• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SOS Childrens kwa kudhaminiwa na Kampuni ya HEMPEL Foundation Wafanya ziara Halmashauri ya WIlaya ya Iringa

Imewekwa : August 30th, 2022

Kampuni ya HEMPEL Foundation ambayo inadhamini Shirika la SOS Childrens imetembelea Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kuona shughuli zinazotekelezwa katika miradi inayoendelea kwenye Kata ambazo wanazihudumia.

Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ni miongoni mwa Halmashauri 5 za Mkoa wa Iringa yenye shule 158 zikiwemo shule 153 za Serklai na 5 za Binafsi. Shule hizi zina jumla ya wanafunzi wapatao 75,995 wakiwemo wavulana 38,259 na wasichana 37,736.

Toka mwaka 2016 Shirika la SOS Childrens limekuwa likishirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Iringa katika kutoa huduma za elimu na uboreshaji wa kipato cha jamii katika Kata tatu za Nyang’oro, Malengamakali na Ulanda ambapo Shule nane za Msingi zilikuwa zikihudumiwa ambazo ni; kwa Kata ya Nyang’oro – Shule za Msingi za Chamndindi, Mawindi, Ikengeza na Holo. Kwa Kata ya Malengamakali ni Shule za Msingi za Iguluba, Makadupa na Isaka. Kwa Kata ya Ulanda ni Shule ya Msingi ya Ulanda.

Aidha shughuli zilizofanyika kutoka mwaka 2016 hadi 2022 ni kama kujenga maktaba mbiliza jamii katika vijiji vya Makadupa ambapo ipo Kata ya Malengamakali na Chamndindi ambapo ipo Kata ya Nyang’oro, pia kufanya ukarabati wa vyumba vya madarasa 20 katika shule zilizohudumiwa. Kuwasaidia watoto waliokosa nafasi katika mfumo rasmi wa elimu au kuacha shule kutokana na sababu mbalimbali, kujenga miundombinu ya kunawia mikoni ili kuwasaidia wananfunzi kuepuka maambukizi ya virusi vya korona.

Aidha, kuwapa walimu semina za umahiri wa masomo ya Lugha na Sayansi, pia kujenga madarasa na matundu ya vyoo kwa kushirikiana na wanajamii, na kufanya kuongezeka kwa umahiri wa masomo ya Lugha na Sayansi.

Mratibu wa Miradi hiyo Bwana David Mlowe amesema, “tumepata mafanikio mengi kutokana na ushiriano na Shirika la SOS Children, kama kupatikana kwa huduma za maktaba kwa jamii ambapo inawasaidia wanafunzi na jamii kujiongezea maarifa. Pia kuboreshewa mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji na kufanya mazingira ya shule na elimu kuwa bora, kupanda kwa ufaulu kwa wanafunzi katika mitihani ya Kitaifa, na kuimarika kwa mahudhurio ya wanafunzi shuleni kutokana na kuboreka kwa mazingira ya kujifunzia”.

Mlowe ameongeza kusema kuwa, “Shirikia hili limekuwa likiwalipa pesa ya posho kwa walimu wa kujitolea ili kuwaongezea ari ya kuendelea kufundisha watoto. Pia kupatikana kwa mahitaji ya wanafunzi wanatoka katika mazingira magumu na kuwafanya waipende shule  na kutokata tamaa ya masomo”

Aidha mafanikio mengine ni ni kwa kupatika kwa vifaa vya TEHAMA kama vile kompyuta, prina nakadhalika. Pia kupungua upungufu wa madawati kutokana na utengezaji wa madawati mapya.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halamshauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja, ametoa shukurani za dhati kwa Shirika la SOS Childrens kwa msaada uliotolewa ambao kwa kiasi kikunwa umeboresha utoaji wa elimu katika Halmashauri.

Wakili Muhoja amesema, “tunaomba Shirika la SOS Childrens kuendelea kushirikiana nasi katika utoaji wa huduam za keilimu ili kuinua kiwango cha ubora wa elimu katika Halmashauri”

  

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa