• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Waziri Jafo Aagiza Waliovamia Vyanzo vya Maji Kuondoka Mara Moja

Imewekwa : November 15th, 2022

Waziri Jafo Aagiza Waliovamia Vyanzo vya Maji Kuondoka Mara Moja

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo ametoa maagizo kwa wananchi wote waliovamia vyannzo vya maji kuondoka haraka iwezekanavyo na pia ameiagiza Mamlaka za Mabonde kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wanaochepusha maji kinyume cha sheria.

Waziri Jafo ameziagiza Mamlaka za Mabonde kote nchini kuhakikisha wanasimamia sheria ya maji kwa kuangalia pia wale wote waliopata vibali vya kutumia maji hayo kuhakiki kama maji hayo yanatumika kwa kuzingatia sheria na utaratibu lengo kubwa likiwa ni kuendelea kutunza maji katika maeneo yetu.

Ameyasema hayo leo tarehe 15 Novemba, alipokua katika ziara ya kutembelea na kukagua madhara ya kimazingira yaliyotokana na changamoto za ukame katika Mto Ruaha unaopatikana katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha na kisha kufanya mkutano kujadili changamoto hizo na kuona ni kwa namna gani changamoto hizo zinaweza kutatuliwa.

"...Hali hii imesababisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa maelekezo kwa Ofisi ya Waziri Mkuu kufanya kazi ya kufanya tathmini kwa kina hali inayoendelea na nini kifanyike ile tuiokoe nchi yetu, na ndio maana leo tupo hapa ". Amesema.

Aidha ameipongeza Serikali ya Mkoa wa Iringa na Mbeya kwa kuendesha kampeni ya kuondoa mifugo katike sehemu ya chanzo cha maji Ihefu ambayo iko mkoani Mbeya na pia ameishukuru TANAPA kwa kuendelea kuitunza hifadhi.

Waziri Jafo amesema shughuli za kibinadamu ndio chanzo kikuu cha kukauka kwa Mto Ruaha mkuu wakiwemo wakulima ambao wamekuwa wakichepusha maji bila kujali utaratibu wa maji, na ukataji wa miti uliokithiri, na kupelekea ukame ulioonekana kwa dhahiri.

Amesema timu ya wataalamu itapeleka mapendekezo kwa Viongozi wa juu kuhusu nini kifanyike kadhalika amesema kamati hiyo ya viongozi waliohudhuria wamekubaliana kuwa wale wote waliovamia vyanzo vya maji kuondoka mara moja kuanzia leo hii, pia shughuli zote zinazoendelea lazima zizingatie sheria zote zikiwemo zile za mazingira.

Mkutano huo umewakutanisha Mawaziri mbalimbali wakiongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Seleman Jafo, Waziri wa Utalii na Maliasili Mhe. Dkt. Pindi Chana, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo na Makazi Mhe. Dkt. Angelina Mabula, Waziri wa Maji Mhe. Juma Aweso, Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Anthony Mavunde, Katibu Mkuu Wizara ya TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe na Wakuu wa Mikoa nane wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Halima Dendego, Wakuu wa Mikoa wengine ni pamoja na Mbeya, Dodoma, Njombe, Kigoma, Tabora, Morogoro, Pwani, Katavi, Rukwa, Songwe.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI - MBOMIPA March 18, 2023
  • RATIBA YA VIKAO VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA KWA ROBI YA PILI KWA MWAKA FEDHA 2022/2023. January 16, 2023
  • ZIARA YA MKUU WA MKOA WA IRINGA December 14, 2022
  • Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA YA IRINGA AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUBORESHA SEKTA YA ELIMU

    March 24, 2023
  • WATENDAJI KATA WILAYANI IRINGA WAAGIZWA KUSIMAMIA UTOLEWAJI WA CHAKULA SHULENI

    March 20, 2023
  • ZAIDI YA MADAWATI 162 YATOLEWA KWA SHULE YA SEKONDARI KIDAMALI NA SHAFA AGRO COMPANY LIMITED

    March 18, 2023
  • Maandalizi ya Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2023

    March 14, 2023
  • Tazama zote

Video

FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA POLIO, DALILI NA NJIA ZA KUJIKINGA
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Gangilonga

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0767778106

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa