• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TCRA Yawakumbusha Wanahabari Kufuata STK za Kazi Zao

Imewekwa : May 3rd, 2024

TCRA Yawakumbusha Wanahabari Kufuata STK za Kazi Zao

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ni Taasisi ya Serikali yenye kusimamia Sekta ya Mawasiliano nchini.

Mamlaka hiyo imekutana na Wanahabari wa Mkoa wa Iringa Mei 03, 2024 katika Ukumbi wa Maktaba ya Mkoa wa Iringa na kukumbushana masuala muhimu ya kuzingatia katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, kwani Mamlaka ina jukumu la kusimamia Sekta hii katika nyanja mbalimbali, na kuhakikisha kuwa Sekta ya Mawasiliano inafanya vizuri.

Akitoa maelezo ya namna Mamlaka hiyo inavyofanya kazi wakati akifungu kikao kilichowakutanisha Wanahabari hao Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini Mhandisi Boniphace Shoo amesema, “Wanahabari ni muhimu kufanya majukumu yenu kwa kufuata mambo matatu muhimu, ambayo ni Sheria, Taratibu na Kanuni (STK) ili kusiwepo na vikwazo kutoka Mamlaka hiyo na jamii kwa ujumla”.

Mhandisi Shoo ameendelea kusema, “kwa mfano Mtangazaji ni muhimu kutumia lugha ya staha, kumlinda mpokeaji huduma, kuelimisha jamii, kuburudisha, hii yote itafanya Sekta hii kushamili na kutokuwepo na malalamiko yoyote, na kwamba sisi kama Mamlaka tumepewa jukumu la kuhakikisha tunafuatilia hatua kwa hatua ili kuhakikisha hakuna ukiukwaji wa maadili”.

Akitoa mada ya Pili inayohusu Leseni Mhandisi Sunday Richard kutoka Makao Makuu ya Mamlaka amesema, “Mtoa huduma lazima azingatie anafanya kazi yake kwa kufuata leseni yake aliyoomba, kama mtu ameomba leseni ya kusambaza vifaa vya mawasiliano basi asichanganye na kazi nyingine. Kama mtoa huduma anahitaji kuongeza au kupanua huduma yake basi atalazimika kuomba kubadilishiwa leseni yake inayoendana na huduma anayotaka kutoa.”

Mhandisi Sunday amesema pia, kuna aina nyingi za leseni kulingana na huduma mtu anayotaka kutoa, kwani kuna Leseni Kubwa, Leseni Ndogo, Leseni za Makundi ya mitandao. Pia amesema namna ya kuomba leseni katika mifumo ya Mamlaka na viambatishi vinavyotakiwa kuwepo wakati mtoa huduma anaomba leseni.

Naye Mhandisi Balongo Mwesiga Kutoka Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ameongelea Kitengo cha Ufuatiliaji na Utekelezaji na kusema namna kitengo hicho kinavyofanya kazi, ikiwa ni pamoja na kusimamia michakato ya utekelezaji na uzingatiaji wa shughuli za Sekta 3 ambazo ni Mawasiliano/Intaneti, Utangazaji na Posta. Pia kuandaa, kupitia na kutekeleza Kanuni, Sheria na miongozo, na ufuatiliaji wa utekelezaji wa majukumu kwa ujumla.

Mada ya Nne ambayo ilitolea na Mhandisi Kisaka kutoka Makao Makuu ya Mamlaka, inayohusu Kanuni za Radio na Runinga ambayo ilitolewa mwaka 2008 na kufanyiwa maboresho 2022, amesema mtangazaji anapaswa kuzingatia haki za watoto, kutotoa maoni binafsi, kutoweka tangazo la biashara katika kipindi maalumu kama Bunge na mengine mengi.

Naye Mhandisi Bathlomeo Titus amesisitiza kupata leseni za maudhui ya kimtandao (Digital), na kufuata kanuni za kutuma maudhui mtandaoni (Parental Guarding – PG).

Baadhi ya Wanahabari walipata nafasi ya kutoa maoni mbalimbali na kuuliza maswali ambapo Wahandisi hao wa Mamlaka ya Mawasiliano waliweza kujibu na kuchukua maoni ili wakayafanyie kazi.

Mhandisi Shoo aliweza kuwashukuru Wanahabari hao na kuendelea kuwasisitiza kufuata STK ili kuepuka kufanya mambo kinyume na maadili.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa