• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

AFISA TEHAMA IRINGA DC AKIWASILISHA MADA YA MATUMIZI YA TEHAMA MAHALI PA KAZI KATIKA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Imewekwa : June 24th, 2022

Afisa TEHAMA Iringa DC: Tujiepushe na Matapeli wa Mtandao

Afisa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) Halmashauri ta Wilaya ya Iringa Ndugu Christopher Aron Mfugale amewataka Watumishi wa Halmashauri kuacha kutoa Nywira za akaunti za mifumo mbalimbali ya serikali amesema kufanya hivyo kunaweza kupelekea kuvuja kwa taarifa za serikali.

Changamoto zote zinazohusu masuala ya mfumo yanatatuliwa na Wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Iringa na si vinginevyo, amesisitiza kuwa mtumishi anapopata changamoto asikimbilie katika vibanda vya intaneti na badala yake awasiliane na ofisi ya TEHAMA Wilaya kwa wakati wowote ule.

Ameyasema hayo alipokuwa akiwasilisha mada ya Matumizi sahihi ya TEHAMA kwa Watumishi ikiwa ni siku ya pili ya Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika 25.06.2022, katika Kata ya Idodi, Shule ya Sekondari Idodi ambapo Watumishi mbalimbali kutoka maeneo tofauti tofauti Kata ya Idodi pamoja na wataalamu kutoka Makao Makuu wamekutana kuadhimisha wiki hiyo.

Amesema kuwa Watumishi wa Umma wana nafasi kubwa kwa jamii katika kuwaelimisha juu ya matumizi sahihi ya risiti, kudai na kutoa risiti pale unaponunua na kuuza kitu, bidhaa, huduma au rasilimali yoyote ile.

"Tunatakiwa tuwe wajumbe wazuri wa kufikisha hii elimu kwa wananchi hata kwa wakusanyaji wa mapato kutoka Halmashauri yetu, Kwani mapato yakiongezeka ndivyo maendeleo yatakavokuja katika Halmashauri yetu".

Amesema pia Serikali kwa sasa imekuja na mfumo mzuri na bora wa kupokea maoni, ushauri, kero, changamoto pamoja na pongezi kutoka kwa Watumishi na wananchi kuelekea kwa Taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.

Akifafanua amesema kuwa mfumo huu utarahisisha kuokoa gharama za nauli pamoja na muda ambapo hapo awali ilikuwa mpaka utoke katika kituo chako cha kazi na kwenda Makao Makuu ya Taasisi kwa ajili ya kuwasilisha tatizo au hoja yako kuhusu jambo fulani lakini kwa sasa huduma hii itapatikana kwa njia ya mfumo rasmi.

"Kuna njia mbili za kuingia katika mfumo huu, Njia ya kwanza ni kwa intanenti ambapo Mtumishi anatakiwa kuwa na simu janja pamoja na bando la intanenti ambapo ataingia katika kivinjari chake na kuandika emrejesho.gov.go.tz kisha atafuata maelekezo. Njia ya pili ni njia ya kawaida ambapo Mtumishi au Mwananchi atatakiwa kupiga *152*00# kisha kuchagua namba 9 kisha kuendelea. Huduma hii ni bure na inapatikana mitandao yote".

Aidha amewasisitiza watumishi wote kupenda kutembelea na kuhamasisha wananchi kufuatilia Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ili kujua taarifa zote zinazohusu Halmashauri zikiwemo shughuli za miradi inayopangwa kutekelezwa, iliyokamilika na inayoendelea. Pia taarifa na matukio mbalimbali ya Serikali huwa yanachapishwa huko.

"Nia ajabu kuona kuwa Mtumishi wa Halmashauru yetu hajui kuwa tuna tovuti ya Halmashauri wala mitandao ya kijamii, Ninawaomba muwe mnafatilia tovuti yetu ni www.iringadc.go.tz na pia Facebook ni Iringa Dc, Instagram ni Iringa_Dc mfuatilie na muwaambie na wenzenu ambao hawapo hapa".

Maadhimisho haya ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanatarajiwa kuendelea siku ya Jumatatu 27.06.2022 katika Tarafa ya Pawaga.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa