• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Ziara ya Mh. Rais Samia Suluhu Hassan Mkoani Iringa

Imewekwa : August 13th, 2022

Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan alifanya ziara ya siku tatu Mkoani Iringa, na kutembelea maeneo mbalimbali ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.

Wakati wa hotuba yake aliyotoa katika Uwanja wa Samora uliopo Manispaa ya Iringa alisisitiza mambo mbalimbali ikiwemo; kutambua maeneo ya malisho na kuyapima ili kupunguza migogoro ya ardhi. Kuwapatia Maafisa Ugani vitendea kazi kama pikipiki, ili kuwasaidia kuwafikia wakulima kwa urahisi.

Aidha Mh. Rais amesema, ni muhimu kuimarisha kilimo cha umwagiliaji mfano ujenzi wa skimu ili wakulima wapate kulima misimu miwili mfululizo.

Pia kwa upande wa ufugaji amesema, wananchi wananchi wafuge kwa kuzingatia kanuni za ugaji bora ili kujipatia kipato.

Kwenye suala la Utalii Mh. Rais amesema, ujenzi wa barabara kutoka Iringa kwenda Mbuga ya Ruaha itajengwa kwa kiwango cha lami ili kurahisisha wa watalii kuja kwa wingi.

Mh. Rais ameongeza kuwa, Awamu ya Pili ya Royal Tour itajikita katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini na Iringa ikiwemo.

Kwa upande wa Afya Mh. Raisi amesisitiza kuendelea kuboresha Hospitali ya Rufaa na ujenzi wa Zahanati na Vituo vya Afya katika maeneo mbalimbali, bila kusahau ununuzi wa vifaa tiba.

Mh. Rais ameipongeza Mkoa wa Iringa kwa ufaulu wa Kidato cha Nne cha Kidato cha Sita. Pia amewata wanafunzi waendelee kuweka jitihada katika masomo kwa nafasi za mafunzo zipo wazi na mikopo ya elimu ya juu itatolewa kwa wakati ili kutokwamisha jitihada za wanafunzi.

Vilevile upande wa Misitu, Maliasili na Mazingira Mh. Rais ametaka Wilaya zote kuendelea kutunza misitu na kuitunza na kuzingatia upandaji miti. Pia kuanzisha kwa viwanda hasa maeneo yanayolimwa mazao ya misitu. Pia ametoa pongezi kwa Mkoa wa Iringa kwa utunzaji wa mazingira.

Aidha Mh. Rais amesema Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya maji katika maeneo ya Ismani na Migoli, pia kutunza vyanzo mbalimbali vya maji kama Bwawa la Mtera. 

Mh. Rais amesema, suala la ajira kwa vijana litaendelea kutatuliwa taratibu na kwa kusisitiza Sekta binafsi kuendelea kutoa ajira kwa vijana. Pia Serikali itaendelea kuwapa nguvu Machinga kwa kuwajengea masoko yenye miundombinu rafiki.

 Pamoja na mengine yote Mh. Rais amesisitiza wananchi wajitokeze kuhesabiwa katika zoezi la Sensa ya watu na makazi litakaloanza tarehe 23/08/2022, kwani ni muhimu kwa maendeleo yetu.

Pia Mh. Rais ameendelea kusisitiza wananchi wote kuendelea kujikinga dhidi ya UVIKO 19.

Mwisho ametoa shukurani kwa Wanahabari kwa kuwa naye toka siku ya kwanza ya ziara hadi alipoondoka Mkoani Iringa, pia na Watumishi na wananchi wote kwa kujitokeza kumpokea na kusikiliza hotuba yake.

 

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa