• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Idara ya Ujenzi

IDARA YA UJENZI IRINGA

UTANGULIZI

Idara ya ujenzi katika halmashauri ya wilaya ya Iringa ina mtandao wa barabara wenye jumla ya Km  1323.93. Kati ya hizo barabara kuna Km 7 ni barabara za lami sawa na 0.5%, Km 986.33 sawa na  74.5% ni za changarawe  na  jumla ya Km 330.60 sawa na 25%  ni za udongo.  Barabara za changarawe na lami hupitika vizuri karibu kwa 90% katika vipindi vyote vya mwaka lakini barabara za udongo hupitika kwa shida katika wakati wa mvua.

Pia idara inahusika moja kwa moja katika ujenzi na ukarabati wa majengo  mbalimbali ya  idara mbalimbali kaika halmashauri kwa kuhakikisha majengo hayo hayahatarishi maisha ya watumiaji.

MAJUKUMU YA IDARA

Majukumu makuu ya idara ya ujenzi ni kuhakikisha barabara zote zinapitika mwaka mzima kwa kufanya matengenezo ya barabara hizo kulingana na bajeti. Katika hilo idara inajukumu kuu la kuhakikisha kuwa wakandarasi wanaoshinda zabuni za barabara na majengo wanatekeleza kazi husika kwa ubora na viwango kulingana na mikataba yao.

MUUNDO WA IDARA NA WATUMISHI

Ili kuweza kutekeleza majukumu ya kila siku ya Idara ya ujenzi, idara ina muundo halisi wa idara  unaoundwa na watumishi mbalimbali.  Muundo wa idara ya ujenzi  upo kama hivi, Kiongozi mkuu ni mkuu wa idara na chiniyake kuna vitengo vikuu viwili ambavyo ni Kitengo cha Barabara na Kitengo cha Majengo. Kila kitengo kina mkuu wa kitengo na kuwa na wahandisi pamoja na mafundi sanifu ili kuweza kutekeleza kazi katika vitengo hivyo. Idara ina jumla ya wahandisi  watatu akiwemo mkuu wa idara, mkadiriaji majengo (QS) mmoja, mafundi sanifu saba. Pia idara ina katibu muktasi mmoja na muhudumu mmoja. Timu hii ya wataalamu kwa pamoja ndio wanaowezasha idara kuweza kutimiza majukumu ya idara ya kila siku na kuleta jija katika mkoa na taifa kwa ujumla.


MIRADI ILIYOTEKELEZA

Mradi wa lami Km 34.967 katika barabara ya Kising’a – Ilambilole – Isimani tarafani

Ujenzi wa barabara hii katika kiwango cha lami unatoka na ufadhili wa Jumuiya ya Ulaya (EU) katika halmashauri yetu. Mradi huu upo katika utekelezaji kwa sasa na kuwa na  unagharimu  (є): 5,919,667.85 ambazo ni sawa karibu na  TZS: 14,799,169,625.00.

Barabara hii inajengwa na kuwekwa lami njia moja yaani (single lane) kutokana na idadi ya watumiaji wa barabara hii. Barabara hii ikikamilika itawawezesha wananchi kusafirisha mazao yao na bidhaaa zinginezo kwa urahisi zaidi katika kipindi chote cha mwaka tofauti na hapo awali ambapo ikifika wakati wa mfua barabara hii ilikuwa ikipitika kwa shida. Ujengwaji wa barabara hii itapunguza pia gharama za usafirishaji na pia kuviinua vijiji vilivyo kandokando ya barabara hii. Vilevile barabara hii itawafanya wananchi waweze kufikia huduma muhimu  kirahisi kwa jamii husika hasa za afya na elimu kwa watoto.

Ujenzi wa barabara ya Itunundu – Kisanga

Ujenzi wa barabara hii katika kiwango cha changalawe  unatoka  katika mfuko wa barabara wa Taifa. Mradi huu upo katika utekelezaji kwa sasa na kuwa na  unagharimu  TZS: 668,022,300.00 utakapokamilika. 

Barabara hii inajengwa kwa kiwango cha changalawe lakini ni barabara ambayo  imechokwa kwa kilomita 7 mfululizo na kuinua kuinuwa tuta lake. Barabara hii ikikamilika itawawezesha wananchi kusafirisha mazao yao na bidhaaa zinginezo kwa urahisi zaidi  kutoka kijiji cha Kisanga na kupeleka katika kijiji cha Itunundu na hatimaye mjini katika kipindi chote cha mwaka tofauti na hapo awali ambapo ikifika wakati wa mfua barabara hii ilikuwa ikipitika kwa shida na wananchi walikua wakizunguka na kupita njia ya Kinyika ambayo ni ndefu. Ujengwaji wa barabara hii itapunguza pia gharama za usafirishaji na pia kuwezesha barabara ya kuingia katika gereza la Itunundu kuwa nzuri na yenye kupitika mwaka mzimz. Vilevile barabara hii itawafanya wananchi waweze kufikia huduma muhimu  kirahisi kwa jamii husika hasa za afya katika hospitali ya pawaga  na elimu kwa watoto.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa