• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Walimu wa Kidato cha Tano na Sita Kuweka Mikakati ya Kupandisha Ufaulu

Imewekwa : March 9th, 2023

Kikao Kazi cha Wakuu wa Shule na Walimu wa Kidato cha Tano na Sita

“Kwa kuweka nidhamu kati yenu Walimu na Wananfunzi, mnaweza kufuta daraja la nne na sifuri katika katika mitihani ya mwisho ya wanafunzi. Kwani nidhamu ni kitu cha kwanza kwa Mwalimu”.

Kauli hii imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja alipokuwa katika kikao kazi cha Wakuu wa Shule na Walimu wa Kidato cha Tano na Sita kilichofanyika leo tarehe 09/03/2023 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Siasa ni Kilimo.

Walimu hao wamekutana katika kikao kazi hicho ili kupeana mikakati ya kupandisha ufaulu kwa Kidato cha Sita, japo ufaulu upo vizuri. Hata hivyo pamoja na ufaulu huo, kuna baadhi ya Walimu wameshuka kiwango cha kufundisha kutokana na sababu mbalimbali.

“Napenda kuwahakikishia kuwa, madeni na stahiki mbalimbali mnazodai zitalipwa ikiwemo madeni ya likizo, uhamisho na malimbikizo  mbalimbali”.

Akifafanua tatizo la ucheleweshaji wa madeni hayo Wakili Muhoja amesema kuwa, “Mtumishi anapokuwa na madai fulani ni lazima aombe kuandika barua akiainisha anachodai kwa wakati, na kwamba mtumishi anapochelewa kuomba stahiki zake ndipo ulipaji wa deni hili unapochelewa”.

Wakili Muhoja ameongeza kusema kuwa, japo mazingira wanayofanyia kazi Walimu ni magumu, amewaomba wasikate tamaa, pia wingi wa wanafunzi katika darasa moja ni moja kati ya jambo linalofifisha ufundishaji.

Aidha Wakili Muhoja amesisitiza suala zima la ushoga mashuleni kwa wanafunzi, jambo ambalo ni kilio kikubwa kwa Taifa. Ameomba Walimu kufuatilia na kuchunguza wanafunzi kama kuna viashiria vya vitendo hivyo ambavyo siyo maadili kwa tamaduni za Kiafrika.

Pia Wakili Muhoja amewaasa Walimu kutojihusisha na mahusinao ya kimapenzi na wanafunzi wa kike, kwani kufanya hivyo ni kinyume na kosa baada yake wajiheshimu na kuwaheshimu wanafunzi kwani ni wanafunzi hao ni kama watato wao.

Walimu nao wamepata nafasi ya kuzungumza kero na changamoto zao zikiwemo, uchache wa Walimu ikilinganishwa na idadi wa wanafunzi, miundombinu na motisha hata pale wanapofanya vizuri, kutolipwa madai yao kwa wakati na kutopandishwa madaraja.

Pamoja na changamoto hizo, Walimu hao wameahidi kujitoa kufundisha kwa moyo ikiwemo kufundisha muda wa ziada na siku za mwishoni mwa Juma ili kufikia malengo waliyojiwekea.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari Ndugu Sylivester Mwenekitete amewashukuru Walimu hao kwa kuitika wito na kueleza lengo la kikao hicho ni kuwekeana mikakati ya kupunguza au kuondoa Daraja Sifuri na Daraja la Nne.

Akizitaja shule zilizofanya vizuri kwa Mwaka wa Masomo wa 2022/2023 ni pamoja na Shule ya Sekondari Nyerere, Shule ya Sekondari Isimani, Shule ya Sekondari Kiwere, Shule ya Ufundi Ifunda, Shule ya Sekondari ya Wasichana Ifunda, Shule ya Sekondari Isimila, Shule ya Sekondari Tosamaganga, Shule ya Sekondari Idodi, Shule ya Sekondari Mtera na Shule ya Sekondari Pawaga.

Mwenekitete ameongeza kusema kuwa, “malengo yenu yatafikia vizuri ikiwa kutakuwa na ushirikiano ndani shule, baina ya shule na shule na ndani ya Halmashauri. Kwa kufanya hivi italeta mafanikio ya kiwango cha juu sana”.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Bi. Beatrice Augustine alipokuwa anajibu hoja ya madai na stahiki mbalimbali za Watumishi amesema kwamba” kutokana na zoezi la kuhakiki vyeti, zoezi la upandishaji madaraja lilisitishwa lakini sasa hivi watumishi wanapandishwa vyeo na madaraja kama ilivyokuwa awali. Pia madai ambayo watumishi walikuwa wanadai wameanza kulipwa tangu mwaka wa fedha 2021/2022 hadi sasa yanaendelea kulipwa, na kwamba zaidi ya robo Tatu watumishi wamepanda madaraja.

Bi. Beatrice ameendelea kusema kuwa” hata watumishi ambao hawakupanda zaidi ya miaka kumi iliyopita, sasa hivi wameomba kibali kwa Katibu Mkuu ili waweze kupandishwa kwa utaratibu utakaolekezwa”.

 

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa