha Kwanza shuleni hapo hivyo hakuridhishwa na jambo hilo.

Mheshimiwa Dendego ametoa maagizo kwa Mtendaji wa Kata hiyo ya Migoli kwa kumuambia kuwa, kwa kushirikiana na viongozi wa Kata hiyo na akiwemo Diwani, kupita nyumba kwa nyumba katika kila Kijiji kukagua ni mzazi gani ambaye hajampeleka mtoto kwenda kuanza shule na kuripoti Kidato cha Kwanza.

Mheshimiwa Dendego ameendelea na ziara yake hadi Kata ya Kising’a na kukagua Zahanati iliyopo Kijiji cha Matembo. Zahanati hiyo ilijengwa kwa msaada wa Mdau Ndugu Asas Abri, kwa gharama ya Shilingi Milioni 180. Mheshimiwa Dendego na wananchi wa eneo hio wamemshukuru Mdau huyo kwa kuwasogezea huduma za afya karibu kwani walikuwa wanatembea umbali mrefu sana kufuata huduma hiyo. Zahanti hiyo imekamilika na imeanza kutoa huduma.  

 

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa