• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RC IRINGA MHE. DENDEGO AAGIZA WANAFUNZI WOTE KURIPOTI SHULENI HADI IFIKAPO JANUARI 30

Imewekwa : January 17th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe.Halima Dendego ametoa agizo kuwa wanafunzi wote wawe wameripoti shuleni ifikapo Januari 30, 2024. Ameyasema hayo akiwa katika ziara ya kikazi ya siku tatu tarafa ya Pawaga katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ambapo 17.01.2024 ametembelea shule ya Sekondari Mlenge, shule ya Msingi Mseke, kufanya mazungumzo na viongozi wa vijiji na baadaye kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji cha Itunundu kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

“Tumeona elimu ya msingi na sekondari shule zimejengwa zinang’aa kabisa lakini nimepita watoto hawapo shuleni kwa hiyo kazi ninayowapa ninyi wananchi pamoja na watendaji kila mmoja ahakikishe kwa siku chache hizi zilizobaki kuelekea tarehe 30 Januari kila mtu mtoto wake yupo shuleni, kama ni awali, msingi au sekondari awe darasani. Kwa hiyo kupitia kikao hiki naagiza hayo nasheria ziko wazi, asiyepeleka mtoto wake shule ni miezi sita jela na faini au kifungo bila faini”.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja amesema miundombinu yote inayohitajika ipo tayari kwa ajili ya kupokea wanafunzi na kwamba maeneo mengine ambayo bado yanachangamoto hasa kwa upande wa matundu ya vyoo yatafanyiwa kazi na hatua kadhaa zimeshaanzakuchukuliwa.

Kwa upande wa miundombinu ya maji Mhe. Dendego amesema amejionea hali ya maji kwamba yapo ya kutosha lakini sio masafi hivyo ameahidi kuwa ndani ya wiki mbili suala hilo litatafutiwa suluhu kwa kushirikiana na meneja wa RUWASA.

Aidha Mhe. Dendego amepata wasaa wa kusikiliza kero na changamoto za wananchi ambapo kwa sehemu kubwa ni migogoro ya ardhi na kuipatia suluhu. Pia amewaasa wananchi kutokuuza ardhi kwani tayari kulishawekwa zuio na anayetaka kuuza mashamba apate kibali cha serikali ili serikali ya kijiji ijiridhishe kuhusu eneo hilo. Na kwa maeneo ya serikali yaliyouzwa bila kufuata utaratibu, Mhe. Mkuu wa mkoa ametangaza kufuta mauziano hayo hadi hapo taratibu zote za mauziano zitakapofuatwa kama mauziano yatahitajika.

Ziara hii ya Mkuu wa mkoa wa Iringa katika tarafa ya Pawaga inaendelea kwa siku ya tatu ikiwa na lengo la kutatua kero na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamojana changamoto za ardhi.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa