• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

UGONJWA WA TRAKOMA KUTOKOMEZWA IRINGA

Imewekwa : March 3rd, 2023

UGONJWA WA TRAKOMA (VIKOPE) KUTOKOMEZWA IRINGA

Serikali kwa kushirikiana na  shirika la  Helen Keller International inaendelea na jitihada mbalimbali za kuhakikisha ugonjwa wa Trakoma (vikope) unatokomezwa mkoani humo.

Akizungumza wakati wa zoezi la usawazishaji wa macho kwa  wagonjwa katika kijiji cha Izazi Halmashauri ya Wilaya ya Iringa mapema leo 3 Machi 2023, Mratibu wa macho wa Mkoa Bi Jasmin Kachemela amesema zoezi hili linafanywa kwa hatua ambapo hatua ya kwanza ni ya mafunzo kwa wahudumu ngazi ya jamii (CHW), upimaji, matibabu kwa wagonjwa waliobainishwa na baadaye ufuatiliaji wa kina kwa wagonjwa waliopata matibabu kuhusu hali zao na kujiridhisha na uponaji wao.

Hivyo ametoa wito kwa watu wote wenye changamoto za macho zilizobainishwa  na wahudumu kujitokeza ili kupata matibabu, “ vikope husababisha upofu na ni upofu wa kudumu kwa mtu kama hatapata matibabu kwa wakati” amesema.

Kwa upande wake Mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaombele wa Mkoa wa Iringa ndugu John Asukile Mwakabungu amesema lengo kuu la zoezi hili ni kuwa ugonjwa wa vikope (Trakoma) unatokomezwa kabisa hasa kwenye mkoa wa Iringa.

“tatizo sio kubwa sana kiasi cha kufanya tuanze kugawa dawa kwa kila mtu lakini lengo letu kuu ni kuhakikisha kuwa kupitia zoezi hili tunatokomeza kabisa ugonjwa huu, pia tunamshukuru mdau Helen Keller International kwa kujitokeza” amesema.

Vilevile wananchi waliofika kupata huduma ya usawazishaji wa macho (matibabu kwa njia ya upasuaji mdogo) kwenye zahanati ya Izazi wameishukuru serikali na mdau “Helen Keller International” kwa kuwafikishia huduma kijijini na kuongeza kuwa wao wasingeweza kuzifuata huduma hizi kwenye hospitali kubwa ikizingatiwa kuwa wengi ni wazee sana na hawana uwezo wa mumudu gharama za matibabu kwenye hospitali hizo.

Afisa mradi kutoka Helen Keller International Odiria Costantine amefafanua kuwa  zoezi la kutoa mafunzo na  utambuzi wa wagonjwa limefanyika kwa kata 13 za Halmashauri ya wilaya ya Iringa hadi sasa. Na matibabu kwa waliobainika na tatizo la vikope yanaendelea kutolewa ambapo hadi sasa tayari kata tisa (9) za Halmashauri ya Wilaya ya Iringa zimefikiwa na matibabu kutolewa. Idadi ya wagonjwa waliotibiwa hadi sasa ni 105 na zoezi linatarajiwa kufanyika kwa kata zote 28 za Halmashauri ya wilaya ya Iringa.

Pia Odiria Costantine, Afisa  mradi ameshukuru kwa ushirikiano mkubwa uliotolewa na viongozi wa Mkoa pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Iringa na kwamba hadi sasa zoezi la upimaji na utoaji wa matibabu kwa wagonjwa wa vikope linaendelea vizuri.

Kwa mjibu wa wataalamu wa afya inaelezwa kuwa Ugonjwa wa Trakoma (vikope) huambukizwa na bakteria ambao kichocheo kikubwa ni uchafu wa kwenye macho. Ili kuepuka au kujikinga na ugonjwa huu, watu hasa watoto wanashauriwa kunawa uso mara kwa mara kwa maji safi na sabuni.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa