• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Land and Natural Resources


IDARA YA ARDHI MALIASILI

Idara ya Ardhi na  Maliasili ni mojawapo ya Idara za Halmashauri za Wilaya ya Iringa. Idara hii inaundwa na jumla ya vitengo vidogo saba (7) chini ya sekta za Ardhi na Maliasili ambavyo ni: (i) Mipango Miji (ii) Usimamizi wa Ardhi (iii) Upimaji na Ramani (iv) Uthamini wa mali (v) Misitu (vi) Wanyamapori (vii) UtaliiIdara ya Ardhi na Maliasili ina jumla ya Watumishi 22.

MAJUKUMU YA IDARA YA ARDHI NA MALIASILI

Kwa ujumla majukumu ya Idara ya Ardhi na Maliasili  ni ya kutoa huduma za kitaalam na ushauri kwa wakazi wa eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, wananchi wengine wa Tanzania na wawekezaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi ya Tanzania. Majukumu hayo ni kama ifuatavyo:

  • Kupanga, Kupima na kumilikisha maeneo ya matumizi mbalimbali ya Ardhi kama vile matumizi ya viwanja, taasisi mbalimbali, kilimo, malisho, makazi, wanyamapori nk.
  • Kutoa elimu ya sera na sheria mbalimbali kuhusu masuala ya Ardhi, makazi, wanyamapori, misitu na mazingira ili wananchi wazielewe na kuzizingatia wanapopanga na kutekeleza mipango yao ya maendeleo
  • Kudhibiti na kushauri uendelezaji wa maeneo mbalimbali ya Ardhi unaokwenda kinyume cha sheria na taratibu zinazohusika.
  • Kudhibiti uvunaji holela wa maliasili mbalimbali kama vile misitu na wanyamapori.
  • Kulinda na kuendeleza ustawi wa wanyamapori kwa kutoa leseni za kuwezesha uwindaji endelevu ili shughuli za uwindaji na upigaji picha wa kitalii ziwe endelevu.
  • Kukuza na kuainisha vivutio mbalimbali vya utalii ndani ya eneo la Halmashauri ya Wilaya na uwepo wa kituo cha taarifa mbalimbali za utalii ndani ya Halmashauri ya Wilaya.

WANYAMAPORI NA UTALII KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA

Katika Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ni maarufu kwa wanyamapori na vivutio mbalimbali vya utalii kama ifutavyo;

  • Inayo maeneo mbalimbali ya hifadhi za wanyamapori katika ukanda ambao uoto wa mimea ya Kaskazini mwa Afrika (Migunga) inakutana na uoto wa mimea ya Kusini (Miombo). Hifadhi hizo ni kama vile Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, Pori Tengefu la Lunda Mkwambi Kaskazini, Maeneo ya Hifadhi za Jamii (WMA’S) ya MBOMIPA na WAGA na eneo la wazi la Izazi ambayo yote yapo ndani ya Mipaka ya eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.
  • Uoto wa asili uliopo kwenye maeneo ya mbuga za wanyamapori unachangia uwepo wa aina mbalimbali za wanyamapori kama vile Tandala Wakubwa na Wadogo, Simba, Tembo, Nyati, Mbwa mwitu waliopo katika hatari ya kutoweka, Viboko, Nyani, Mbweha Maskio, pia ndege wa aina mbalimbali, Reptilia na Amphibia. Mto Ruaha unaopita ndani ya hifadhi ya mbuga ya Ruaha na Bwawa la Mtera ni muhimu sana kwa ustawi wa wanyamapori ambao ni kivutio kikubwa kwa watalii wa ndani na kutoka katika nchi mbalimbali.

 

VIVUTIO MBALIMBALI VYA UTALII KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA

Makumbusho ya Mtwa Mkwawa Tarafa ya Kalenga.

 Hili ni jengo la Makumbusho ya Mtwa Mkwawa lililopo katika kijiji cha Kalenga. Eneo hili  linalopatikana  umbali wa Km 15 kutoka Iringa mjini.  Eneo  .Kalenga ndiyo asili ya MAisha ya Kiutawala ya Mtwa Mkwawa. Katika jengo hili kichwa cha Mtwa mkwawa aliyetawala 1855-1898 kimehifadhiwa. Pia Mtalii utapata historia ya utawala wa Mtwa Mkwawa na Kabila la Wahehe.

 

Kielelezo Na 1.Makumbusho ya Kalenga katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.

Pango la Masalia ya Binadamu Magubike             

                              

Kielelezo Na 2  Eneo la Mapango ya Magubike eneo lenye masalia ya binadamu wa kale na zana za chuma

 

Magubike ni pango lililopo katika Kilima katika kijiji cha Mugabike Halmashauri ya Iringa .Kuna sehemu mbili ambazo zimetapakaa masalia ya muhula wa chuma ,zana za mawe zinazoonekana katika maeneo yenye mmonyoko wa ardhi zana za muhula wa kati zinaonekana wazi katika mteremko chini ya pango kwenye shamba la tumbaku.

Pango la Magubike  yamepatikana masalia ya muhula wa chuma,, kulikuwa na masalia ya zana za muhula wa chuma  na masalia ya zana za  Miuhula wa kati. na masalia ya mifupa ya wanyama mbalimbali, konokono ( Genus Achatina), na vipande 6.5 vya meno ya binadamu wa kale ( Homo sapiens) aliyeishi kipindi cha miaka 50,000 hadi 200,000 iliyopita Umri halisi wa masalia ya binadamu na masalia mengine utapatikana baada ya kukamilisha utafiti .Meno haya ni ya binadamu wa mwanzo aliyefanana kimaumbile kama binadamu wa sasa.  

Mapango ya Mlambalasi (Mlambalasi Rockshelter)

Mlambalasi  ipo umbali wa km 50 magharibi mwa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Njia iendayo Hifadhi ya Ruaha. Mlambalasi ni eneo alilozikwa Mtwa Mkwawa, Mtemi wa kabila la Wahehe katika karne ya 19. Pango hili lipo juu ya eneo la makaburi na lina sehemu kuu 2. Katika sehemu zote mbili kuna mtawanyiko mkubwa wa zana za muhula wa chuma na za kihistoria. Sehemu ya kwanza,yalipatikana masalia ya kihistoria ya muhula wa chuma, vyungu na zana za mawe za muhula wa mwisho zilichanganyikana na masalia ya chuma.

                                        

Kielelezo Na 3 Pango la Mlambalasi ambalo lilitumiwa na Mtwa MKwawa Kiongozi wa Kabila la Wahehe

Chemchemi ya Maji moto Kikongoma

Hili ni eneo lililopo km 16 kutoka  mji mdogo wa Kalenga katika kijiji cha Kalenga.  Eneo hili hutembelewa na watalii wengi kwa ajili ya kunawa maji ya moto. Maji haya huaminika kuwa ni maji ya Baraka, ambayo  mtu akiyatumia mikosi na matatizo mbalimbali katika maisha yanaisha. Waganga Mbalimbali wa tiba za asili hutumia maji haya kwa ajili ya tiba. Hiii ni chemchem ambayo maji yake hayaongezeki wala kukauka.

Kielelezo Na 2 Sehemu ya Majimoto  KIkongoma  katika kijiji cha Mangalali sehemu  ambayo hutembelewa na watalii Wengi 

 

Daraja la Mungu Kikongoma – Mangalali

Hili ni eneo ambalo ni mojawapo ya vivutio vya utalii katika Halmashauri kivutio cha utalii. Katika eneo hili Mto Raha Ndogo hupotea na mita  baada ya mita 53 kuibuka. Daraja linalofunika mto huu ni mawe yenye rangi mbalimbali za kuvutia ambayo yamepangwa kwa asili na kufanya sauti nzuri za maporomoko ya maji ya Mto ruaha ndogo. Eneo hili ndiko alikofia Mama yake na Mkwawa akipinga kutoa siri ya nguvu ya utawala utawala wa mwanae Mtwa Mkwawa.

Kielelezo Na 5 Daraja la Mungu Kikongoma katika kijiji cha Mangalali

 

Maeneo kwa ajili ya Utalii wa Kutembea

Halmashauri ya wilaya ya Iringa imejaliwaa kuwa na utajiri wa mazingira mazuri yenye mvuto na salama kwa ajili ya utalii wa kutembea kama vile kutembelea milima, Mawe na misitu mbalimbali ya asili. Hili ni eneo la Igangidungu Katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Hili ni jiwe kubwa lenye mvuto wa rangi mbalimbali ambalo huvutia wageni wengi kutembelea na kupiga picha

 

Kielelezo 6 Jiwe lililopo katika kijiji cha Igangidung’u kwa utalii wa kutembea

 

Utalii wa kuona Wanyama

Utalii wa wanyama  katika maeneo ya mapori ya Jumuia za wanyamapori zinazozunguka Hifadhi ya Taifa ya Ruaha. Utalii unaofanyika katika maeneo haya ni utalii wa kuona, kutembea na Utalii wa picha. Hifadhi ya RAha ipo umbali wa Km 146 kutoka Iringa Mjini .

Kielelezo7 Wamyama aina ya swala wanapatikana katika Hifadhi ya Ruaha na jumuiya za wanyamapori MBOMIPA- Iringa

IDARA YA ARDHI,NA  MIPANGO MIJI

Idara ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ni mojawapo ya Idara za Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Idara hii inaundwa na jumla ya vitengo vidogo nane (7) chini ya sekta za Ardhi na Maliasili ambavyo ni: (i) Mipango Miji (ii) Usimamizi wa Ardhi (iii) Upimaji na Ramani (iv) Uthamini wa mali (v) Misitu (vi) Wanyamapori (vii) Utalii

Idara ya Ardhi na Maliasili ina jumla ya Watumishi 27.

MAJUKUMU YA IDARA YA ARDHI NA MALIASILI

Kwa ujumla majukumu ya Idara ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ni ya kutoa huduma za kitaalam na ushauri kwa wakazi wa eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, wananchi wengine wa Tanzania na wawekezaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi ya Tanzania. Majukumu hayo ni kama ifuatavyo:

  • Kupanga, Kupima na kumilikisha maeneo ya matumizi mbalimbali ya Ardhi kama vile matumizi ya viwanja, taasisi mbalimbali, kilimo, malisho, makazi, wanyamapori nk.
  • Kutoa elimu ya juu ya sera na sheria mbalimbali kuhusu masuala ya Ardhi, makazi, wanyamapori, misitu na mazingira ili wananchi wazielewe na kuzizingatia wanapopanga na kutekeleza mipango yao ya maendeleo
  • Kudhibiti na kushauri uendelezaji wa maeneo mbalimbali ya Ardhi unaokwenda kinyume cha sheria na taratibu zinazohusika.

           Kudhibiti uvunaji holela wa maliasili mbalimbali kama vile misitu na wanyamapori.

  • Kulinda na kuendeleza ustawi wa wanyamapori kwa kutoa leseni za kuwezesha uwindaji endelevu ili shughuli za uwindaji na upigaji picha wa kitalii ziwe endelevu.
  • Kukuza na kuainisha vivutio mbalimbali vya utalii ndani ya eneo la Halmashauri ya Wilaya na uwepo wa kituo cha taarifa mbalimbali za utalii ndani ya Halmashauri ya Wilaya.

WANYAMAPORI NA UTALII KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA

Katika Ukanda ya Nyanda za Juu Kusini, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ni maarufu kwa wanyamapori na vivutio mbalimbali vya utalii kama ifutavyo;

  • Inayo maeneo mbalimbali ya hifadhi za wanyamapori katika ukanda ambao uoto wa mimea ya Kaskazini mwa Afrika (Migunga) inakutana na uoto wa mimea ya Kusini (Miombo). Hifadhi hizo ni kama vile Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, Pori Tengefu la Lunda Mkwambi Kaskazini, Maeneo ya Hifadhi za Jamii (WMA’S) ya MBOMIPA na WAGA na eneo la wazi la Izazi ambayo yote yapo ndani ya Mipaka ya eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.
  • Uoto wa asili uliopo kwenye maeneo ya mbuga za wanyamapori unachangia uwepo wa aina mbalimbali za wanyamapori kama vile Tandala Wakubwa na Wadogo, Simba, Tembo, Nyati, Mbwa mwitu waliopo katika hatari ya kutoweka, Viboko, Nyani, Mbweha Maskio, pia ndege wa aina mbalimbali, Reptilia na Amphibia. Mto Ruaha unaopita ndani ya hifadhi ya mbuga ya Ruaha na Bwawa la Mtera ni muhimu sana kwa ustawi wa wanyamapori ambao ni kivutio kikubwa kwa watalii wa ndani na kutoka katika nchi mbalimbali.

PICHA ZA WANYAMA NA NDEGE MBALIMBALI

Tembo (Elephant -Loxodonta africana) wa Iringa ni wakubwa na wanapatikana kwa wingi katika eneo moja kuliko eneo lingine lolote la Afrika Mashariki.

Mbwa mwitu (Wild dog), ni mnyamapori aliyehatarini kutoweka pia anapatikana katika maeneo yetu ya Hifadhi. Hatari hii ya kutoweka inatokana na ujangili na kupungua kwa maeneo ya hifadhi kwa kuwa wanaishi kwenye kundi kubwa, hivyo wanahitaji wanahitaji eneo kubwa la hifadhi. Pia wanauawa na simba, fisi na wafugaji)

Tandala wakubwa dume na jike Tandala mdogo jike na watoto

Korongo (Roan Antelope) Palahala/Mbalapi (Sable antelope)

Maeneo ya hifadhi ya Iringa ni maeneo pekee kwa kuwa na wingi wa Tandala wakubwa (Greater Kudu), Tandala wadogo (Lesser Kudu), Palahala/Mbalapi (sable Antelope) na Korongo (Roan antelope).

Simba dume wakinywa maji

Simba jike na watoto wake kama walivyoonekana kwenye eneo la MBOMIPA

 

 

          

Chui wanaopatikana katika Hifadhi ya Ruaha

 

 

          

Viboko wanapatikana katika bwawa la Mtera

 

 

              

Ramani ya Hifadhi za wanyama katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

 

VIVUTIO MBALIMBALI VYA UTALII KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA

 

Pamoja na wanyamapori, vipo vivutio mbalimbali vya utalii kama vile Nguzo za Asili (Natural Pillars) za Isimila, Daraja la Mungu na Maji ya Moto ya Kikongoma, Mapango ya Mlambalasi alikojificha Chifu Mkwawa wakati alipopambana na Wajerumani, Zana za Kale katika eneo la Isimila, Jengo la Makumbusho ya Mtwa Mkwawa Kalenga, Ngome ya Chifu Mkwawa katika eneo la Kalenga nk.

  

PICHA ZA VIVUTIO VYA UTALII

 

Daraja la Mungu la Kikongoma,

           

Eneo hili linalojulikana kama jiwe jeusi linapatikana kwenye kijiji cha Mangalali Kata ya Ulanda katika barabara kuu itokayo Iringa mjini kuelekea hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

 

Ni eneo ambalo mama yake Chifu Mkwawa aliyeitwa Sengimba alijiua baada ya kupata taarifa kuwa mwanawe Mkwawa amekamatwa na wajerumani.

 

Katika eneo hili mto Ruaha mdogo unazama ardhini umbali wa mita zaidi ya 100 na kutengeneza daraja la asili linalojulikana kama daraja la Mungu. Jirani na eneo hili kuna chemi chem ya maji moto na eneo la matambiko.

 

Eneo hili linafaa kwa utalii wa picha na ujenzi wa kambi za muda, changamoto iliyopo ni kutofikika kwa urahisi kutokana na ubovu wa barabara

               

Pillars za Ismila

 

Minara hii inapatikana nje kidogo ya kituo cha kihistoria cha Isimila.

 

Minara hii ni kivutio kizuri cha utalii.

 

Katika eneo hili zama za kati na za mwisho zinapatikana.

 

Eneo hili linahitaji kutangazwa zaidi kama kivutio cha utalii cha kihistoria

          

Fuvu la Mkwawa

 

Mkwawa alizaliwa mwaka 1855 na kufa mwaka 1898, Fuvu la mtwa Mkwawa lilipelekwa Ujerumani mwaka 1898 lilirudishwa na Wajerumani mwaka 17/06/1954 na kuwekwa kwenye Kituo cha Makumbusho Kalenga kilichopo kijiji cha Kalenga kata ya Ulanda umbali wa kilometa 10 toka Iringa Mjini.

 

Kituo hiki kinamilikiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii - Idara ya mambo kale.

 

Katika Kijiji hiki Halmashauri imeanzisha kikundi cha utalii wa kiutamaduni wa wahehe.

 

Ngoma za kimila kama mbayaya, mangala na kiduo pia zinapatikana.

  

 

   





Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa