• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wanawake Waaswa Kutokaa Kimya Wanapofanyiwa Ukatili

Imewekwa : March 7th, 2023

WANAWAKE WAASWA KUTOKAA KIMYA WANAPOFANYIWA UKATILI ILI KUONDOA MAKOVU MIOYONI

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Veronica Kessy amewaasa wanawake kutokaa kimya pale wanapofanyiwa ukatili ili kuondoa makovu kwenye mioyo yao yanayotokana na kuumizwa.

Mh. Kessy ameyasema hayo alipokuwa akitoa Hotuba yake katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, ambapo kwa Halmashauri ya Wilaya Iringa iliadhimishwa siku ya Tarehe 06/03/2023 kwenye Kata ya Migoli.

Aidha Mh. Kessy amesema kuwa Siku hii iliadhimishwa Kimataifa kwasababu wanawake walifanyishwa  kazi ngumu, kunyimwa muda wa kunyonyesha na kulipwa ujira mdogo, Hivyo wakaanzisha siku hii 1975 ili kupinga mambo hayo na kupewa haki zao.

Kupitia Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu, Mh. Kessy amesema, Serikali kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wa Maendeleo wamekuwa wakishirikiana vema katika kuchochea maendeleo.

“Serikali yetu ikiongozwa na Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa mstari wa mbele kwa kushirikiana na Mashirika yasiyo ya Kiserikali kuchukua juhudi za makusudi za kuwaelimisha wananchi wote kuhusu masuala ya Ubunifu na Technolojia, kwa lengo la kuleta maendeleo endelevu miongoni mwa wananchi. Juhudi nyingi za kuhakikisha wanawake wanakuwa wabunifu katika Nyanja za teknolojia ni pamoja na kuwapa nafasi ya kujiendeleza katika Nyanja za kielemu na kuwawezesha kiuchumi”

Aliendelea kusema kuwa, kwa kuwa mwanamke ni mlezi hivyo hapaswi kumwacha mtoto asiende shule. Njia pekee ya ukombozi ni Elimu. Pamoja na jitihada za Kiserikali za kuboresha miundombinu ya Elimu, lakini hadi sasa watoto 2149 hawajaripoti, 78% ndio wameripoti

Pia Mh. Kessy amewasisitiza wazazi na walezi kuhusu suala la malezi ya watoto ili kuwa na kizazi bora. Amesema tuangalie kwa makini katuni za watoto kwani kuna baadhi ya hizo katuni zinahamasisha ushoga.

Sanjari na hayo Mh Mkuu wa Wilaya amewashukuru wadau mbalimbali wa maendeleo na kutambua michango yao kwenye jamii. Miongoni mwa wadau hao ni World Vision Tanzania, Lyra in Africa, SOS Childrens, Philips, WWF & Care Alliance, na LTA.

Mh. Kessy amepokea na kukabidhi misaada mbalimbali iliyolenga kwenda kwa watoto na watu wenye uhitaji wa Kata ya Migoli kutoka kwa Waheshimiwa Madiwani, Shirika la World Vision Tanzania, Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, kikundi cha Ngoma Migoli na Viongozi wa Wanawake Chama cha Mapinduzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mh. Stephen Mhapa ametoa pongezi kwa Diwani  wa Kata ya Migoli Mh. Benitho Kayugwa, Diwani wa viti Maalumu Mh. Yuster Kinyaga, Mbunge wa jimbo la Isimani Mh. William Lukuvi na Watumishi wa Halmashauri wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji (W) kwa uhodari na uchapa kazi wao.

Pia Mh. Mhapa amewashukuru na kuwapongeza wadau wa maendeleo wanaoshirikiana na Serikali kufanya shughuli za maendeleo na kumwagiza Mkurugenzi Mtendaji (W) kuandaa taarifa ya Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali na Wadau wa maendeleo yanayofanya kazi kwenye maeneo ya Halmashauri na kumpatia Mh. Mkuu wa Wilaya ili aweze kuwatambua.

Aidha Diwani wa Migoli Mh. Benitho Kayugwa ametoa shukrani kwa shughuli nzima ya maadhimisho ya siku ya wanawake iliyofanyika Migoli Kiwilaya na kushukuru kwa misaada iliyotolewa na makundi mbalimbali kwenda kituo cha watoto yatima na watu wenye uhitaji, na kutumia fursa hiyo kuishukuru Serikali kupitia Shirika la Akiba ya Chakula la Taifa (NFRA) kwa kutoa chakula kwa bei nafuu kwa wananchi wa Kata ya Migoli.

Mtaalamu wa Saikolojia na Afya ya Akili Ndugu Baraka Mshobozi ametoa elimu ya saikolojia ili kukabiliana na madhara yatokanayo na ukatili wa kijinsia. Pia mtaalamu kutoka Dawati la jinsia la Jeshi la Polisi alitoa elimu juu ya ukatili wa kijisia na hatua mbalimbali zinazopaswa kuchukuliwa ili kuzuia ukatili.

Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani mwaka 2023 yamebebwa na Kauli Mbiu isemayo,”Ubunifu na Mabadiliko ya Teknolojia, Chachu Katika Kuleta ustawi wa Kijinsia”

@tamisemi

@samiasuluhuhassan

@angelakairuki

@msemajimkuuwaserikali

@halimadendego

@veronicakessy

@iringars




Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa