• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Maji

  IDARA YA MAJI

Eng. LUCAS MADAHA 

MKUU WA IDARA YA MAJI

MAELEZO YA IDARA:

Idara ya Maji ni moja kati ya Idara zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Idara ya Maji ina jumla ya wataalam 14 wahandisi 3 na mafundi sanifu 11, Pia Idara ina watumishi wengine karani 1, Mtunza Ofisi 1, Walinzi 2, Wahudumu 2, na madereva 2, Idara ina gari moja na pikipiki 3 ambazo hutumika kufanikisha ufanyaji kazi wa kila siku.

 

SHUGHURI ZA IDARA

Shughuri kuu zinazofanywa na Idara ya Maji ni kutoa huduma ya ushauri wa kitaalamu juu ya matumizi ya maji, Kuunda na kusimamia Jumuiya za watumiaji maji.

  • Kusanifu na kujenga miradi mbalimbali ya Maji
  • Uandaaji wa mipango, Bajeti na ripoti mbalimbali kwa kila wiki, Mwezi, Robo na mwaka
  • Usimamizi na kufanya tathimini ya miradi ya maji inayoendelea kutekelezwa

MIRADI YA MAJI ILIYOTEKELEZWA NA INAYOTEKELEZWANA IDARA

Miradi ya Maji ya vijiji 10 yenye thamani ya bilioni 7 iliyopo chini ya Programu ya Maji na Usafi wa Mazingira- RWSSP.

  • Mradi wa maji wa mtiriko na msukumo kijiji cha Igangidung’u wenye jumla ya vichotea Maji 15 na mitego ya Maji miwili na matenki mawili umekamilika na unatoa huduma kwa watu 1,399
  • Mradi wa Maji wa kijiji cha Kikombwe wenye jumla ya vichotea Maji 15 na Mtego wa Maji mmoja na tenki moja umekamilika na unatoa huduma kwa watu 1,938
  • Mradi wa Maji wa mtiriko na msukumo kijiji cha Weru wenye jumla ya vichotea Maji 10 na mitego ya Maji miwili na matenki mawili umekamilika na unatoa huduma kwa watu 1,478
  • Mradi wa Maji wa wa mtiriko na msukumo kijiji cha mfyome wenye jumla ya vichotea Maji 11 na visima virefu viwili umekamilika na unatoa huduma kwa watu 2,600
  • Mradi wa Maji wa kijiji cha Izazi-Mnadani wenye jumla ya vichotea Maji 15 na visima virefu viwili unaendelea kutekelezwa kwa sasa umefikia 55%
  • Mradi wa Maji wa kijiji cha Migoli-Mtera wenye jumla ya vichotea Maji 22 na visima virefu viwili unaendelea kutekelezwa kwa sasa umefikia 65%
  • Mradi wa Maji wa kijiji cha Malinzanga wenye jumla ya vichotea Maji 26 na mtego mmoja unaendelea kutekelezwa kwa sasa umefikia 70%
  • Mradi wa Maji wa vijiji vya Isupilo, Itengulinyi na Lumuli wenye jumla ya vichotea Maji 30 na mtego mmoja unaendelea kutekelezwa kwa sasa umefikia 45%
  • 2. Miradi ya Maji iliyopo chini ya ufadhili wa UNICEF
  • Idara ya Maji imekuwa ikitekeleza Miradi ya Maji ya uchimbaji visima virefu na uwekaji wa mfumo wa umeme juwa na pampu katika shule za Msingi za Ibumila, Katenge, Kidilo, Magunga, Kinyika, Kisanga, Maperamengi, Mtera, Kihanga, Kinyali,Mbwelelina Kibebe imekamilika na inatoa huduma.
  • 3. Miradi ya Maji chini ya ufadhili wa AQUAL WELL DRILLING
  • Idara ya Maji imekuwa ikitekeleza miradi ya Maji ya upimaji visima katika vijiji 51, Uchimbaji visima katika vijiji 39 na ufungaji pampu wa mfumo wa umeme katika vijiji 12.
  • 4. Mradi wa Maji chini ya ufadhili wa REA (Rural Energy Agency)
  • Idara ya MAji inatekeleza Miradi ya Maji katika vijiji 19 na mfumo wa umeme jua na pampu
  • 5. Mradi wa Maji chini ya ufadhili wa SECO (Sustainable Energy Conservation Organization)
  • SECO ni shilika lisilo la kiserikali limeweza kutekeleza mardi wa Maji wa uchimbaji visima viwili na kujenga vinara vya tenkina kwa sasa wako kwenye harakati za kulaza mabomba na kufunga mfumo wa umeme juana pampu.
  • 6. Mradi wa Maji chini ya ufadhili wa kanisa la Anglikani kupitia taasisi ya Emmanuel International.
  • Idara ya Maji imetekeleza mradi wa Maji ya mtiririko katika kijiji cha Kiwere na kwa sasa Mradi umekamilika unajumla ya vichotea  maji 10 na unatoa huduma.
  • 7. Mradi wa Maji chini ya ufadhili wa BOB & HELEN
  • Idara ya Maji imeweza kutekeleza Mradi wa Maji chini ya ufadhili wa BOB & HELEN katika kijiji cha Malagosi na vichotea maji 12 kwa sasa umekamilika na unatoa huduma.
  • 8. Miradi ya Maji inayoendelea kutekelezwa na wadau wengine ni Mradi wa Maji katika kijiji cha Lupembelwasenga unaofadhiliwa na BOB & HELEN na kanisa la Anglikani kupitia shirika la Emmanuel International, Mradi Maji katika kijiji cha Mgama, Ifunda, Magubike unaofadhiliwa na WARIDI.

AINA ZA MIRADI NA HALI YA UPATIKANAJI WA MAJI KATIKA HALMASHAURI YA IRINGA

 

Na

AINA YA MRADI

IDADI 

1
 Miradi ya maji ya mtiririko na mfumo wa bomba

16

2
Miradi ya maji ya visima inayosukumwa na mashine za diseli

3

3
Miradi ya maji mito inayosukumwa na mashine za diseli

2

4
Miradi inayosukumwa na umumu wa TANESCO

2

5
Miradi ya maji ya visima virefu inayosukumwa na umeme wa nguvu za jua

41

6
Miradi ya maji ya chemche inayosukumwa na umeme wa nguvu za jua

1

7
Miradi ya maji ya visima virefu inayosukumwa na pampu za mkono

100

8
Miradi ya maji ya visima vvifupi inayosukumwa na pampu za mkono

67

 

Hali ya upatikanaji wa maji katika halmashauri nzima ya Iringa ni 69.7%, idara inaendelea na juhudi mbalimbali ikiwa ni kuwashirikisha wadau katika kusaidia kuongeza hali hii ya upatikanaji wa huduma ya maji kufikia 85% ifikapo mwaka 2020.

CHANGAMOTO ZINAZOIKABILI IDARA

  1. Jamii kutotunza vyanzo vya maji na kuviharibu makusudi kwa shughuli zao binafsi.
  2. Upungufu wa wataalamu wa kutosha wa kusanifu, kutengeneza mitandao ya maji na mitambo ya kusukuma maji.
  3. Fedha za miradi kutofika kwa wakati na kupelkea kucheleweshwa kwa ukamilikaji wa miradi.

PICHA MBALIMBALI ZA MIRADI

     

Tanki la maji la Mradi wa Malinzanga              Mtego wa maji Mradi wa Malinzanga

   

Kituo cha maji Mradi wa Maji ya kisima                      Mashine ya kuchuja maji na kutoa maji safi na                                                                                 kinachosukumwa na nguvu ya umeme jua                 salama inayotumia nguvu ya umeme jua katika                                                                                                                       shule ya msingi Katenge                                                 kituo cha afya Kimande

             

Ujenzi wa tanki la juu  la maji  lenye ujazo wa                   Uwekaji wa mfumo wa umeme jua na                                                                                                                lita 150,000 la Mradi wa  maji Migoli Mtera                        uchimbaji mitaro na uwekaji mtandao wa maji                                                                                  ukiendelea

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa