• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Baraza la Watoto Wilaya Lazinduliwa

Imewekwa : June 12th, 2024


Baraza la Watoto Wilaya Lazinduliwa

Hatimaye Baraza la Watoto limezinduliwa katika Halmashauri limezinduliwa ikiwa na lengo la kuwaleta watoto pamoja, kujadili matatizo yao na kuwajengea uwezo na ujasiri katika kila jambo.

Baraza hilo limezinduliwa Juni 10, 2024 katika Ukumbi wa Kanisa la Anglikana na kuchagua uongozi mpya baada ya uongozi wa awali kuisha muda wake.

Katika Hotuba yake ya ufunguzi wa uzinduzi wa Baraza hilo Mgeni Rasmi Mheshimiwa Stephen Mhapa ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri amesema, ameshukuru sana viongozi wa Mashirika kwa kuwezesha Baraza hili liundwe, na kushukuru uongozi wa Baraza uliopita kwa kuongoza vizuri katika kutekeleza  majukumu yao.

“Mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha hata akiwa Mzee”, Mheshimiwa Mhapa amenukuu maneno hayo kutoka katika Biblia Takatifu na kuwahusia wazazi watimize wajibu wao.

Naye Padre Emilyo Kindole ambaye ni Mlezi wa Baraza aliweza kutoa mafunzo mafupi kwa watoto na kuwahusia wazazi/walezi wasiwaumize wala kuwadhalilisha au kuwafanyia ukatili watoto. Pia amewaambia watoto kuwa wanapofanyiwa ukatili wanapaswa kusema kwa polisi, Mwenyekiti wa Mtaa, Afisa Maendeleo au kwa mtu anayemuamini ili aweze kupata msaada.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo Wilaya Bi. Saumu Kweka amewashukuru Wadau kwa kuandaa Baraza hilo na kusema kuwa, “Watoto mmeletwa hapa ili mjengewe uwezo wa kuwatetea watoto wenzenu. Hivyo mmechaguliwa ninyi ili muwe mfano na kuwaongoza watoto wenzenu kwenye kila jambo”.

Kupitia Baraza hilo, watoto walifanya uchaguzi wa uongozi na kupata Mwenyekiti Angel Robert Ng’anguli kutoka Kata ya Ulanda wa Shule ya Sekondari Kalenga Kidato cha Kwanza na Makamu wake Emanuel Nwenzi kutoka Kata yaa Migoli wa Shule ya Msingi Mtera Darasa la VI, Pia Katibu Natalia Sanga wa Kata ya Kihorogota wa Shule ya Msingi Isimani Darasa VII na Makamu wake Elisha Mfume wa Kata ya Itunundu wa Shule ya Sekondari Pawaga Kidato cha II, Kadhali Mtunza Hazina Jackline Mtove wa Kata ya Ifunda Shule ya Sekondari Lyandembela Kidato III na Makamu wake Resmida Mhangala wa Kata ya Maguliwa Shule ya Msingi Maguliwa Darasa la VII.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa