• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Elimu Msingi

IDARA YA ELIMU YA MSINGI

0 UTANGULIZI:

Halmashauri ya Wilaya ya Iringa inasimamia utoaji wa elimu katika ngazi ya Elimu ya Awali, Msingi na Elimu ya Watu Wazima na Idara ina vitengo vinne. Aidha yapo madarasa ya awali 113 na shule za msingi 149, madarasa ya Elimu ya Watu Wazima….na vituo vya Ufundi Stadi 2

Katika usimamizi na utekelezaji wa Elimu ya Msingi yapo baadhi ya mafanikio, changamoto na athali za changamoto hizo ili kufikia malengo yaliyokusudiwa kama ifuatavyo:-

 MAJUKUMU YA IDARA:

Kusimamia uandikishaji katika

Kusimamia utoaji wa Elimu bora.

Kujenga uwezo wa utawala bora, usimamizi na ufuatiliaji katika Elimu.

Kusimamia na kuratibu masuala mtambuka.

Kufafanua na kusimamia utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo, Sheria na

Elimu ya awali.

Elimu ya Msingi.

Elimu Maalumu.

Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya mfumo Rasmi.

Ukimwi na VVU.

Elimu ya mazingira.

Usawa wa Kijinsia katika Elimu.

kanuni zinazoongoza utoaji wa Elimu na mafunzo ya Ufundi.

Kutayarisha na kusimamia utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya Elimu.

Kuhimiza udhibiti wa nidhamu ya walimu na wanafunzi.

Kusimamia maendeleo ya taaluma na michezo.

Kukusanya, kuratibu na kuchambua takwimu za Elimu kwa ajili ya Mipango ya Maendeleo katika ngazi ya shule, Halmashauri, Mkoa na Taifa.

Kusimamia wajibu na haki za walimu.

 MAFANIKIO YA ELIMU YA MSINGI

1.Elimu ya Msingi

Idadi ya Shule za Msingi imeongezeka kutoka shule 118 mwaka 2006 kufikia shule za msingi 146 mwaka 2014.

2 Ikama ya walimu na idadi ya wanafunzi

Idadi ya walimu imeongezeka kutoka walimu 1226 mwaka 2006 kufikia walimu 1358 mwaka 2014 sawa na ongezeko la uwiano wa 1:45. Mchanganuo wa idadi ya wanafunzi pamoja na mahitaji, waliopo na upungufu wa walimu ni kama ilivyooneshwa hapo chini.

 

 

Ikama ya walimu na idadi ya wanafunzi

IDADI YA WANAFUNZI
IKAMA YA WALIMU
 
WAV
WAS
JUMLA
MAHITAJI
WALIOPO
UPUNGUFU
UWIANO
AWALI
4050
4040
8090
404
127
277
1:64
MSINGI
29370
29544
58914
1473
1358
115
1:43

NB: Uwiano unaohitajika ni 1:40 (yaani mwalimu 1 kwa wanafunzi 40 kwa elimu ya msingi na 1:20 kwa elimu ya awali.)

3 Uandikishaji wa wanafunzi

Uandikishaji wa wanafunzi wenye umri wa kuanza darasa la kwanza umeongezeka kutoka 52.9% mwaka 2005/2006 hadi 99.1% mwaka 2013/2014 kama inavyooneshwa kwenye jedwali lifuatalo:

HALI HALISI YA UANDIKISHAJI KWA MUDA MIAKA 10 MFULULIZO

MWAKA
WALIOTEGEMEWA
KUANDIKISHWA
WALIOANDIKISHWA
ASILIMIA (%) YA UANDIKISHAJI
WAV
WAS
JUMLA
WAV
WAS
JUMLA
WAV
WAS
JML
2005
10,000
11,000
21000
5641
5469
11110
56,41
49.7
52.9
2006
4500
4886
9386
4419
4385
8804
98.2
89.7
93.7
2007
4500
4884
9364
4695
4699
9394
104.3
96.2
100.3
2008
5000
3692
8692
4195
4133
8328
82.6
103.5
95.8
2009
4500
4500
9000
4450
3990
8440
98.8
88.6
93.7
2010
4700
4750
9450
4818
4518
9336
102.5
94.94
96.7
2011
4956
4522
9478
4645
4695
9340
93.7
103.8
98.75
2012
4789
4661
9450
4748
4668
9416
99.1
100
99,5
2013
4022
4192
8214
3971
4172
8143
98.7
99.5
99.1
2014
4689
4881
9570
4856
4618
9474
99.2
99.5
99.8

NB: Tofauti katika idadi ya wanafunzi waliotegemewa kuandikishwa na walioandikishwa inatokana na sababu ya kuhama na kuhamia kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

4 Elimu Maalum

Wilaya ya Iringa ni kati ya Wilaya chache zenye shule maalum. Shule ya Msingi Kipera iliyopo kata ya Nzihi ilianzishwa mwaka 1976 kama shule ya kawaida. Mwaka 2013/2014 shule hii ilianzisha kitengo cha Elimu maalum ikiwa na wanafunzi wenye ulemavu wa aina mbili uziwi na wasioona ambapo hadi sasa idara imepokea wanafunzi 10 wasiosikia na 12 wasioona.

Miundombinu ya shule ya watoto wenye ulemavu (Kipera) imeboreshwa kwa kiasi kikubwa hadi kufikia 80% mwaka 2013/2014)

5 Miundombinu ya shule

Idadi ya vyumba vya madarasa imeongezeka kutoka vyumba 986 mwaka 2005/2006 kufikia vyumba 1238 mwaka 2013/2014 ongezeko hili ni sawa na asilimia 20.

Matundu ya vyoo yameongezeka kutoka matundu 1326 mwaka 2005/2006 hadi 1824 mwaka 2013/20014 ongozeko hili ni sawa na asilimia 28. Nyumba za walimu zimeongezeka kutoka nyumba 398 mwaka 2005/2006 kufikia nyumba 611 mwaka 2013/2014 na madawati kwa mwaka 2013/2014 ni 18490 upungufu 10967

0 MATOKEO YA MITIHANI YA TAIFA YA DARASA LA

 IV NA VII

1 Matokeo ya Mtihani wa darasa la iv (2011-2013)

Tathmini ya mtihani wa Taifa wa darasa la IV kwa miaka 3 mfululizo kuanzia mwaka 2011` hadi 2013.

MWAKA
 
WALIOFANYA
KIWANGO CHA UFAULU
 
%
IDADI YA WANAFUNZI WALIOFAULU
DARAJA ‘A’
DARAJA ‘B’
DARAJA ‘C’
JUMLA (A+B+C)
WV
WS
JML
WV
WS
JML
WV
WS
JML
WV
WS
JML
WV
WS
JML
2011
3769
3908
7697
03
01
04
189
212
401
1154
1346
2500
1346
1559
2905
37.7
2012
3488
3769
7257
0
0
0
54
56
110
633
636
1269
691
688
1379
19
2013
3339
3833
7172
06
09
15
93
113
206
591
688
1279
690
810
1500
20.9

 

2 MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA VII (2004 2013)

 

Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ilikuwa na jumla ya wanafunzi 6,403 waliofanya mtihani wa Taifa mwaka 2013. Wanafunzi waliochaguliwa kuendelea na Kidato cha kwanza ni wale waliopata alama 100 - 250 ambao jumla yao ni 3,982 (Wavulana 1916 na Wasichana 2,066) sawa na 62.2%. Wanafunzi ambao hawakupata nafasi kuendelea na masomo ni 2,421 (Wavulana 1,148 na Wasichana 1,273) sawa na 38.6% jumla ya shule 138  kati ya 146  zilizokuwa na watahiniwa.

Idadi ya wanafunzi wa darasa la VII waliofanya, waliofaulu, waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza na kiwango cha ufaulu kuanzia mwaka 2002 hadi 2013

HALI HALISI YA UFAULU KWA MIAKA 10 MFULULIZO



WALIOSAJILIWA
WALIOFANYA
WALIOFAULU
ASILIMIA
N/O
MWAKA
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
%
1
2004
4061
4061
8122
3958
4335
8293
1708
1469
3177
38.31
2
2005
3818
4172
7990
3358
4129
7487
2130
1819
3949
52.74
3
2006
3016
3136
6152
2965
3114
6079
2179
2072
4251
69.93
4
2007
3443
3626
7029
3265
3478
6743
2435
2255
4690
69.55
5
2008
4273
4411
8684
4231
4372
8603
2346
2350
4696
54.5
6
2009
4388
4367
8775
3931
4065
7996
1823
1580
3403
42.56
7
2010
3042
3038
6080
2984
3005
5989
1730
1449
3179
53.09
8
2011
4541
4752
9293
4370
4820
9190
2922
2354
5276
57.4
9
2012
3403
3643
7046
3350
3628
6978
2466
2760
5226
74.69
10
2013
3111
3377
6488
3064
3339
6403
1916
2066
3982
62.19

 

3 Changamoto zinazoathiri maendeleo ya taaluma

 

Ufaulu wa mtihani kwa watahiniwa wanaomaliza elimu ya msingi una kabiliana na changamoto mbalimbali kama zifuatazo:

Upungufu mkubwa wa walimu

Upungufu mkubwa wa nyumba za walimu

Kukosekana kwa chakula cha asubuhi/mchana kwa baadhi ya shule

Ukosefu wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia

Ukosefu wa madarasa na walimu wa awali katika baadhi ya shule za msingi

 

0 MIKAKATI YA KUINUA UBORA WA ELIMU - 2014

 

Kuongeza idadi ya udahili wa walimu wa fani mbalimbali

Wanafunzi kuwa na chakula cha mchana shuleni

Kusogeza huduma za elimu pale inapostahili

Walimu kuimarisha usimamizi, Kuimarisha mazingira

Kuimarisha upatikanaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia

Kuwa na uwiano wa 1:1 wa vitabu kwa wanafunzi

Kuwa na walimu mahiri wa KKK katika kila shule

Kuwa na elimu ya kutosha juu ya matumizi ya OMR.

Kupunguza kero za walimu kuangalia haki na wajibu wa walimu

Kuwa na mafunzo kabilishi juu ya mitaala.

Kwa kutumia walimu mahili katika mafunzo yatolewe kwa walimu wengine

Kuwawezesha walimu kwa kuwa na ukaguzi wa ndani

Kuwawezesha wakaguzi kukagua shule nyingi kwa mwaka

Kuhamasisha jamii kuwa shule ni mali yao

Kuwa na mashamba darasa shuleni ili kupata chakula.

Kuhamasisha watu wenye uwezo wa kuchangia chakula shuleni.

Kuelimisha jamii kuwa shule ni mali yao.

Kuelimisha jamii pia kuwa wao pia ni moja ya jamii ya pale waliopo.

Kuwajengea uwezo wa masomo walimu wakuu na walimu

Kuboresha utaratibu wa kushughulikia masuala ya walimu.

 KITENGO CHA ELIMU YA WATU WAZIMA

 

Idadi ya vituo/madarasa ya MEMKWA ni 19

(i) idadi ya wanafuzi wote wa MEMKWA 2014

KUANDIKA
WAVULANA
WASICHANA
JUMLA
KUNDIRIKA LA I
99
108
209
KUNDIRIKA LA II
62
57
119
JUMLA KUU
161
137
326

(ii) taarifa ya matokeo ya mtihani kwa wanafunzi wa MEMKWA waliofanya mtihani mwaka 2013

Wanafunzi wa MEMKWA kundirika la I waliofanya mtihani wa darasa IV mwaka 2012

WAV
WAS
JUML
87
72
152

Waliofaulu na kuingia darasa la V (mfumo rasmi)

WAV
WAS
JUML
74
50
124

Wanafunzi wa MEMKWA kundirika la II, waliofanya mtihani wa darasa VII – 2012

WAV
WAS
JUML
32
38
70

Wanafunzi wa MEMKWA kundirika la II waliofaulu na kujiunga kidato cha kwanza 2014

WAV
WAS
JUML
15
25
40



B: MUKEJA

Idadi ya vituo/madarasa ya MUKEJA yaliyopo katika Halmashauri ya Iringa ni 66 yaliyohai mpaka sasa hivi ni 35

Idadi ya wanakisomo waliopo katika madarasa

Walio katika madarasa ya K.K.K

ME 304

KE 693

JUMLA 997

Shughuli za ugani (SU)

ME 162

KE 329

JUMLA 491

JUMLA ya wanakisomo kwa madarasa yote ni

ME 833

KE 1655

JUMLA 2488

C: Idadi ya madarasa/mduara kwa kila aina ya programu

Darasa KCM
KCK

K.K. K
SU
UMALI
UMALI
SU
UST
Elimu masafa
JUMLA
8
6
8
27
15
2
-
66

K.K.K – Kusoma, kuandika na kuhesabu

SU – Shughuli za ugani (kilimo, ufugani n.k)

UMALI Shughuli za uzalishaji mali (mfano: ujaliamali, vikoba n.k)

UST – Ufundi stadi (uselemala, ushonaji n.k)

E: IDADI YA VITUO VYA MTAALA MPYA NA FANI ZAKE

Tanangozi (sayansikimu)

Kibena (sayansikimu)

Tungamalenga (kilimo)

Kilichohai na kinatoa huduma ni kituo cha Tanangozi

F: IDADI YA VYUO VYA UFUNDI STADI VYA SERIKALI NI VIWILI

Tanangozi

Kalenga

Idadi ya vituo vya ufundi stadi usinyo vya serikali ni 14 (binafsi na mashirika ya dini)

Fani zinazofundishwa vituo vya serikali (Tanangozi)

Sayansikimu

Wanaume
Wanawake
Jumla
-
7
7

Useremala

Wanaume
Wanawake
Jumla
10
-
10

Uashi

Wanaume
Wanawake
Jumla
7
-
7

Jumla ni 24

Idadi ya wanafunzi wanaosomo elimu masafa(Distance learining) ni 4 wapo katika kituo cha Ifunda shule ya msingi

MAFANIKIO

Wanafunzi wa ufundi stadi waliofaulu kuanzia 2012 hadi 2013 ni 33

Wanafunzi wa MEMKWA waliofaulu kuanzia 2010 hadi 2012 wavulana ni 67 na wasichana 60 jumla ni 127

Wananchi kupitia madarasa ya Elimu ya Watu Wazima wanakisomo 133 wameweza kujua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Idara ya Elimu imeweza kusambaza viti 20,200 katika kipindi cha 2013 katika shule za Msingi

Wananchi mbalimbali wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu na wale wanaohitaji kujiendeleza wamehamasishwa kujiunga na mfumo wa elimu masafa (odl) kupitia sekondari 12 walihitimu elimu ya sekondari kupitia kituo cha sekondari Mseke.

CHANGAMOTO NA UTATUZI

Baadhi ya walimu kutokuwa na ari ya kufundisha

Idara ya elimu wilaya, waratibu, walimu wakuu tunafanya vikao vya kielimu na kubaini changamoto na namna ya kuzitatua kwa wakati

Malipo ya honoralia kutokutoka kwa wakati

Idara inalipa honoralia kulingana na upatikanaji wa fedha

Mtaala wa ufundi stadi bado haujaboreshwa ili uweze kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia

Kutoa ushauri kwa mamlaka zinazohusika ili utatuzi wa tatizo hilo uzingatiwe

Vituo vya ufundi havina na vyombo vya kutosha

Kutafuta wahisani watakaoweza kusaidia ununuzi wa vyombo hivyo

KITENGO CHAUTAMADUNI NA MICHEZO

KAZI ZA KITENGO / MAJUKUMU

Kukuza na kuendeleza Utamaduni wa Mtanzania

Kusimamia sera zinazohusiana na shughuli za Utamaduni kama Sera ya Utamaduni, Sera ya Michezo, Sera ya Vijana n.k.

Kukuza, kusimamia na kuhimiza matumizi ya Lugha ya Kiswahili na kusimamia maendeleo yake.

Kukuza na kuendeleza Mila na Desturi nzuri kwa jamii

Kuhimiza nidhamu na uwajibikaji kwa jamii

Kusimamia maendeleo ya shughuli za sanaa na wasanii.

Kusimamia maendeleo ya michezo yote

Kusimamia maendeleo ya shughuli za vijana

Kuhimiza moyo wa uzalendo wa Taifa letu.

Kuratibu na kusimamia vyama vya michezo katika wilaya

Kuratibu shughuli za Mwenge wa Uhuru.

VIKUNDI VYA SANAA:

 Halmashauri ya wilaya ya Iringa ina jumla ya vikundi vya Sanaa 80 kati ya hivyo vikundi 40, vimesajiliwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).

Vikundi hivyo vinajishughulisha na fani za Ngoma, Ngoma za Asili, Maigizo, Kwaya, Muziki wa kizazi kipya, Muziki wa Asili, Ngonjera, Mashairi, Utambaji wa hadithi

na Majigambo.

VYA MICHEZO:

 Katika Halmashauri ya wilaya ya Iringa tuna jumla ya Vilabu vya Mpira wa miguu 60 kati ya hivyo jumla ya Vilabu 16 vimesajiliwa. Pia kuna chama cha mpira wa miguu kimoja.

VIKUNDI VYA VIJANA:

 Halmashauri ina jumla ya vikundi vya vijana 180 ambavyo vinajishughulisha na shughuli mbalimbali za maendeleo kama vile, kilimo, ufugaji, ufugaji nyuki, ufyatuaji wa tofali, utengenezaji wa vigae na biashara ndogondogo. Jumla ya vijana 1360 wanafanya shughuli hizo.

CHANGAMOTO:

Vikundi vingi vya sanaa, sanaa zao hazipo kibiashara kwa kukosa stadi za ujuzi

Ukosefu wa fedha wa kuendesha mafunzo ya sanaa kwa wasanii

Uongozi wa Vilabu kutokuwa makini

Uhaba wa walimu wa michezo mbalimbali

Ukosefu wa mitaji kwa vijana

Ukosefu wa elimu ya Ujasiliamali kwa vijana.

MIKAKATI YA UTEKELEZAJI:

Kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tutaandaa Semina za Ujasiliamali kwa vijana

Mafunzo ya Stadi za ujuzi zitatolewa.

Mafunzo kwa walimu wa michezo yameanza kutolewa na yataendelea kutolewa.

Halmashauri inatenga fedha kwa ajili ya kuwakopesha vijana pia kwa kushirikiana na Asasi zisizo za Kiserikali zinaendelea kutoa mikopo.

MAONI NA USHAURI

Mambo yafuatayo hayanabudi kufanyika ili kuwezesha hali ya ufaulu wa wanafunzi kuwa mzuri kwa kuzingatia nafasi za wadau wote ambao ni:

Wanafunzi, walimu, wazazi / walezi/jamii na serikali kila kundi litimize wajibu wake katika kutekeleza majukumu ya elimu ili kufanya elimu kuwa bora zaidi

 HITIMISHO:

Ufaulu katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka 2013 umepanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa na kufikia malengo ya BRN. Ufaulu huu umepelekea Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kushika nafasi ya 3 kimkoa. Idara ya Elimu msingi imeweka lengo la kuongeza ufaulu kufikia asilimia 100 kwa mwaka 2014 kwa kujiwekea mikakati madhubuti ya usimamizi na uendeshaji wa elimu kwa shule za msingi.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa