• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Watendaji Wahimizwa Kuwatembelea Wajawazito na Wazazi Wanaonyonyesha

Imewekwa : February 16th, 2024

Watendaji Wahimizwa Kuwatembelea Wajawazito na Wazazi Wanaonyonyesha   

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Veronica Kessy, amewataka Watendaji wa Kata kwa kushirikiana na Watoa Huduma za Afya kuwatembelea akina Mama Wajawazito na Wazazi wanaonyonyesha kuwapa elimu ya umuhimu wa lishe bora ili kuepukana na udumavu.

“Kuna baadhi ya Kata hazijatembelewa na Watoa huduma za afya, kuongea na wazazi wanaonyonyesha na wajawazito kuwapa elimu ya umuhimu wa lishe bora yenye milo mitatu kwa siku. Hii inasababisha kuleta asilimia chini ya 100 kwa kutotekeleza. Hivyo nawasisitiza kufanya hivyo ili kipindi cha Robo ya Tatu kuwepo na utekelezaji wa 100% kwa kila Kata. Kufanya hivyo kutaleta matokeo chanya kwenye suala zima la udumavu”.

Mheshimiwa Kessy ameyasema hayo alipokuwa anatoa hotuba katika kikao cha Tathimini ya Mkataba wa Lishe kwa Robo ya Pili (Oktoba – Desemba) kwa mwaka wa Fedha 2023/2024.

Mheshimiwa Kessy ameendelea kusisitiza kuwa, Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo ya Surua imeanza, na kuwataka Watendaji kuwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kupeleka watoto kupata chanjo hiyo. Watoto wanaotakiwa kupata chanjo ni wenye umri wa miezi 0 – 9.

Aidha Mheshimiwa Kessy amewataka Watendaji hao kusimamia usafi wa mazingira ya maeneo yao, kutatua kero mbalimbali za wananchi, kwani mwaka huu ni uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kusiwepo sababu za wagombea kukosa kura.

Isitoshe Mheshimiwa Kessy amewataka Watendaji kutojihusisha na masuala ya kisiasa, na kuwataka kusimamia haki kwa kila jambo linalojitokeza.

Akiwasilisha taarifa ya Muongozo wa Chakula na Ulaji Tanzania Bara Afisa Lishe wa Halmashauri Bi. Tiliza Mbulla amesema, Muongozo huo ulitolewa mwaka 2023 na kusambazwa Januari 2024.

Lengo la Muongozo huo ni kuboresha hali ya Lishe na Afya za watu wa rika na makundi yote katika jamii ya Watanzania.

Bi. Tiliza amesema, Mwongozo wa Kwanza ni kula vyakula mchanganyiko kutoka makundi sita ya chakula kila siku. Mwongozo wa Pili ni kujitahidi kufikia lishe inayopendekezwa na akina mama wajawazito na wanaonyonyesha watoto wachanga ili kuhakikisha afya bora ya mama na ukuaji wa mtoto. Muongozo wa Tatu ni kupunguza ulaji wa vyakula vilivyokaangwa na mafuta mengi. Mwongozo wa Nne ni kuhakikisha ussafi wa mazingira mahali unapoishi. Muongozo wa Tano ni kuwa na mtindo bora wa maisha ili kupata afya bora n uzito unaoshauriwa na Muongozo wa Sita ni kuepuka tabia hatarishi kama vile matumizi ya sigara na unywaji wa pombe ili kupunguza hatari ya kupata magonjwa.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa