• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Agriculture


OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA 

HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA 

 

FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA MISITU

Imetolewa na:

 

Mkurugenzi Mtendaji (W)

S. L. P 108,

IRINGA 

2022

              

        UTANGULIZI

Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ina eneo lenye ukubwa wa kilometa za mraba 20,576, kati ya hizo, eneo lenye ukubwa wa kilometa za mraba 10,718.5 sawa na asilimia 52 ya eneo lote la Halmashauri limetengwa kama eneo la Hifadhi ya Taifa ya wanyamapori ya Ruaha, Pori la Akiba la Lunda Mkwambi na mabwawa na eneo lenye kilometa za mraba 9857.5 ndilo lililobaki kwa matumizi anuwai ya binadamu ikiwemo hifadhi za misitu na wanyamapori (WMA) sawa na asilimia 48 ya eneo lote la Halmashauri. Wilaya ipo kati ya nyuzi za Latitudo 7 00o and 8 30o Kusini na Longitudo 34o na 37o Mashariki. Kwa ujumla, Wilaya ipo katika mwinuko kati ya meta 900 na 2000 juu ya usawa wa bahari. Aidha, Wilaya inapokea mvua kati ya mm 500 na 1000 na jotoridi kati ya 10 na 30 oC. Wilaya ya Iringa ni moja ya Wilaya zinazounda Mkoa wa Iringa. Halmashauri ina Tarafa 6, Kata 28 na Vijiji 134.

Eneo la Halmashauri limejaliwa kuwa na raslimali nyingi za misitu ya kupandwa na misitu ya asili. Misitu ya kupandwa iliyopo ni ile inayopandwa na taasisi au watu binafsi katika maeneo wanayomiliki. Kwa sasa, maeneo yenye mashamba ya miti ya kupandwa yanakadiriwa kufikia hekta 30,000 (Tarafa ya Kiponzelo Hekta 20,000, Tarafa ya Mlolo Hekta 8000 na Tarafa ya Kalenga Hekta 2000). Miti inayostawi ni mikaratusi (Eucalyptus) na misindano (Pines). Misitu ya asili iliyopo ni ile ya Miyombo ikiwa imechanganyika na aina nyingine za miti kama vile Acacia, Terminalia na Combretum.  Maeneo yaliyohifadhiwa na yasiyohifadhiwa yanakadiriwa kufikia hekta 250,000 za misitu ya asili.

Halmashauri ya Wilaya ya Iringa pia ipo katika eneo la kimkakati la Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania (SAGCOT) na ipo katika kitovu cha eneo la Ihemi Cluster. Eneo hili lina sifa ya kuwa na mvua za kutosha na hali ya hewa inayostawi mazao mengi ikiwepo misitu.

  • MAENEO YA UWEKEZAJI 

Fursa zilizopo za uwekezaji katika sekta ya misitu ni pamoja na:-

  • Uwekezaji katika uanzishaji wa mashamba ya miti. Maeneo yanayofaa kuanzisha mashamba ya miti yanapatikana katika Tarafa za Kiponzelo, Mlolo na Kalenga, ambayo kwa pamoja yana ukubwa wa hekta 403,810 ambazo zinafaa kwa matumizi mbalimbali ikiwemo uanzishaji wa mashamba ya miti. Kwa sasa matumizi ya eneo hili ni asilimia 7.5 tu ya eneo linalofaa kwa upandaji miti kibiashara. Hivyo eneo hili lina fursa kubwa ya uwekezaji;
  • Uwekezaji katika uanzishaji wa viwanda vya kuchakata mazao ya misitu. Kwa sasa kuna viwanda vya kuranda mbao 8 na mtambo wa kuchemsha nguzo 1 (Agora Poles). Uwekezaji katika kuanzisha viwanda una fursa kubwa. Maeneo yanayofaa ni pamoja na kata za Ifunda, Lumuli na Mgama. Maeneo haya yapo karibu na barabara kuu ya TANZAM na yapo karibu na vyanzo vya raslimali zinazolisha viwanda hivyo katika Wilaya za Mufindi na Kilolo;
  • Uwekezaji katika biashara ya hewa ukaa. Halmashauri ina maeneo ya misitu ya asili yanayokadiria kufikia hekta 250,000. Baadhi ya maeneo haya yametengwa kuwa maeneo ya misitu ya hifadhi ya vijiji (Hekta 197,000) na maeneo ambayo hayajatengwa yanafikia hekta 53,000. Hivyo yote kwa pamoja yanaweza kutumika katika biashara hiyo; na
  • Uwekezaji katika mazao ya misitu yatokanayo na miti ya asili (non-timber forest products -NTFPs). Eneo hili lina na fursa kubwa ya uwekezaji kwa kuwa lina mazao mengi yatokanayo na misitu ya asili. Mazao hayo ni pamoja na matunda, dawa, mboga, uyoga na asali. Mazao haya yanapatikana kwa wingi katika maeneo ya misitu ya asili yaliyopo Wilayani.
  • MAFANIKIO YA SEKTA YA MISITU

Sekta ya misitu katika Wilaya imepiga hatua kubwa katika kuletea maendeleo wananchi na kuingizia Serekali mapato. Yafuatayo ni mafanikio yaliyopo katika sekta hii:-

  • Kutenga misitu ya vijiji ambayo inasimamiwa kisheria yenye ukubwa wa hekta zinazofikia 197,000 katika vijiji 38;
  • Kuhamasisha upandaji miti. Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, jumla ya miti iliyopandwa na kupona inakadiriwa kufikia milioni 7. Miti hii imepandwa katika maeneo ya watu binafsi na taasisi yenye ukubwa wa hekta Zaidi ya 4600;
  • Sekta hii imeendelea kutumika kama chanzo kikuu cha nishati ya joto katika familia zetu. Zaidi ya asilimia 92 ya wananchi Tanzania wanatumia kuni au mkaa kama nishati kupikia;
  • Sekta ya misitu imekua chanzo cha mapato kwa wananchi walio wengi kupitia biashara ya mazao ya misitu; na
  • Sekta ya misitu ni chanzo cha mapato katika Serekali yetu, ambapo takwimu za miaka 4 iliyopita zinaonesha kuwa Halmashauri ya Wilaya imeingiza zaidi ya shilingi Milioni 796.
  • UMUHIMU WA UWEKEZAJI KWENYE UKUAJI WA SEKTA YA MISITU

Uwekezaji katika sekta ya misitu utawezesha ukuaji wa sekta ya misitu katika maeneo yafuatayo:-

  • Ongezeko la wawekezaji wenye mitaji mikubwa, hivyo kuchangia ukuaji wa uchumi wa wananchi na pato la Taifa.
  • Uwekezaji utachochea ongezeko la viwanda vya kuchakata mazao ya misitu, hivyo kuongeza mnyororo wa thamani (value chain) ya mazao yatokanayo na misitu.
  • Uwekezaji utachochea kasi ya upandaji miti kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya miti katika soko.
  • HUDUMA ZINAZOTOLEWA NA SERIKALI KWA WADAU WA MISITU

Sekta ya misitu inategemea sana mazingira rafiki ya ufanyaji biashara kwa kuwa inahitaji mitaji mikubwa na wakati mwingine inahitaji muda mrefu ili mwekezaji kupata manufaa yatokanayo na uwekezaji wake. Kwa mantiki hiyo, mchango wa serikali unahitajika kwa kiwango kikubwa ili kujenga uwezo wa kujiamini wa wawekezaji. Huduma zinazotolewa na Serikali kwa wadau wa misitu ni pamoja na:-

  • Kutoa elimu kuhusu sera, sheria, kanuni na miongozo ya serikali katika sekta ya misitu;
  • Kutoa nyaraka za kisheria kwa wafanyabiashara wa mazao ya misitu;
  • Kutoa elimu ya ugani kuhusu misitu kama vile uanzishaji wa vitalu vya miche ya miti, kusimamia mashamba ya miti na matumizi endelevu ya raslimali za misitu ya asili;
  • Kutenga maeneo ya uwekezaji wa viwanda ikiwemo viwanda vya uchakataji wa mazao ya misitu. Tayari maeneo matatu yameshatengwa katika Wilaya ya Iringa. Maeneo hayo yapo Nduli (ekari 27), Igingilanyi (ekari 25) na Tungamalenga (ekari 50).

#KARIBU WILAYA YA IRINGA

#MISITU INALIPA

#WEKEZA SASA





  • KANDA ZA KILIMO:
  • 2.1. UKANDA WA CHINI:
  • Ukanda huu una mwinuko wa meta 900 – 1,200 kutoka usawa wa bahari, hupata mvua chache kiasi cha mm 500 – 600 kwa mwaka na kiwngo cha joto ni kati ya 20 °c – 30 °c.
  • Ukanda huu unajumuisha maeneo ya Tarafa za Pawaga, Idodi na Isimani.  Mazao yanayoliwa ni pamoja na mahindi, mpunga, vitunguu, nyanya, ndizi, karanga, pamba, mtama, mhogo, maembe, machungwa, korosho, mapapai, ufuta na viazi vitamu.
  • 2.2. UKANDA WA KATI:
  • Ukanda huu una mwinuko wa meta 1,200 – 1,600 kutoka usawa wa bahari, hupata mvua za wastani na juu ya wastani mm 600 – 1,000 kwa mwaka na kiwango  cha joto ni kati ya  15 °c – 20 °c.
  • Ukanda huu unajumuisha maeneo ya Tarafa za Mlolo, Kalenga, Kiponzelo na Kata za Kising’a na Kihorogota katika Tarafa ya Isimani.  Mazao yanayolimwa ni tumbaku, alizeti, kabeji, ngano, soya, mahindi, pamba nyanya, viazi vitamu, viazi mviringo, maharage, ufuta, mboga na matunda.  Mazao mengine yanayoweza kustawi ni kahawa, pareto na njegere.

 

 

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa