• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

"TUSHIRIKIANE WAZAZI WOTE KATIKA MALEZI ILI KULETA UFANISI" - ROBERT MASUNYA

Imewekwa : May 21st, 2024

“Tushirikiane Wazazi Wote Katika Malezi Ili Kuleta Ufanisi” – Robert Masunya

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Iringa Ndugu. Robert Masunya, amewaomba Wadau, Walezi na Wazazi kushirikiana katika malezi na makuzi ya watoto.

Ndugu Masunya amesema hayo leo Mei 21 alipokuwa anaongoza kikao cha Ulinzi na Usalama wa Mtoto na Mwanamke kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri wa Siasa ni Kilimo.

Ameongeza kusema kuwa, "ni vizuri wazazi kuwa karibu na watoto ili kuweza kufuatilia nyendo na kubaini tabia zao. Hata watoto wakiona wazazi wapo karibu ni rahisi wao kueleza changamoto wanazopitia”.

Pia wazazi ni vizuri kutoa elimu juu ya malezi kwa watoto wanaozaa kwenye umri mdogo ili wapate kujua haki na sheria zao.

Aidha, Ndugu Masunya amesema jamii ikubali mabadiliko katika kila jambo, kwani mawazo ya maana yanatoka katika jamii yenyewe na hatimaye inaweza kubadilisha Sera, na kwamba Serikali itaendelea kushirikiana na Wadau na Mashirika mengine yasiyo ya Kiserikali katika masuala mbalimbali. Serikali ipo wazi muda wote kwa kupokea ushauri.

Pamoja na hayo, Katibu wa Kikao hicho Bi. Gladness Amulike aliweza kutumia kikao hicho kutambulisha Program Jumuishi ya Kitaifa (PJT) – MMMAM, ambayo ina mpango wa kutambua mtoto mwenye umri wa miaka 0-8 pamoja na mama.

Program hii inaanzia ngazi ya Kata hadi Taifa, ambapo inaangalia afya ya mtoto, malezi chanya, ujifunzaji, uchangamshaji, ulinzi na usalama wa mtoto ili mtoto aweze kukua vizuri. Katika hili Wadau mbalimbali wanahusika juu ya jambo hili.

Katika kikao hicho taarifa mbalimbali za Kisekta ziliweza kutolewa ambazo zimefanyika kwa kipindi cha Robo ya Tatu Januari – Machi.

Idara/Sekta zilizowasilisha taarifa zake za utekelezaji ni pamoja na Maendeleo ya Jamii, Elimu ya Awali na Msingi, Elimu Sekondari, TAHEA, Wawakilishi wa Vikundi vya Wanawake, SOS, Jeshi la Magereza, na World Vision.

Kadhalika Bi. Gladness aliweza kuwakumbusha wajumbe juu ya Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika, ambayo hufanyika Juni 16, ya kila mwaka, na kwamba kufanya maandalizi mapema.

 

 

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa